Sitachoka
JF-Expert Member
- Nov 17, 2011
- 3,030
- 1,303
BABA wa Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Madaktari, mzee Steven
Mwaitenda amejikuta akiangua
kilio kwa uchungu mbele ya
wanaharakati ambao
walimtembelea mwanae, Dk.
Steven Ulimboka kumpa pole
kufuatia tukio la kutekwa na
kujeruhiwa vibaya na watu
wasiojulikana.
Hali hiyo ilitokea jana jioni katika
Taasisi ya Tiba ya Mifupa
Muhimbili (MOI), ambapo
wanaharakati kutoka taasisi na
asasi mbalimbali za utetezi wa
haki za binadamu walifika kwa
lengo la kumpa pole Dk. Ulimboka
kufuatia kitendo kilichomfika.
Mzee Mwaitenda alijikuta
akibubujikwa na machozi na
kushindwa kuendelea
kuzungumza alipokuwa akitoa
shukrani kwa wanaharakati hao,
kwa niaba ya mwanaye ambaye
wanaharakati hao walishindwa
kumuona wote kutokana na hali
yake ilivyo sasa.
Niseme wazi nimefarijika sana
kwa ujio wenu kumwona
mwanangu dhidi ya mambo ya
kikatili aliyofanyiwa akitetea haki
za wengine , alisema mzee
Mwaitenda kabla ya kushindwa
kuendelea na kuangua kilio mbele
ya wanaharakati.
Baada ya tukio hilo baadhi ya
wanaharakati walimshika
wakishirikiana na wanafamilia ya
mzee Mwaitenda na kumbebeleza
kisha kumtoa mbele ya
mkusanyiko huo wa
wanaharakati na kumrudisha
wodini huku wakimfariji.
Wakizungumza mara baada ya
tukio hilo wanaharakati
wameelezea kusikitishwa na
vitendo vinavyoendelea MOI eneo
ambalo amelazwa kiongozi huyo
wa madaktari ambavyo
vimeendelea kutishia usalama wa
Dk. Ulimboka.
Akifafanua zaidi mwakilishi wa
wanaharakati hao, Markos Albania
alisema taarifa walizozipata usiku
wa juzi kuna wagonjwa feki
ambao walijitokeza MOI huku
wakitaka kulazwa wodi ya
Wagonjwa Mahututi (ICU)
alipolazwa Dk. Ulimboka lakini
baadaye waligoma kuingizwa
wodini.
Wapo wagonjwa ambao
waliletwa na kutaka kupelekwa
ICU moja kwa moja kuna watu
wanakuja usiku wa manane
wakitaka kumtembelea Dk.
Ulimboka matendo
yanayoendelea kutokea
ukilinganisha na kauli za Serikali
zilizotolewa bungeni yanatishia
usalama na uhai wa mgonjwa,
alisema Albania.
Aidha amesema kitendo cha
vyombo vya usalama kuendelea
kumuhoji Dk. Ulimboka akiwa hoi
hospitalini si vya kiungwana
kwani tayari muhusika amewataja
hadi kwa majina watu ambao
anawashuku lakini hadi sasa
hakuna aliyechukuliwa hatua
yoyote.
Pamoja na hayo wanaharakati
hao wameitaka Serikali kuunda
tume huru mchanganyiko na raia
ambayo itachunguza kiundani
suala hilo, kwani hawana imani
na Jeshi la Polisi ambalo limedai
kuunda timu ambayo
inachunguza kwa kina suala hilo.
Dk. Ulimboka ambaye ni kiongozi
wa madaktari ambao
wanaendelea na mgomo wan chi
nzima kuishinikiza Serikali
kutekeleza madai yao alitekwa
juzi na watu wasiojulikana na
kupigwa na kuteswa kikatili kabla
ya kutelekezwa katika msitu wa
Mabwepande.
*Habari hii imeandaliwa na
kuletwa hapa na Mtandao wa
Thehabari.com
ya Madaktari, mzee Steven
Mwaitenda amejikuta akiangua
kilio kwa uchungu mbele ya
wanaharakati ambao
walimtembelea mwanae, Dk.
Steven Ulimboka kumpa pole
kufuatia tukio la kutekwa na
kujeruhiwa vibaya na watu
wasiojulikana.
Hali hiyo ilitokea jana jioni katika
Taasisi ya Tiba ya Mifupa
Muhimbili (MOI), ambapo
wanaharakati kutoka taasisi na
asasi mbalimbali za utetezi wa
haki za binadamu walifika kwa
lengo la kumpa pole Dk. Ulimboka
kufuatia kitendo kilichomfika.
Mzee Mwaitenda alijikuta
akibubujikwa na machozi na
kushindwa kuendelea
kuzungumza alipokuwa akitoa
shukrani kwa wanaharakati hao,
kwa niaba ya mwanaye ambaye
wanaharakati hao walishindwa
kumuona wote kutokana na hali
yake ilivyo sasa.
Niseme wazi nimefarijika sana
kwa ujio wenu kumwona
mwanangu dhidi ya mambo ya
kikatili aliyofanyiwa akitetea haki
za wengine , alisema mzee
Mwaitenda kabla ya kushindwa
kuendelea na kuangua kilio mbele
ya wanaharakati.
Baada ya tukio hilo baadhi ya
wanaharakati walimshika
wakishirikiana na wanafamilia ya
mzee Mwaitenda na kumbebeleza
kisha kumtoa mbele ya
mkusanyiko huo wa
wanaharakati na kumrudisha
wodini huku wakimfariji.
Wakizungumza mara baada ya
tukio hilo wanaharakati
wameelezea kusikitishwa na
vitendo vinavyoendelea MOI eneo
ambalo amelazwa kiongozi huyo
wa madaktari ambavyo
vimeendelea kutishia usalama wa
Dk. Ulimboka.
Akifafanua zaidi mwakilishi wa
wanaharakati hao, Markos Albania
alisema taarifa walizozipata usiku
wa juzi kuna wagonjwa feki
ambao walijitokeza MOI huku
wakitaka kulazwa wodi ya
Wagonjwa Mahututi (ICU)
alipolazwa Dk. Ulimboka lakini
baadaye waligoma kuingizwa
wodini.
Wapo wagonjwa ambao
waliletwa na kutaka kupelekwa
ICU moja kwa moja kuna watu
wanakuja usiku wa manane
wakitaka kumtembelea Dk.
Ulimboka matendo
yanayoendelea kutokea
ukilinganisha na kauli za Serikali
zilizotolewa bungeni yanatishia
usalama na uhai wa mgonjwa,
alisema Albania.
Aidha amesema kitendo cha
vyombo vya usalama kuendelea
kumuhoji Dk. Ulimboka akiwa hoi
hospitalini si vya kiungwana
kwani tayari muhusika amewataja
hadi kwa majina watu ambao
anawashuku lakini hadi sasa
hakuna aliyechukuliwa hatua
yoyote.
Pamoja na hayo wanaharakati
hao wameitaka Serikali kuunda
tume huru mchanganyiko na raia
ambayo itachunguza kiundani
suala hilo, kwani hawana imani
na Jeshi la Polisi ambalo limedai
kuunda timu ambayo
inachunguza kwa kina suala hilo.
Dk. Ulimboka ambaye ni kiongozi
wa madaktari ambao
wanaendelea na mgomo wan chi
nzima kuishinikiza Serikali
kutekeleza madai yao alitekwa
juzi na watu wasiojulikana na
kupigwa na kuteswa kikatili kabla
ya kutelekezwa katika msitu wa
Mabwepande.
*Habari hii imeandaliwa na
kuletwa hapa na Mtandao wa
Thehabari.com