Mirlz B Matthew
JF-Expert Member
- Oct 10, 2011
- 2,207
- 3,059
Solar ni Pasua kichwa. .......Vifaa vikidumu zaidi ya mwaka unashukuru....
Vipi una uzoefu wa zile taa za solar za nguzo ambazo huwekwa barabarani au kwenye fence za nyumba.?Ushauri wangu kulingana na uzoefu katika matumizi ya hizi system za umeme wa solar au tanesco.
1. Kama eneo ulilopo kuna upatikanaji wa umeme wa tanesco basi acha kufikiria solar hata kama matumizi yako ni madogo we unga tu umeme wa tanesco.
2. Kama eneo ulipo hakuna umeme wa tanesco basi nenda kwenye solar tu.
Ila kulinganisha umeme wa tanesco na solar kwa upande wa gharama, ubora na nguvu basi tanesco uko vizuri.
Tumia umeme wa solar kama alternative na sio substitute way.
With proper calculations and investment, solar ni umeme reliable sana. Lakini hapa kwenye mahesabu umechanganya mambo.Hello!
Umeme wa jua ni bora na ninatamani Watanzania wote wangekuwa nao.
Ukinunua system ya umeme wa jua kwa sh.laki nane unaweza kutumia kwa matumizi ya friji dogo la nyumbani, ukawasha TV, redio, ukanyoosha nguo and so.
Hakuna kulipa kila mwezi kama zamani au kukosa umeme kwakuwa luku imeisha.
Ukiweka system ya milioni 2 unaweza kuwasha ma friji mengi, ukavuta maji chini nyumba yako isikatike maji na hawa dawasa sijui dawasco na TANESCO ukaishia kuwasikia redioni tu.
Solar energy is simple and reliable source of power.
Mimi sio fundi wala siuzi vifaa vya solar. Sitangazi biashara bali nawahamasisha tu tutumie umeme wa jua, hauishi na ni salama
Bila shaka inategemea na aina ya brand na materials zilizotumika.So long unasema wewe sio fundi, naelewa kuwa you have no clue kwenye solar systems.
Yani system ya milioni 2 iwashe friji nyingi na water pump? Ingekua hivyo tusingehangaika na Tanesco
Umeme wa jua ni bure kimatumizi lakini unafaa kwa matumizi madogo tu ya kuwasha taa na TV, kwa matumizi makubwa kama hayo uliyotaja investment cost ni kubwa sana up to 10 million na bado maintenance costs ipo kwa sababu ukiwa na matumizi makubwa battery life span inashuka kiasi cha kuhitaji replacement hata kila mwaka
Mimi ni fundi na pia nina kiwanda kidogo nyumbani chenye matumizi ya 1.5Kwatts tu lakini batteries 10 za 100Watts zikiwa full charged (mpya) haziwezi run hiyo load kwa zaidi ya 8 hours
Fikiria ukitaka kuendesha such load for 24hrs utahitaji betri ngapi na panels ngapi?
Wewe unaongelea water pump na friji nyingi
Zinakufaje mkuuZinakufa sekunde tu hzo unaanza kutafuta lak8 ya kufnga mpya bora uvte umeme ujipimie matmiz yako ulipe tratbu
Ni batteries ndio zinazochoka na sio panels.Solar Kuna kipind huwa inachoka na kuwa kero mwanga unaanza kuwa hafifu hata frij itashndwa kfnya kaz ipasavyo na badae hata taa zinazimika kabla hakujakucha umeme sahiv kuvuta ni 27k tu kama huduma ipo karbu na ww unaweza kuvuta tu hzo solar zinasaidia huko vjijin sehem ambayo haina umeme
Mkuu sidhani kama umeshawahi kutumia solar system iliyopangiliwa vizuri. Solar ni reliable sana. Shida ni kuwa nyingi za humu mitaani watu wanaokota tu vifaa ambavyo havina ubora. Inapoanza kusumbua mtu anakata tamaa na umeme wa solar.Ushauri wangu kulingana na uzoefu katika matumizi ya hizi system za umeme wa solar au tanesco.
1. Kama eneo ulilopo kuna upatikanaji wa umeme wa tanesco basi acha kufikiria solar hata kama matumizi yako ni madogo we unga tu umeme wa tanesco.
2. Kama eneo ulipo hakuna umeme wa tanesco basi nenda kwenye solar tu.
Ila kulinganisha umeme wa tanesco na solar kwa upande wa gharama, ubora na nguvu basi tanesco uko vizuri.
Tumia umeme wa solar kama alternative na sio substitute way.
Exactly, na muulize mtu ni aina gani ya battery anatumia. Hapo ndo utajua watu wananunua vitu vya solar vya bei nafuu na wanategemea ufanisi mkubwa.Ni batteries ndio zinazochoka na sio panels.
Hii sio kweli kama ni kweli basi itakuwa fake au cheap product.Zinakufa sekunde tu hzo unaanza kutafuta lak8 ya kufnga mpya bora uvte umeme ujipimie matmiz yako ulipe tratbu
Ishu sio vifaa kwa ujumla. Ishu tatizo la dunia nzima ni BETRIMkuu sidhani kama umeshawahi kutumia solar system iliyopangiliwa vizuri. Solar ni reliable sana. Shida ni kuwa nyingi za humu mitaani watu wanaokota tu vifaa ambavyo havina ubora. Inapoanza kusumbua mtu anakata tamaa na umeme wa solar.
Mkuu!Ishu sio vifaa kwa ujumla. Ishu tatizo la dunia nzima ni BETRI
nimeandika kwa herufi kubwa muelewe. Umeme hata uzalishe kiasi gani kwa hizo panels ukija kwenye BETRI ya kuhifadhi ili utumie ndo kuna shida. Ukiwa na matumizi makubwa BETRI zinachoka na ni gharama kubadilisha kila mud
Magari ya Umeme duniani wanahangaika na BETRI
Umeme wa solar unashindwa kuwa mainstream kwasababu ya BETRI
Simu zenyewe bado tunahangaika na BETRI
Ni swala la kiteknolojia bado sayansi haijafikia huko ila tunable kea
So usije ukajidanganya eti Umeme wa solar utatumia vitu kama wa tanesco bado sana. Solar ni alternative tu kwa sasa
Hizo betri nzuri kwa kutoa mizunguko 5000 (miaka 13) kwa matumizi yapi?Mkuu!
Fundi yoyote wa umeme wa solar atakubali kuwa battery ni sehemu dhaifu katika mfumo wa solar. Lakini sio dhaifu kama unavyozani wewe. Teknolojia katika utengenezaji wa battery imefika mbali sana.
Sasa hivi zipo battery zenye ufanisi mkubwa. Kiasi kwamba mpaka utakapohitaji kubadilisha hizo battery zitakuwa zimeshajilipa tayari. Hivyo hupati hasara.
Nikupe tu mfano!
1. Tesla powerwall battery inaweza kukupa mizunguko (charge-discharge cycles) 5000 na ikabaki na ufanisi wa 90%.
Kumbuka kila mzunguko mmoja ni sawa na siku moja. Kwenye mizunguko 5000 unapata miaka 13 na zaidi. Tesla wenyewe wanatoa warranty ya miaka 10. Can you imagine? Warranty ni miaka 10.
Hapo bado kuna battery za victron, delta, LG na nyingine nyingi.
Narudia tena mkuu, kama unanunua battery cheap za hapo kariakoo, utalalama kila siku.
Hapa bongo zipo battery nzuri kiasi kama ritar, na leoch. Watu hawanunui kwa sababu zina bei. Lakini ufanisi wake ni mzuri kiasi. Uliza watu wanaozitumia.
Kiwanda sehemu ya kufanyia production au manufacturing, kiwanda hakipimwi kwa matumizi makubwa ya umeme ila aina ya matumizi. Mimi natumia 1.5kw kwa masaa 24 kwa siku 365 na kwa namna yoyote sihitaji power shortage kwa hata nusu saaMtaalamu, 1.5kW ni kiwanda cha kufanya nini tena? Tuna pasi zenye mpaka 2.4kW, heater kwa matumizi madogo ya nyumbani ya mpaka 0.89kW.
Nikiwasha vyote vinavyotakiwa kwa usiku, bila pasi na radio hapa home, inasoma 1.39kW
1.5kW au 15.0kW?
Kwa kutumia original quality hiyo 2M aliyosema inanunua betri 2 tu 100watts na panel moja ya 200wattsBila shaka inategemea na aina ya brand na materials zilizotumika.
Au elon musk asingewekeza Billions kwenye mradi wake wa solar city.
ndio ndio upo sawa mkuuPasi ya 12v ipo lakini haina maana kuwa ndio inapunguza matumizi, heating element inahitaji wattage kubwa na high current, hata ukitumia pasi ya 12v huwezi kuitumia kwa zaidi ya dakika 30 kwenye betri ya 100watts
Hizo betri nzuri kwa kutoa mizunguko 5000 (miaka 13) kwa matumizi yapi?
Sidhani na sina uhakika labda ndo unifahamishe wewe kwamba unaweza kutumia AC kwenye nyumba friji 2 na mashine ya kuvuta maji toka ardhini
Price per unit si zinatofautiana kulingana na matumizi na service line uliyoomba kwa Tanesco? Sasa kwa matumizi hayo, huoni kuwa hakuna haja ya kusema ni kiwanda? Mpaka matumizi ya 10kW kwa Tanesco ni matumizi ya kawaida nyumbani.Kiwanda sehemu ya kufanyia production au manufacturing, kiwanda hakipimwi kwa matumizi makubwa ya umeme ila aina ya matumizi. Mimi natumia 1.5kw kwa masaa 24 kwa siku 365 na kwa namna yoyote sihitaji power shortage kwa hata nusu saa
Wewe unaweza kutumia hiyo 2kw lakini ikitokea shortage ya hata kutwa nzima isikuathili kwa sababu ni matumizi ya nyumbani na pia labda load yenyewe unatumia kwa masaa 8 tu kwa siku
Mkuu Culminate, in theory solar inaweza endesha kila kitu, problem hapa ni cost. project uliyo-sight hapo ina faidika na economy of scale. watu wengi wamesema humu Tanesco ni cheap, ni cheap kwa sabau ya economy of scale. ingekuwa kila mtu anazalisha kwenye kijumba chake ingekuwa ghali pia. Hivyo kwa mfano Tanesco wakiamua (najua wanampango huo tayari) kuzalisha umeme wa solar kwa kiwango kama hicho pia utakuwa rahisi. Battery kwa sasa ndiyo kikwazo kwa solar. mimi nimefanya feasibility study ili nitumie solar nyumbani kwangu nikalinganisha actual cost ya solar (upfront cost + maintenance) kulinganisha na Tanesco (upfront cost + monthly tariffs) nimeamua solar uwe backup onlyMkuu umeme kuwa AC haimaanishi kuwa ndio una nguvu zaidi. Kubadilisha umeme wa solar ambao ni DC kuufanya AC ni rahisi tu. Ndio kazi ya Inverter hiyo.
With enough panels and batteries, hakuna ambacho huwezi kuendesha kwa kutumia solar
Tesla ameshafunga power back up yenye uwezo wa 100MW kwa kutumia battery. Huo umeme unatumika kuwasha South Australia na vitu vyote watu wanavyotumia.
Fatilia zaidi utaona teknolojia ya battery iko mbali sana.
View attachment 1867857
Set ya betri ikifa hela itakutoka tena,japo zinakaa muda mrefu.Tupe na hasara zake tuone kama tunaweza kuzikabili