Nimetoka kuongea na Customer care Tanesco (kwa simu namba 0732 979280) kuhusu mgao mpya wa umeme cha kusikitisha jamaa anaongea huku akicheka kuwa sehemu kubwa ya Arusha haitakuwa na umeme kabisa mchana kwa majuma kadhaa..(sishangai kwani sakina kuanznia j'pili hatuna umeme) nilipomuuuliza mpaka lini akasema Mungu ndo anajua....sasa najiuliza hilo jibu maana yake ni nini wakati rais ni juzi ameingiza kampuni ya Kimarekani kuzalisha umeme....au ile kampuni ni kanyaboya wahusika wanaendelea na ishu nyingine? Jamani tutaishije tunaochomelea....wafugaji wa kuku...wauza samaki wabichi.....internet cafe......saloon sawmill mashine za kusaga.....hii mbona ni kama kukomoana?