Kama ndio wewe basi nimepata aliyebora

Sammy1961

JF-Expert Member
Dec 23, 2019
298
303
Ilikuwa siku ya jumamosi nikiwa sina hili wala lile, nikasema acha nishike simu niingie kwenye contact list yangu mana kuna upwiru ulikuwa unanikaba koo.

Baada ya kushusha shusha nikakutana na number yake Jesca, huyu dada alikuwa akitesa sana akili yangu siku nyingi nilikuwa nakesha nikimtafuta mpaka usiku wa manane lakini alikuwa akijibu message zangu kifupi.

Huyu alifanya nipate maumivu makali yaliyoitafuna akili yangu na kuufanya moyo usinyae pale tu ntakapolikumbuka jina lake.

Lakini hii siku sasa nikasema acha nijinywee walau Safari Lager kadhaa nilipozimaliza ndio akili ikaelekea katika kushusha number za simu kwenye simu yangu.

Number ambazo niliapa kutofuta hata nini kitokee, mana alishakuwa akizunguka kwenye barabara ya ubongo wangu kila wakati, nikiwa na imani iko siku atakubali ombi langu.

Sasa baada ya kuona number yake ilibidi nianze tena upya kumweleza jinsi gani nilikuwa nikimuwaza na natamani awe mtu wa muhimu kwenye maisha yangu.

Mwamba nikajitusua huku nishafikisha chupa kadhaa za Safari Lager.

Nikamtext mida kama ya saa sita usiku hivi bahati nzuri huyu mlimbwende alikuwa bado hajalala.
Mimi: Jesca mambo
Jesca: Poa, vipi.
Mimi: Safi kabisa, za masiku mengi.
Jesca: Nzuri tu, nani mwenzangu?
Mimi: Jamani Kumbe ulishafuta na number zangu ?
Jesca: Ndio number za nini na sina mawasiliano na wewe?
Mimi: Ahaa, basi mimi ni Kijana Mpole naamini utakuwa umenikumbuka.
Jesca: Aaaah jamani, samahani sana Kijana ndio nishakukumbuka.
Mimi: Sawa, naomba kidogo kesho tutawasiliana.
Jesca: Sawa, usijiskie vibaya lakini.
Mimi: Usijali.
Jesca: Usiku mwema.
Mimi: Na kwako pia, ulale salama.
 
Sasa baada ya kumtafuta ule usiku alikuwa tayari kashafuta number zangu kisa niliacha kuwasiliana naye, hii ilipandisha zile Safari Lager kichwani ndio maana nikakatisha maongezi na yeye.

Kesho yake niliamka nikiwa vizuri kichwa kimeshaisha pombe, nilienda kwa Mama Gee nipate japo Breakfast kwa sababu ilikuwa Jumapili iyo sikwenda kanisani juu ya uchovu wa zile Safari kwaiyo sikuweza kuamka nihudhirie ibada ya kwanza.

Baada ya kumaliza, basi nikajikalia kwenye kochi langu hapa nyumbani nikasema acha nimtafute tena jesca.

Mimi: Jesca, habari yako.
Jesca: Salama Kijana Mpole, vipi.
Mimi: Safi kabisa.
Jesca: Mbona ni saa tatu hujaenda kanisani?
Mimi: Ndio leo sijaenda, nimeamka nna uchovu sana pia nilichelewa jana si uliona mda nimekutext saa sita usiku?
Jesca: Aah, hii kweli niambie Kijana.
Mimi: Naona number yangu isharudi tena kwenye list yako .
Jesca: Ndio, mimi huwa sikai na number za watu sana kama hatuna mawasiliano.
Mimi: Aah, hiyo ni nzuri sema mimi nlishtuka jana baada ya kuniuliza wewe nani.
Jesca: Sasa ulishtuka nini?
Mimi: Nilijuwa hapa nikileta mlolongo ntakula matusi.
Jesca Wala hata, sasa kijana kuna kazi natakiwa kuifanya hapa.
Mimi: Sawa hamna shida baadae.
Jesca: Sawa.
 
Baada sasa ya kuona nimerudisha mawasiliano na yeye, nilianza kutafuta mawasiliano ya rafiki zake wa karibu ili niweze kujua namna gani ntaweza kumwambia jinsi gani anavyoivuruga akili, jinsi nilikuwa nikimuwaza siku zote.

Nilifanikiwa kupata namba za rafiki yake anaitwa Brenda, yeye niliweka ukaribu nae ili nipate kujua zaidi kumuhusu Jesca ni anapenda nini hapendi ili nisije kufanya mistake nilifanya mwanzo.

Kwaiyo Brenda tuliwasiliana mda kama miezi kadhaa mbele huku nikiwa nawasiliana na Jesca pia nikiwa namjulia hali, nayeye tulishaweza kuzoeana.

Sasa siku moja ikabidi nimuulize Brenda maswali yanayo muhusu Jesca, nayo ilikuwa hivi.

Mimi: Brenda rafiki yangu.
Brenda: Abee.
Mimi: Mambo
Brenda: Poa vipi Kijana
Mimi: Safi kabisa, umeshindaje.
Brenda: Salama tu, niambie rafiki yangu.
Mimi: Leo nataka nikuulize kitu kuhusu Jesca.
Brenda: Hee mbona gafla sana .
Mimi: Eeh nataka kufanya kitu, utaniambia?
Brenda: Sawa usijali.
Mimi: Hivi unaweza kuniambia Jesca huwa anapenda vitu gani na ni vitu gani ukifanya kama mtu wake wa karibu anaweza kukuchukia maisha yake yote, wewe si rafiki yake kipenzi .
Brenda: Bwana bwana, ngoja nisisema vingi ila kwa Jesca yeye vitu anapenda ni mtu awe anamindset nzuri hawazi kinyume pia anapenda mtu anayependa maendeleo na vitu ambavyo hapendi ni mtu mbabaishaji hapendi kona kona ukiwa mtu wa kona kona anaweza akakuchukia siku zote na usiweze kumrudisha kwenye hali yake ya kawaida. Ni ivyo Rafiki yangu.
Mimi: Asante sana Brenda .
 
Basi mimi baada ya kupata hicho kwa kifupi kutoka kwa Brenda, nilianza sasa kuongea na Jesca kuhusu swala langu nilililotaka kumwambia.

Sasa nikaanza mawasiliano na Jesca, kipindi hiki ilibidi niwe namtafuta kwa umakini mkubwa ili nisije nikazingua tena.

Mawasiliano yalizidi kutaradadi tukawa sasa tunatoka mpaka out kwenda kwenye movie (cinema), yaani kiufupi urafiki wetu ulienda mbali sana kiasi cha Jesca kuanza kuniamini.

Kuna siku alikuwa amepata shida nyumbani kwao, mama yake alikuwa anaumwa ilibidi aniambie basi na mimi bila kuwa na shaka nilimwambia nyumbani ni wapi?

Jesca aliniambia nyumbani ni Tarakea, Rombo.

Mimi bila kusita nilienda nikafanyia gari service ili sasa tutoke Arusha kwenda kwa mama yake Jesca Rombo, safarini tulikuwa tukipiga stori kadhaa ili kuondoa uchovu wa mimi kutokulala, na kipande cha stori kilikuwa hivi.
 
Jesca: Hivi huwa mnawezaje kuendesha gari umabli mrefu hivi?
Mimi: Inabidi tu uzoee mana tayari ishakuwa sehemu ya maisha yetu.
Jesca: Hahaha, kwaiyo wewe ulianza kuendesha gari mwaka gani mana unaonekana dereva mzuri sana.
Mimi: Gari sina muda mrefu sana, ila nazingatia tu sheria za barabara.
Jesca: Sawaa, aya nenda speed ya kawaida mana unakimbiza tusije tukashindwa kumuona mama.
Mimi : Usiwe na shaka, ntaenda mwendo wa kawaida.

Basi vaada ya masaa manne kupita tulikuwa tumeshafika nyumbani kwa kina Jesca kweli mama yake alikuwa anaumwa japo sio sana ilikuwa tu mchafuko wa damu mwilini.

Basi tulitoka nyumbani tukaenda mpaka hospitali ya karibu mama akapatiwa matibabu na nilimwambia Jesca acha pesa ya matibabu ntagharamikia.

Mama alipatiwa matibabu, akapewa na dawa matibabu hayakuwa ya bei ya juu sana ila mama aliweza kupata utabibu. Mimi ilibidi niwarudishe mpaka nyumbani ili nirudi Arusha.

Jesca alisema anabaki nyumbani kwao ili aendelee kukaa na mama mpaka apone.

Sasa hapa nilivyofika Arusha.
 
Ilikuwa siku ya ijumaa Jesca akiwa bado yupo kwao Rombo, ilibidi iyo siku nijitutumuwe nimwambie kuwa natamani awe mke wangu wa maisha.

Basi nikavuta simu kutoka mfuko wa suruale yangu.

Maongezi yakawa kama hivi.

Mimi: Jesca, habari yako.
Jesca: Poa, habari yako Kijana Mpole.
Mimi: Niko salama kabisa, vipi nyumbani wazima? Mama je anaendeleaje.
Jesca: Mama anaendelea vizuri kabisa pia nyumbani hawajambo.
Mimi: Basi ni jambo la kheri, leo nilikaa hapa nikasema ni muda umepita na nlikuacha na mgonjwa.
Jesca: Hata usiwe na shida Kijana, ila asante sana.
Mimi: Asante ya nini tena?
Jesca: Umefanya kitu sitaweza kukusahau.
Mimi: Usiwe na shida, ila leo kuna kitu nataka kukwambia.
Jesca: Kitu gani icho?
Mimi: Utakubali?
Jesca: Wewe niambie ni kitu gani kwanza.
Mimi: Jesca unajua toka zamani nlikuwa nikikutumia message za kukuomba tuwe japo wachumba, ila uliniambiaga bado haupo tayari gafla nikapoteza mawasiliano na wewe?
Jesca: Ndio nakumbuka, kwaniyo leo unataka kuniambia nini tena?
Mimi: Leo sasa nataka nirudie kauli yangu ile ya zamani lakini sasa awamu hii sitaki tuwe tena wachumba mana naona ni kama umri umeenda kidogo.
Jesca: Unataka tuwe kina nani Kijana?
Mimi: Nataka Mungu akijaalia tuwe mume na mke mana, niwe direct maana nshaambiwaga na rafiki yako Brenda hupendi kona kona.
Jesca: Mmmmh! Mbona imekuwa gafla sana.
Mimi: Hapana sio gafla imebidi niseme kike kitu nataka nisiwe mbabaishaji.
Jesca: Basi ngoja nifikirie, nikirudi Jumapili tutaongea vizuri.
Mimi: Sawa, acha nisubiri ombi lako. Basi ubaki salama pia wasalimie nyumbani.
Jesca: Sawa, siku njema Kijana.
Mimi: Asante.
 
Basi baada ya kumwambia hivi ni kama akili sasa ilikuwa sawa.

Ila mpaka nafika hii hatua ya kuumwambia ile kauli, nilishatafuta ushahidi kama miezi kadhaa hivi (miezi 10+) kama kweli alikuwa hana hata boyfriend kwa pale mtaani, ambapo hiyo nayo nilimuuliza Brenda.

Brenda alikuwa anasita sita kuniambia ila kuna siku alinambia bana huyu yuko single mda mrefu na wala huwa hanipi story za vijana wanaomsumbua.

Lakini kuna siku nliskia akinipa, story zako hata ulivyoenda kwao kaniambia alinambia kati kati ya hii week na akasema wewe uko na roho nzuri sana ila kama unataka kweli kutoka nae bora umwambie mapema ndege asije akapeperuka.

Ndio ilibidi sasa nimwambie ili nijuwe moja.

Sasa jumapili alirudi na alivyorudi tu akaniambia kasharudi sema ilikuwa jioni nikasema acha ntamtafuta siku nyingine hata ijumaa inayofuta mana kati kati ya week inakuwaga ni vigumu mana kuna kupambana na majukumu siku hiyo sikumkumbusha chochote.

Ila niliweza tu kumtumia message nikimpa pole kwa uchovu wa safari na kuwasiliana kwa namna ya kawaida tu katika hiyo week.

Siku zikasonga muda nao ukawa unakimbia kweli kweli hiyo week .
 
Ilifika ijumaa hata sikufahamu imefikaje.

Ilikuwa mida ya saa nne asubuhi nikamcheck Jesca nikiwa niko ofisini, nikimuomba kama atakuwa na muda siku iyo tuende mahali tukaongee alikubali.

Basi saa saba nilitoka mishe mitaa ya Unga Limited mpaka Ngaramtoni, kwakuwa ilikuwa ijumaa na ni mchana barabara za ndani ya mji zilikuwa zishaanza kuwa na foleni basi mimi nlitoka moja kwa moja nikapita East Afrika Road moja kwa moja hadi ngaramtoni.

Nilienda kuangalia wapi naweza kwenda kukaa na Jesca ambayo atajiskia kidogo yupo huru, akili ikaja kichwani moja kwa moja nikasema ngoja niangalie sehemu ambayo kutakuwa na sauti za ndege na wadudu pamoja na maji yanayotiririka ndio ziwe kelele pekee tukae tuongee.

Nilipo maliza kuwaza nikamwambia Jesca saa kumi ndio tutaenda sehemu.
 
Ilikuwa siku ya jumamosi nikiwa sina hili wala lile, nikasema acha nishike simu niingie kwenye contact list yangu mana kuna upwiru ulikuwa unanikaba koo.

Baada ya kushusha shusha nikakutana na number yake Jesca, huyu dada alikuwa akitesa sana akili yangu siku nyingi nilikuwa nakesha nikimtafuta mpaka usiku wa manane lakini alikuwa akijibu message zangu kifupi.

Huyu alifanya nipate maumivu makali yaliyoitafuna akili yangu na kuufanya moyo usinyae pale tu ntakapolikumbuka jina lake.

Lakini hii siku sasa nikasema acha nijinywee walau Safari Lager kadhaa nilipozimaliza ndio akili ikaelekea katika kushusha number za simu kwenye simu yangu.

Number ambazo niliapa kutofuta hata nini kitokee, mana alishakuwa akizunguka kwenye barabara ya ubongo wangu kila wakati, nikiwa na imani iko siku atakubali ombi langu.

Sasa baada ya kuona number yake ilibidi nianze tena upya kumweleza jinsi gani nilikuwa nikimuwaza na natamani awe mtu wa muhimu kwenye maisha yangu.

Mwamba nikajitusua huku nishafikisha chupa kadhaa za Safari Lager.

Nikamtext mida kama ya saa sita usiku hivi bahati nzuri huyu mlimbwende alikuwa bado hajalala.
Mimi: Jesca mambo
Jesca: Poa, vipi.
Mimi: Safi kabisa, za masiku mengi.
Jesca: Nzuri tu, nani mwenzangu?
Mimi: Jamani Kumbe ulishafuta na number zangu ?
Jesca: Ndio number za nini na sina mawasiliano na wewe?
Mimi: Ahaa, basi mimi ni Kijana Mpole naamini utakuwa umenikumbuka.
Jesca: Aaaah jamani, samahani sana Kijana ndio nishakukumbuka.
Mimi: Sawa, naomba kidogo kesho tutawasiliana.
Jesca: Sawa, usijiskie vibaya lakini.
Mimi: Usijali.
Jesca: Usiku mwema.
Mimi: Na kwako pia, ulale salama.
Tatizo linaanzia hapo kwenye kijana mpole
 
Binafsi nlichagua kwenda THEMI GARDEN, hii ipo maeneo kama unaelekea Njiro na ilikuwa ni majira ya jioni kama saa 10:30 hivi foleni hapa ndio imeshika magari kuelekea moshono, kijenge, njiro, kwa msola yanapita hiyo hiyo njia.

Basi nikaweka sawa baja langu (pikipiki) ilikuwa ni XLR Honda pikipiki kutoka Japan, ilikuwa na Mileage 9,950, 250cc nilichukua used kutoka huko kwa wajapani miezi kadhaa iliyopita.

Ilipokuwa sawa nilihakikisha helmet ziko mbili pia vya kujikinga ili hata ikitokea ajali tusiumie sana, niliwasha baja langu nikaenda mpaka alipokuwa anakaa Jesca kibanda maziwa nilikuta kashajiandaa, tulienda moja kwa moja huku baja linapiga kelele njia nzima mpaka THEMI GARDEN.

Kiukweli Jesca alifurahia kuona ile sehemu, kwani hajawahi kutolewa out akapelekwa sehemu kama ile, alifurahi sana.

Naomba niweke story iwe fupi mana stori ni ndefu kweli kweli .

Tulikaa pale tukala tukapata na juice ya matunda kutoka vilikuwa vinatengenezwa vyote, tukaongea story nyingi ikafika jioni saa kumi na mbili giza likaanza kuzama

Lakini niliona kuna picha moja kwa wale wachoraji waliopo pale THEMI GARDEN, ilikuwa ni picha ya simba dume anapigana na madume wengine watatu (Vita kama ile ya Bon Junior), yule simba alikuwa anamlinda Simba jike alikuwa yupo nyuma yake asikaribiwe na wale simba watatu nilimnunulia Jesca akapendezeshe chumbani kwake.

Lakini Jesca akanikimbusha kuhusu swala nililomwambia kuwa natakaa awe mke wangu wa maisha, ile siku alikubali akasema sawa nimekubali kuwa mke wako pia mama wa watoto wako, baada ya kusema hivi aliongea maneno kadhaa.

Nanukuu "KAMA NDIO WEWE BASI NIMEPATA ALIYE BORA"

Kama umefika mpaka hapa mwisho umeonaje stori mkuu .

Weka comment yako, kuna sehemu ya pili naandika tena.
 
Back
Top Bottom