Kama IGA inayozungumzwa ni hii basi Mwabukusi na wenzake watashindwa kesi na tutaona wameonewa

RNA

JF-Expert Member
Mar 27, 2013
1,584
2,683

Habari jf ,
Kwanza kabisa ifahamike IGA hii ni MKATABA sio makubaliano ya kawaida kama yanavyosemwa ,sababu ni makubaliano ya kimaandishi na yana ulinzi wa kisheria .

Pili huu Mkataba Una Ukomo lakini huo ukomo unategemea HGA -ukisoma vizuri utagundua umefichwa kwenye HGA ,ambayo ndio mikataba tutakayo ingia na DP WORLD .

Tatu IGA iko very technical hivyo HGA inabidi wahusishwe watu wenye uelewa sana sio wale vilaza kule vinginevyo tutauza mali za Nchi .

MAPUNGUFU nliyoyaona kwenye huu mkataba ambayo kina Mwabukusi na wenzake hawayapigii kelele .

1.Hakuna sehemu ambayo imetuweka wazi kwamba baada ya Kusaini IGA tunaweza kataa HGA kama zitakuwa hazieleweki .

2.Mkataba wa IGA inabidi uweke wazi kwamba tukishindwana na HGA au DP world basi na IGA ife hapo wamekataa kabisa .

3.Mkabata ukiusoma vizuri utagundua kuna maeneo unaonyesha kwamba ukisha saini hii IGA basi umebariki Dp World kuweza kufanya kazi regardless ya HGA .

KWA MAANZA RAHISI KUNA IGA NA HGA kwenye huu mkataba----Hapa wanasheria watanielewa ,nadhani kina Mwabukusi na wenzake waupitie upya kuna mapungufu mengi sana lakini yako more TECHNICAL ,mengi yanayopigiwa kelele yana majibu kwenye huo Mkataba .​
Screenshot_20230713-095031.png

Screenshot_20230713-094445.png

 

Attachments

  • AZIMIO LA BANDARI.pdf
    2.3 MB · Views: 6
Hicho kipengele chako namba tatu kimemaliza huu mjadala wako, ule mkataba ukiusoma vizuri utaona wazi mwarabu anaruhusiwa kuanza shughuli zake tangu October 2022, sasa kwa mantiki hiyo, kwanini kina Mwabukusi washindwe kesi zao?

Hicho kipengele chako kwa maana nyingine umekiri kwamba, mambo yote yaliyowekwa kwenye IGA yapo tayari kutekelezwa kimkataba, na hii ndio sababu iliyowafanya kina Mwabukusi wakafungue kesi, mambo ya hovyo kama mwarabu kujitawala ndani ya ardhi yetu, mkataba usiokuwa na ukomo na mengine, haya yalishasainiwa na yapo tayari kiutekelezaji tangu October 2022, mkataba wa IGA uliposainiwa..

Hapa usiweke HGA, hiyo haina maana tena, kama mkataba wa IGA ulishapitishwa na bunge, na upo tayari kutekelezwa, hiyo HGA itakuwa na maana gani? HGA inatumika tu kama kichaka cha kutuzubaisha pale wanapoulizwa maswali wanayokosa majibu yake, lakini kimsingi HGA haina maana tena.
 

Habari jf ,
Kwanza kabisa ifahamike IGA hii ni MKATABA sio makubaliano ya kawaida kama yanavyosemwa ,sababu ni makubaliano ya kimaandishi na yana ulinzi wa kisheria .

Pili huu Mkataba Una Ukomo lakini huo ukomo unategemea HGA -ukisoma vizuri utagundua umefichwa kwenye HGA ,ambayo ndio mikataba tutakayo ingia na DP WORLD .

Tatu IGA iko very technical hivyo HGA inabidi wahusishwe watu wenye uelewa sana sio wale vilaza kule vinginevyo tutauza mali za Nchi .

MAPUNGUFU nliyoyaona kwenye huu mkataba ambayo kina Mwabukusi na wenzake hawayapigii kelele .

1.Hakuna sehemu ambayo imetuweka wazi kwamba baada ya Kusaini IGA tunaweza kataa HGA kama zitakuwa hazieleweki .

2.Mkataba wa IGA inabidi uweke wazi kwamba tukishindwana na HGA au DP world basi na IGA ife hapo wamekataa kabisa .

3.Mkabata ukiusoma vizuri utagundua kuna maeneo unaonyesha kwamba ukisha saini hii IGA basi umebariki Dp World kuweza kufanya kazi regardless ya HGA .

KWA MAANZA RAHISI KUNA IGA NA HGA kwenye huu mkataba----Hapa wanasheria watanielewa ,nadhani kina Mwabukusi na wenzake waupitie upya kuna mapungufu mengi sana lakini yako more TECHNICAL ,mengi yanayopigiwa kelele yana majibu kwenye huo Mkataba .​
View attachment 2686495
View attachment 2686493
Wanashindwa Kesi ,niko hapa.
Mkataba hakuna ambacho umeacha jamani, IGA inawez expiry ndani ya Miezi 12 . Na HGA hatulazimishwe kuzisaini .

Nipe Kifungu kutokq IGA kinachotulazimisha
 
Sawa sisi tupo teyari kwa maamuzi yoyote yatakayotolewa na mahakama Ili tu baadae likija tokea la kutokea tunyooshee vidole mihimili yote ya nchi maana itakua yote imeshiriki kikamilifu kuingiza Chaka nchi yetu tunataka kusiwe na kisingizio kwamba mlichukua hatua gani angali mlikua mnajua kunashida pahala
 
Back
Top Bottom