Kama ingelitokea msanii Mkristu akashutia video yake Msikitini

Kama ingelitokea msanii Mkristu akashutia video yake Msikitini

Wanawatoa pesa kwa viongozi wa makanisa.Sijaona movie za misikitini wala kuchezea uislamu kwenye movie,
Kanisa ni open minded society chief na ndio linaongoza hii Dunia , unayoyaona yote hayo hakuna jipya... wewe umemuona amezalilisha ila kanisa limeona ametangaza dini kupitia mziki wake na ndio maana huwezi kuona wanatoa tamko kumlaani ... vijana wa kislamu ndani ya kanisa takatifu hiyo ndio INJILI na unaambiwa script ili kaguliwa na ma-sister
 
Hivi mbona watz tunazidi kuwa wapumbavu kila kukicha hivi hapo Daimond ana kosa gani?

Kwani walienda wakalivamia kanisa na kuwashikia bunduki viongozi wa hilo kanisa na karekodi kwa razima?

Mpaka anakuja kufanya hicho alicho kifanya ina maana alipata baraka zote kutoka kwa viongozi wa kanisa husika na waliona hakuna tatizo yeye kufanya hivyo.
Sasa hapo Daimond ana kosa gani?
Wakulaumiwa ni wale walio waruhusu kifanya walicho kifanya.

Hizi hoja za sijui kwa nn hawajaenda msikitini ni hoja za kipumbavu kwa sababu msimamo wa viongozi wa kiislam uko wazi kabisa ya kuwa hayo mambo hayaruhusiwi ndani ya msikiti ,wakati upande wa viongozi wa pili ni rukusa na tumeshudia mara nyingi miziki na maigizo yakofanyika ndani ya makanisa tena waigizaji wakiwa wamevaa nusu uchi mbona hamkuwahi kusema huko nyuma?

Hata wanawake siku hizi wamekuwa wanaenda makanisa kwenye ibada na mavazi ya ajabu ajabu tukisema mnajitetea eti mungu ahaangilii mavazi bali ana angalia matendo.
Kwanza tuanze na wew.....je ......ni me au ke??
 
Msikiti wa kufanya hivyo ataupata wapi?
Makanisa yenyewe yanatakiwa yajiheshimu
 
Nasibu ni katika aliepotea kama mimi kafiri tu yaani mimi na huyo nasibu wala hatuna tofauti kwa sababu ya majibu yangu machafu niliyonayo, mwenyezi mungu aniepushe na tabia mbaya ya kuutukana ukristu, kwa kuwa nayo ni dini takatifu kama ulivyo uislamu wetu
Nashukuru kwa kuwa umelitambua hilo [emoji23]
Abdulhayy
 
FB_IMG_16521180681193008.jpg
 
Kutokana na kejeli za Diamond Platinumz juu ya kanisa Katoliki, imeonekana wazi kuwa kitendo alichokifanya sio cha haki wala heshima!

Hata isitoshe kauli yake kwenye post ya Zuchu aliyoandika kuwa hii nchi ina wenyewe mara acha tuendelee kuwawakilishia taifa lao inaonesha wazi mmomonyoko mzima wa maadili!

Unahisi tungelikuwa tunaongelea habari gani kwa sasa kama angelitokea msanii Mkristu akashuti video ya wimbo wake akiwa Msikitini?

Na je, viongozi wa Msikiti husika wangekubaliana na jambo kama hili lifanyike?
Nimekuwa muumini wa kanisa kwa muda mrefu sana, na pia niweke wazi mimi sio mpenzi wa mziki na wasanii.
Niseme yafuatayo:
1. Tukubali kwamba kitendo kilicho fanywa na BASATA ni cha kipumbavu na ikiwa wamefanya kwa shinikizo la madai basi madai hayo yalibeba mlengo wa chuki binafsi.
2. Kazi ya sanaaa itabaki kuwa kazi ya sanaa, neno sanaa linajieleza.
3. Kuuungwa mkono kwa swala hili ni kuchochea ubaguzi wa kidini.
4. Kisha ni hitimishe, Walipo kwenda kufanya shooting kanisani hawakuingia hivihivi, waliomba ridhaa kwa wahusika(inadaiwa Masister) walieleza wanacho kwenda kufanya, Walio waruhusu walishuhudia kilicho fanyika, Video imetoka na sasa ni wiki kadhaa, Je ikiwa walio waruhusu walikuwa ni waumini wa dini hiyo tena watawa BASATA waliwezaje kupokea madai hayo pasipo kuwahoji walioruhusu waliruhusu kwa misingi gani na badala yake kuwahujumu vijana hawa wawili?.

Ninapo tamatisha ninaomba nirejee tena kitendo walichofanya BASATA hakina mbolea, madhara yake ni mpasuko wa kidini na ndio maana punguwani wanahoji eti "Si angeenda msikitini?" Kauli hizi ni za kibaguzi.
 
Kutokana na kejeli za Diamond Platinumz juu ya kanisa Katoliki, imeonekana wazi kuwa kitendo alichokifanya sio cha haki wala heshima!

Hata isitoshe kauli yake kwenye post ya Zuchu aliyoandika kuwa hii nchi ina wenyewe mara acha tuendelee kuwawakilishia taifa lao inaonesha wazi mmomonyoko mzima wa maadili!

Unahisi tungelikuwa tunaongelea habari gani kwa sasa kama angelitokea msanii Mkristu akashuti video ya wimbo wake akiwa Msikitini?

Na je, viongozi wa Msikiti husika wangekubaliana na jambo kama hili lifanyike?
Sio mkristu hata kama angekuwa muislam tungemnyoosha
 
 
Kwani wewe ni dini gani?

Hayo maneno ndio aliyoyasema huyo jamaa uleyekuwa ukijadiliana naye hapo juu, sijayasema mimi.

Mimi nilikuwa namuambia kwa maneno yake hayo anakuwa amemtoa muislamu katika uislamu(kumkufurisha) hivyo awe makini, wala sijataja ukristu.
Samahani mkuu! [emoji26][emoji26]
 
Mkristo akikosea, wakristo wote wanataka alaumiwe huyo mkoseaji na hayo makosa aliyo yafanya yasihusishwe kabisa na dini ya kikristo.
Ajabu wakristo haohao endapo muislamu akikosea hua ndio wanakua wa kwanza kuubeza na kuudhihaki Uislamu na waislamu.

Yaani mpuuzi mmoja amekosea tena amekosea akiwa chini ya uangalizi wa viongozi wa kanisa lakini tuhuma zinabebeshwa kwa waislamu wote pamoja na dini yao.
 
Daaah! Nimecheka sana eti alivizia hawapo
Inawezekana! labda walikuta kanisani li wazi kwa ajili ya watu kuingia kusali, wakaingia zao, wakafanya yao! hukuona jinsi ambavyo walikuwa wanaimba kwa pupa! hata mpiga kinanda alikuwa amekaa tako moja! Yule panua domo alikuwa akijeuza shingo yake kutazama huku na huko wasije kukutwa!

Kwani waliokuwa wanakwaya ni akina nani kama sio wakina Juma lokole, Zuchu, mama Dangote, Esma na wenzao!!
 
Back
Top Bottom