T14 Armata
JF-Expert Member
- Mar 7, 2017
- 13,289
- 44,739
Asubiri aone
Huyo Muiran ana IQ kubwa na yupo mbele ya muda kuliko hao washamba mnaowategemea. Of course simkubali, ila hilo halinizuii kuona alivyo smart kwenye uovu wake.Awamu hii mchezo uko tofauti mzee
Yupo tangu enzi Lowassa na Kikwete ni marafiki, Lowassa kajiuzuru umemsikia Rostam anatikisika? Kikwete kastaafu kaja mtu mwingine completely umeona Rostam anapotea? Kaja Hangaya umeona Rostam anafifia?
Anao uwezo wa kuhama biashara, kuuza hisa, kuwekeza kwenye fursa nyingine, kuondoka nchini akarudi baadae. Yaani huwezi mfanya lolote hesabu zake ziko mbele kabisa na kila kitu analindwa na sheria. Aliuza hisa za Vodacom Tanzania alikuwa largest shareholder akiwa na 35% ya shares mkajua atafirisika. Ikawaje?
Ni rahisi kumkamata Kikwete kwa ufisadi lakini sio Rostam. Sio kichwa cha kuku kile.