Kama nimeimbiwa mimi!

Kama nimeimbiwa mimi!

Slim5

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
28,374
Reaction score
38,248
Kuna baadhi ya nyimbo za bongo fleva huwa nikiziskiliza najihi kama msanii husika aliniimbia mimi, yaani inatokea wimbo unanigusa moja kwa moja! Nyimbo zifuatazo huwa zinarandana na nyakati tofauti tofauti za maisha yangu:

Mwambieni nampenda (baba uko wapi?) by Q-chief
Huu wimbo huwa unanigusa moja kwa moja na hasa katika maneno yanayotengeneza ujumbe ambayo Q chilla aliyatumia hapa! Huwa Nakumbuka namna maisha yangu yasivokuwa na historia chanya kumhusu baba!

Ningekusamehe by 20% & Mama Halima by Linex:
Kipindi fulani, hata sijui ilikuwaje! Ikatokea kumpenda binti mmoja, japo hakuwa mzuri wa kiviile, lakini alikuwa na moyo wa upendo ambao kwa binadamu wa kawaida lazima ange-appreciate! Katika hali ambayo hata sikuelewa, alikuja kubeba mimba ya mtu mwingine nikiwa chuo mji mwingine, akahama na mji, akaenda kuolewa, akapotea jii! 10 years later nikaja kubambana nae FB!

Mkuki moyoni ba Afande sele, Mapito by Lord eyez & Nishike mkono by Darasa:
Hizi kwangu ni bonge la historia! Maisha ya ki-gangstar niliyoishi nikiwa o-level yanafanya nizipende sana hizi ngoma! Kipindi kigumu sana cha utoto kilinipitisha katika nyufa nyingi za hatari. Kuna wakati ukinambia nisimulie namna gani nimefika hapa huwa sina maelezo ya moja kwa moja! Nimeshachomwa sana na mkuki moyoni! Niliitaji sana kushikwa mkono na si tu sikuwa na mtu wa kunishika mkono bali pia nilikuwa sivutii kushikwa mkono!


Kwa kuwa wasanii na sanaa ni mali ya jamii, najua hata wewe kuna ambazo zimekugusa na kama si kwa masika huenda ni kwa kiangazi ama vuli! Tupia zipi na za kina nani!
 
Marlow~Ritha huu wimbo nikiusikia sehemu unapigwa huwa unanikumbusha mbali sana enzi za ujana nikiwa nakula ujana/dah!ama kweli ujana ni maji yamoto!!
 
 
Last edited by a moderator:
hahaha, Bushoke umekumbuka nini

Fitina za wahaya wa ile radio zimemkimbiza Bushoke! Daah jamaa bonge la msanii, bonge la kipaji! Yupo J'berg kwa babake, namkubali sana Bushoke!
 
..."mimi nitawaeleza" maneno haya yapo kwenye wimbo wa sedekia(marehemu) kwenye album ya kwanza. Huwa yananigusa sana,pamoja na nyingine nyingi sana...
 
Zoba by banana zorro
i hate this song at all
when i listen it i fell pain dah...,,,,!!
 
mtegemee yesu_ambassadors of christ. naupenda tu ila haunikumbushi ki2
Mkuu sio kukumbusha rejea kichwa cha habari Kama nimeimbiwa mimi

Hata wimbo utakaotoka mwaka 2015, 2016 na kuendelea au kifupi nikuambie yale maneno ya kwenye wimbo yanakuwa kama kuna ukweli kuhusiana na wewe
 
Halo by beyonce unanihusu sana siku hizi.
cc; daktari
 
Good Girls By Joe Thomas......unanikumbusha mbali sana......
 
Happy home ya 2Pac - huwa inanipeleka mbali sana yaani haya maisha haya basi tu.
 
Kuna baadhi ya nyimbo za bongo fleva huwa nikiziskiliza najihi kama msanii husika aliniimbia mimi, yaani inatokea wimbo unanigusa moja kwa moja! Nyimbo zifuatazo huwa zinarandana na nyakati tofauti tofauti za maisha yangu:

Mwambieni nampenda (baba uko wapi?) by Q-chief
Huu wimbo huwa unanigusa moja kwa moja na hasa katika maneno yanayotengeneza ujumbe ambayo Q chilla aliyatumia hapa! Huwa Nakumbuka namna maisha yangu yasivokuwa na historia chanya kumhusu baba!

Ningekusamehe by 20% & Mama Halima by Linex:
Kipindi fulani, hata sijui ilikuwaje! Ikatokea kumpenda binti mmoja, japo hakuwa mzuri wa kiviile, lakini alikuwa na moyo wa upendo ambao kwa binadamu wa kawaida lazima ange-appreciate! Katika hali ambayo hata sikuelewa, alikuja kubeba mimba ya mtu mwingine nikiwa chuo mji mwingine, akahama na mji, akaenda kuolewa, akapotea jii! 10 years later nikaja kubambana nae FB!

Mkuki moyoni ba Afande sele, Mapito by Lord eyez & Nishike mkono by Darasa:
Hizi kwangu ni bonge la historia! Maisha ya ki-gangstar niliyoishi nikiwa o-level yanafanya nizipende sana hizi ngoma! Kipindi kigumu sana cha utoto kilinipitisha katika nyufa nyingi za hatari. Kuna wakati ukinambia nisimulie namna gani nimefika hapa huwa sina maelezo ya moja kwa moja! Nimeshachomwa sana na mkuki moyoni! Niliitaji sana kushikwa mkono na si tu sikuwa na mtu wa kunishika mkono bali pia nilikuwa sivutii kushikwa mkono!


Kwa kuwa wasanii na sanaa ni mali ya jamii, najua hata wewe kuna ambazo zimekugusa na kama si kwa masika huenda ni kwa kiangazi ama vuli! Tupia zipi na za kina nani!

pole sana sanaaaa kaka,yan nmesoma ulichoandika na nmeumia sana,nafurah kuona pamoja na yote stil unasonga mbele..maisha yana mitihani mingi lakin pia tumewekewa na njia ya kushinda japo mapambano ni makali,nakuombea maumivu yako yaaje kubeba furaha na kusahau yote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom