Son of Gamba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2012
- 4,358
- 6,077
Mafanikio makubwa hapa duniani ni kwa mtu kuupata UFALME WA MUNGU. Hakuna mafanikio yoyote zaidi ya hayo. Hata kama utakuwa na pesa na mali kuwazidi akina Ellon Mursk, Bill Gates, Mark Zuckerberg n.k. kama hujaupata UFALME WA MUNGU wewe bado hujafanikiwa na unaishi maisha ya hasara.
Hata kama utakuwa na elimu ya juu na maPHd na madegree ya kila namna, kama jina lako halipo kwenye UFALME WA MUNGU, wewe bado hujafanikiwa.
Amini nakwambia ukiupata UFALME WA MBINGUNI basi wewe umefanikiwa tayari maana vyote vinaharibika na kupita, mali na pesa na elimu ya dunia utakufa na kuviacha. Lakini UFALME WA MUNGU ni wa milele.
Jambo la muhimu kufahamu ni kwamba tupo hapa duniani ili tujifunze kwa bidii sana namna ya kuupata UFALME WA MUNGU, na tuutafute UFALME huo kwa bidii sana kuliko kitu chochote kile. Maisha ya duniani ni kama "chuo" au "shule" ya kujifunza namna ya kuupata na kuishi katika UFALME WA MUNGU. Hayo mambo mengine ya utajiri, mali na mapesa ni kikwazo tu ili Wanadamu wasahau lengo la wao kuwepo hapa duniani.
Sisemi watu wasifanye kazi, hapana, tufanye kazi lakini cha muhimu kuliko vyote kwanza ni kuutafuta UFALME WA MUNGU kisha hayo mengine yatafuatia baadaye.
Wachache sana wataelewa nimeandika nini.
Hata kama utakuwa na elimu ya juu na maPHd na madegree ya kila namna, kama jina lako halipo kwenye UFALME WA MUNGU, wewe bado hujafanikiwa.
Amini nakwambia ukiupata UFALME WA MBINGUNI basi wewe umefanikiwa tayari maana vyote vinaharibika na kupita, mali na pesa na elimu ya dunia utakufa na kuviacha. Lakini UFALME WA MUNGU ni wa milele.
Jambo la muhimu kufahamu ni kwamba tupo hapa duniani ili tujifunze kwa bidii sana namna ya kuupata UFALME WA MUNGU, na tuutafute UFALME huo kwa bidii sana kuliko kitu chochote kile. Maisha ya duniani ni kama "chuo" au "shule" ya kujifunza namna ya kuupata na kuishi katika UFALME WA MUNGU. Hayo mambo mengine ya utajiri, mali na mapesa ni kikwazo tu ili Wanadamu wasahau lengo la wao kuwepo hapa duniani.
Sisemi watu wasifanye kazi, hapana, tufanye kazi lakini cha muhimu kuliko vyote kwanza ni kuutafuta UFALME WA MUNGU kisha hayo mengine yatafuatia baadaye.
Wachache sana wataelewa nimeandika nini.