Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

2010 nipo ndani ya fuso, natokea Ifakara kwenda dsm. Kufika Maseyu mida kama saa 8 usiku dereva akapaki, akasema amechoka anapumzika kidogo. Akatuambia saa 10 tumwamshe tuanze safari.

Sijui kama ni uchawi au ni nini, tulipitiwa na usingizi mzito, na wote, tulikuwa watatu tuliota ndoto ya aina moja. TUNAPIGA MECHI. tumejipiga mabao wote, kuangali saa ni dk 20 tu zimepita. Nilichowaeleza wenzangu ndio walichoota. Mwanamke niloyeota namgonga ndio huyo huyo wenzangu walikuwa wakiota wanamgona.

Niliota vipele vya baridi kwa uoga. Tukaondoka kuendelea na safari. Tangu siku hiyo sipandi tena malori ya mzigo yanayosafiri usiku.



Sent from my SM-G570F using Tapatalk
Mliota mnamla dereva au

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nishawahi sikia kisa kinschohusishwa na uchawi

Kuna masela wawili walienda kwa mganga ili wapate utajiri

Mganga akawapa dawa akawaambia wakaoge usiku makaburini na wakitoka mlangoni kwa mganga hawatakiwi kugeuka nyuma

Basi unaambiwa safari yao iliandamwa na misukosuko yakutisha, mara wasikie muungurumo wa simba akiwa nyuma yao na vimbwenga vingi lakini walijitahidi kukaza ili kutovunja sharti la kugeuka nyuma

Sasa ulipofika usiku majira ya saa 8 ikabidi waende makaburini kuoga ili kumalizia zoezi lao la mwisho ili wawe mamilionea

Walipofika makaburini wakavua nguo wote nakubakia uchi kisha wakapanda juu ya kaburi ili waoge

si unajua ukiwa katika ile mood flani hivi unaoga halafu umefumba na macho ili maji yasiingie machoni.

wakastukia tu paap! wameshikwa makalio kwa nyuma.

Aaah unaambiwa wote ilibidi wageuke nyuma kwa haraka huku wanakimbia na kupiga makelele

Kesho yake kijiweni wakaanza kulaumiana "aaah wewe ndiye ulizingua, we ungekausha bila kupiga mikelele mi nisingechochora kwani kushikwa tako kitu gani bwana" yani leo nisingekua nakunywa kahawa hapa ningekua nimejikoki huko kwenye hotel zinazotambulika na dunia"
Kushikwa Tako ni Maandalizi ya Kusukumiwa Mkuyenge.. Jamaa ni Haki Walale Mbele.
 
Kisa kingine nilikisikia kilitokea maeneo ya sumbawanga

Kuna mzee wamakamo alikua ni tajiri sana, pesa zake haweki benk na hata akienda kufanya manunuzi hua haweki kwenye wallet kuzistiri zisionekane yeye hua anazishikilia tu kama wanafunzi wanavyoshika vitini vyao mikononi

Siku moja kuna kosi la majambazi lilijipanga kwenda kumvamia

Walimkuta yuko nyumbani kwake ameshikilia pesa akipata upepo kwenye garden yake

Wakamnyooshea bastola na kumwambia atulie kimya kisha atoe kila kitu alichonacho

Yule mzee akachukua zile pesa akazibana kwenye kwapa lake huku akitetemeka kwa woga

majambazi wakamsisitiza kua anyanyue mikono juu, mzee akatii amri kwa kunyanyua mikono juu kisha pesa alizozibana kwapani zikaanguka chini majambazi wakaziokota

Wakamwambia tena "toa kila kitu ulichonacho"

Round hii unaambiwa mzee alichomoa kichwa chake akakishika mkononi halafu kile kichwa kikiwa mkononi kikatoa sauti ikisema "sina chochote jamani nina kichwa tu hapa"
Hapo ni kutimua mbio tu mamaa nakufaaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna ofisi niliajiriwa miaka mingi kidogo nyuma. Hapo nilipofika sababu ya uchangamfu wangu walinzi walinizoea na kunifungukia mambo yanayofanywa hapo na kunitahadharisha ikiwemo baadhi ya Managers kuchinja mbuzi (kafara) usiku kukiwa hakuna staff hata mmoja.

Haikupita mwezi nikaanza kuumwa kichwa cha ajabu na kutetemeka! Kila nikipima tatizo halionekani na nikipata nafuu kidogo nikakanyaga ofisini kinaanza upya!

Tukaona na wife hapa tuingie kwenye spiritual warfare na kushirikisha waombaji. Siku nimefanyiwa maombi nilikuwa na hali mbaya zaidi lakini baada ya maombi ya nguvu nilitoka jasho jingi na kichwa kikakoma pale pale kuuma!

Mtumishi akanishauri nisikanyage ardhi ya ofisi bila kujifunika kwa damu ya Yesu, ndio imekuwa desturi yangu hadi leo sigusi ardhi ya ofisi bila kujifunika kwa damu ya Yesu na nikiingia ofisini nachukua kitabu cha mawaridi ya sala na kusali kabla ya kazi!

Uchawi upo na shetani yupo kazini kwelikweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
Afadhali wewe umetoa solution ya kumtukuza mwana wa Mungu, naona wengi huku solution zao ni kwenda kwa waganga wa kienyeji ambao wanatumia majini kuwaponya, ni vyema na inapendeza watu tumkumbuke, kusimama, na kuishi na Mungu wa kweli, tuwe na imani isiyo na mashaka juu ya uweza wake. Tusali na kumuomba yeye, watu waache kuitegemea kuzimu kutimiziwa mahitaji yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee baba uko siriaz au unatania? maana hata mie nilikuwaga siamini mambo ya kusikia, Nakumbuka siku moja nipo chuo nakula msuli kimbweta jamaa alinifata akidai hajala tangu usiku wa siku moja kabla ya jana( nimekutana nae jumatano mchana halafu akasema hajala tangu alipokula usiku wa jumatatu), nikaona kama ananipanga tu nikampa buku 2 akasepa. Ila nilikuja kufulia kuna kipindi nikawa nakoroga uji tu geto nakunywa asubuhi afu navunga mpaka usiku tena, ilifikia kipindi nikawa tena sioni haja ya uji navunga tu tangu asubuhi mpaka usiku napiga maji tu ya dawasco, ndo nikajua hakuna jipya chini ya jua.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah! Hivyo mlitumiwa!!hahahaaaa!!! Huyo mchawi alikuwa na kiu sana. Uzuri mituko chenu mlienjoy haina shida
2010 nipo ndani ya fuso, natokea Ifakara kwenda dsm. Kufika Maseyu mida kama saa 8 usiku dereva akapaki, akasema amechoka anapumzika kidogo. Akatuambia saa 10 tumwamshe tuanze safari.

Sijui kama ni uchawi au ni nini, tulipitiwa na usingizi mzito, na wote, tulikuwa watatu tuliota ndoto ya aina moja. TUNAPIGA MECHI. tumejipiga mabao wote, kuangali saa ni dk 20 tu zimepita. Nilichowaeleza wenzangu ndio walichoota. Mwanamke niloyeota namgonga ndio huyo huyo wenzangu walikuwa wakiota wanamgona.

Niliota vipele vya baridi kwa uoga. Tukaondoka kuendelea na safari. Tangu siku hiyo sipandi tena malori ya mzigo yanayosafiri usiku.



Sent from my SM-G570F using Tapatalk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
2010 nipo ndani ya fuso, natokea Ifakara kwenda dsm. Kufika Maseyu mida kama saa 8 usiku dereva akapaki, akasema amechoka anapumzika kidogo. Akatuambia saa 10 tumwamshe tuanze safari.

Sijui kama ni uchawi au ni nini, tulipitiwa na usingizi mzito, na wote, tulikuwa watatu tuliota ndoto ya aina moja. TUNAPIGA MECHI. tumejipiga mabao wote, kuangali saa ni dk 20 tu zimepita. Nilichowaeleza wenzangu ndio walichoota. Mwanamke niloyeota namgonga ndio huyo huyo wenzangu walikuwa wakiota wanamgona.

Niliota vipele vya baridi kwa uoga. Tukaondoka kuendelea na safari. Tangu siku hiyo sipandi tena malori ya mzigo yanayosafiri usiku.



Sent from my SM-G570F using Tapatalk
Uliliwa kimasihara!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom