Kama upo Chini ya Miaka 45 hii inakuhusu

Kama upo Chini ya Miaka 45 hii inakuhusu

Smart Finance

Member
Joined
Apr 10, 2025
Posts
35
Reaction score
114
Nikiwa nipo zangu Mgahawani hapa kariakoo napata sharubati ya Maembe. Ng'ambo ya pili likapaki gari la mizigo na wabebaji (Makuli) wakafika na kuanza kazi ya kupakua ule mzigo.

Kile kitendo kilinifikirisha na kuibua wazo Fulani akilini mwangu. Kwanza Ile kazi (ya ubebaji mizigo) lazima watakuwa wameifanya Kwa muda mrefu, kwasababu kabla sijamaliza Sharubati yangu gari lote lilikuwa limeisha na kuondoka.

Sasa..

Leo hii wale wabeba mizigo Wana nguvu ya kuifanya Ile kazi. Vipi wakifikisha miaka 60+? Vipi kama wakiumwa na kukosa nguvu tena ya kufanya Ile kazi? Je wamejiandaa na kesho Yao?

Hilo swali nikajiuliza na Mimi pia. NIMEJIANDAA NA KESHO YANGU?

Leo Nina nguvu ya kufanya hichi nachofanya, kupata kipato; kesho Nikiwa Sina hizi nguvu nitaishije? Em jiulize pia Hilo swali kisha utafakari na majibu jipatie mwenyewe.


Kesho yetu inakuja, ipo njiani. Haiwahi Wala haichelewi. Ipo tu pale inasogea taratiiiiibu.

Hivi unajua jinsi ulivyo Sasa, Hali ya maisha uliyonayo Sasa ni matokeo ya yale uliyochagua kufanya mwenyewe hapo awali. Kwa Asilimia 75% sisi wenyewe ni responsible wa haya maisha tunayoishi.

Kama unaishi maisha mabaya, maisha magumu, usimtafute mchawi. Mchawi ni wewe mwenyewe.

Lakini pia kama unaishi maisha mazuri, maisha ya ndoto zako, usimtafute wa kumpongeza. Jipongeze wewe mwenyewe.

Good news ni kwamba hujachelewa, unayo nafasi ya kubadilisha kile unachoona hakifai. Maisha unayoishi huyapendi? Unayo nafasi ya kuyabadili.

ANZA LEO

Mabadiliko huanza kwako binafsi, Kaa chini tafakari. Nini hutaki? wapi ulikosea? Nini unataka? Ufanyaje kukipata?

Weka mifumo, jiwekee mikakati, jiwekee sheri na uanze kuzifata effectively.

Kwa Leo niishie hapo ila kesho nitapost mkakati madhubuti, wenye Uhalisia wa 100% unaoweza kuutumia kuitengeneza kesho Yako hata kama kipato chako ni kidogo Cha chini ya 300,000 Kwa mwezi. Usipange kukosa

Jiunge nasi Sasa Ili usipitwe na jambo hili:- Bonyeza linki hapo chini kujiunga - BURE

/channel/0029Vb4KXi3DjiOlFNeofA0w
 
Mkuu hatuishi kwa ajili ya kesho, mkipata afadhali kidogo ya maisha Huwa mnaanza kuwa na misemo na mawazo ya ajabu ajabu 😄. Ukitaka uone Mungu alivyo na nguvu kwetu njoo upime Imani yangu, hatuna uhakika hata wa Leo wewe umekaa na bando lako unazungumzia akiba ya kesho kweli???. Jitihada zipo na hatuna hofu kuhusu kesho...hata nguvu zikiisha kuna mlango utafunguka na amani itakuwepo kipindi nguvu ikishuka😂😂
 
Mkuu hatuishi kwa ajili ya kesho, mkipata afadhali kidogo ya maisha Huwa mnaanza kuwa na misemo na mawazo ya ajabu ajabu 😄. Ukitaka uone Mungu alivyo na nguvu kwetu njoo upime Imani yangu, hatuna uhakika hata wa Leo wewe umekaa na bando lako unazungumzia akiba ya kesho kweli???. Jitihada zipo na hatuna hofu kuhusu kesho...hata nguvu zikiisha kuna mlango utafunguka na amani itakuwepo kipindi nguvu ikishuka😂😂
Sawa
 
Unaongelea kesho ili hali takribani raia wote hawaijui leo yao; mfano hao makuli n.k
 
Back
Top Bottom