Kama hivi ndivyo ilivyo muda wowote dr. Ulimboka atatutoka duniani, baba yake aangua kilio.

Sitachoka

JF-Expert Member
Nov 17, 2011
3,030
1,303
BABA wa Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Madaktari, mzee Steven
Mwaitenda amejikuta akiangua
kilio kwa uchungu mbele ya
wanaharakati ambao
walimtembelea mwanae, Dk.
Steven Ulimboka kumpa pole
kufuatia tukio la kutekwa na
kujeruhiwa vibaya na watu
wasiojulikana.
Hali hiyo ilitokea jana jioni katika
Taasisi ya Tiba ya Mifupa
Muhimbili (MOI), ambapo
wanaharakati kutoka taasisi na
asasi mbalimbali za utetezi wa
haki za binadamu walifika kwa
lengo la kumpa pole Dk. Ulimboka
kufuatia kitendo kilichomfika.
Mzee Mwaitenda alijikuta
akibubujikwa na machozi na
kushindwa kuendelea
kuzungumza alipokuwa akitoa
shukrani kwa wanaharakati hao,
kwa niaba ya mwanaye ambaye
wanaharakati hao walishindwa
kumuona wote kutokana na hali
yake ilivyo sasa.
“Niseme wazi nimefarijika sana
kwa ujio wenu kumwona
mwanangu dhidi ya mambo ya
kikatili aliyofanyiwa akitetea haki
za wengine…,” alisema mzee
Mwaitenda kabla ya kushindwa
kuendelea na kuangua kilio mbele
ya wanaharakati.
Baada ya tukio hilo baadhi ya
wanaharakati walimshika
wakishirikiana na wanafamilia ya
mzee Mwaitenda na kumbebeleza
kisha kumtoa mbele ya
mkusanyiko huo wa
wanaharakati na kumrudisha
wodini huku wakimfariji.
Wakizungumza mara baada ya
tukio hilo wanaharakati
wameelezea kusikitishwa na
vitendo vinavyoendelea MOI eneo
ambalo amelazwa kiongozi huyo
wa madaktari ambavyo
vimeendelea kutishia usalama wa
Dk. Ulimboka.
Akifafanua zaidi mwakilishi wa
wanaharakati hao, Markos Albania
alisema taarifa walizozipata usiku
wa juzi kuna wagonjwa ‘feki’
ambao walijitokeza MOI huku
wakitaka kulazwa wodi ya
Wagonjwa Mahututi (ICU)
alipolazwa Dk. Ulimboka lakini
baadaye waligoma kuingizwa
wodini.
“Wapo wagonjwa ambao
waliletwa na kutaka kupelekwa
ICU moja kwa moja…kuna watu
wanakuja usiku wa manane
wakitaka kumtembelea Dk.
Ulimboka…matendo
yanayoendelea kutokea
ukilinganisha na kauli za Serikali
zilizotolewa bungeni yanatishia
usalama na uhai wa mgonjwa,”
alisema Albania.
Aidha amesema kitendo cha
vyombo vya usalama kuendelea
kumuhoji Dk. Ulimboka akiwa hoi
hospitalini si vya kiungwana
kwani tayari muhusika amewataja
hadi kwa majina watu ambao
anawashuku lakini hadi sasa
hakuna aliyechukuliwa hatua
yoyote.
Pamoja na hayo wanaharakati
hao wameitaka Serikali kuunda
tume huru mchanganyiko na raia
ambayo itachunguza kiundani
suala hilo, kwani hawana imani
na Jeshi la Polisi ambalo limedai
kuunda timu ambayo
inachunguza kwa kina suala hilo.
Dk. Ulimboka ambaye ni kiongozi
wa madaktari ambao
wanaendelea na mgomo wan chi
nzima kuishinikiza Serikali
kutekeleza madai yao alitekwa
juzi na watu wasiojulikana na
kupigwa na kuteswa kikatili kabla
ya kutelekezwa katika msitu wa
Mabwepande.
*Habari hii imeandaliwa na
kuletwa hapa na Mtandao wa
Thehabari.com
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav
BABA wa Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Madaktari, mzee Steven
Mwaitenda amejikuta akiangua
kilio kwa uchungu mbele ya
wanaharakati ambao
walimtembelea mwanae, Dk.
Steven Ulimboka kumpa pole
kufuatia tukio la kutekwa na
kujeruhiwa vibaya na watu
wasiojulikana.
Hali hiyo ilitokea jana jioni katika
Taasisi ya Tiba ya Mifupa
Muhimbili (MOI), ambapo
wanaharakati kutoka taasisi na
asasi mbalimbali za utetezi wa
haki za binadamu walifika kwa
lengo la kumpa pole Dk. Ulimboka
kufuatia kitendo kilichomfika.
Mzee Mwaitenda alijikuta
akibubujikwa na machozi na
kushindwa kuendelea
kuzungumza alipokuwa akitoa
shukrani kwa wanaharakati hao,
kwa niaba ya mwanaye ambaye
wanaharakati hao walishindwa
kumuona wote kutokana na hali
yake ilivyo sasa.
“Niseme wazi nimefarijika sana
kwa ujio wenu kumwona
mwanangu dhidi ya mambo ya
kikatili aliyofanyiwa akitetea haki
za wengine…,” alisema mzee
Mwaitenda kabla ya kushindwa
kuendelea na kuangua kilio mbele
ya wanaharakati.
Baada ya tukio hilo baadhi ya
wanaharakati walimshika
wakishirikiana na wanafamilia ya
mzee Mwaitenda na kumbebeleza
kisha kumtoa mbele ya
mkusanyiko huo wa
wanaharakati na kumrudisha
wodini huku wakimfariji.
Wakizungumza mara baada ya
tukio hilo wanaharakati
wameelezea kusikitishwa na
vitendo vinavyoendelea MOI eneo
ambalo amelazwa kiongozi huyo
wa madaktari ambavyo
vimeendelea kutishia usalama wa
Dk. Ulimboka.
Akifafanua zaidi mwakilishi wa
wanaharakati hao, Markos Albania
alisema taarifa walizozipata usiku
wa juzi kuna wagonjwa ‘feki’
ambao walijitokeza MOI huku
wakitaka kulazwa wodi ya
Wagonjwa Mahututi (ICU)
alipolazwa Dk. Ulimboka lakini
baadaye waligoma kuingizwa
wodini.
“Wapo wagonjwa ambao
waliletwa na kutaka kupelekwa
ICU moja kwa moja…kuna watu
wanakuja usiku wa manane
wakitaka kumtembelea Dk.
Ulimboka…matendo
yanayoendelea kutokea
ukilinganisha na kauli za Serikali
zilizotolewa bungeni yanatishia
usalama na uhai wa mgonjwa,”
alisema Albania.
Aidha amesema kitendo cha
vyombo vya usalama kuendelea
kumuhoji Dk. Ulimboka akiwa hoi
hospitalini si vya kiungwana
kwani tayari muhusika amewataja
hadi kwa majina watu ambao
anawashuku lakini hadi sasa
hakuna aliyechukuliwa hatua
yoyote.
Pamoja na hayo wanaharakati
hao wameitaka Serikali kuunda
tume huru mchanganyiko na raia
ambayo itachunguza kiundani
suala hilo, kwani hawana imani
na Jeshi la Polisi ambalo limedai
kuunda timu ambayo
inachunguza kwa kina suala hilo.
Dk. Ulimboka ambaye ni kiongozi
wa madaktari ambao
wanaendelea na mgomo wan chi
nzima kuishinikiza Serikali
kutekeleza madai yao alitekwa
juzi na watu wasiojulikana na
kupigwa na kuteswa kikatili kabla
ya kutelekezwa katika msitu wa
Mabwepande.
*Habari hii imeandaliwa na
kuletwa hapa na Mtandao wa
Thehabari.com
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

Nakupa 100%
 
Mwenyezi Mungu alikuwa pamoja nawe Dr Ulimboka ucku ule wa tukio, ataendelea kuwa pamoja kupambana ktk kupona kwako, na yupo pamoja na wale wote wapambanaji dhidi ya hao wapinga Haki kwa Watanzania.

Tupo pamoja Dr Ulimboka, Wanaharakati wote, Madaktari wote, Family ya Dr Ulimboka na Watanzania wote ktk hizi harakati tufanikiwe ktk Tiba ya Dr, na pia kupambana ktk kuleta Ukombozi wa kweli kwa Taifa la Tanzania dhidi ya Udhalimu wa aina yeyote.
 
Kwani hospitali nzima kalazwa Dr.ulimboka peke yake? walizani watamuua kirahisi kaaga kwao huyo hadi awaumbue ndo mkome mmekazana watu wanakufa kwani huwaga hawafi vita ni vita aisee .....serikali imetangaza vita haujui katika kila vita lazima watu wafe...
 
Msifurahie ya wenzenu,kuna familia yamewakuta haya aliyofanyiwa Dr.Ulimboka wakati wa awamu ya kwanza kwa kisingizio cha uhujumu uchumi,bila hata kufunguliwa mashtaka ,kuteswa na kutupwa tu gerezani.Baada ya miaka yakutumikia kifungo wanaambiwa walikuwa hawana hatia. Hata siye tulio na wagonjwa majumbani bado hatujatoa laana hiyo.Kisasi ni cha mungu.
Sasa madaktari wamerudi kazini?Je unadhani ni haki kukodisha madaktari wa nje kwa tz.200mil za walipa kodi?Kama wanazo kwa nini wasirekebisha hali za hospitali na kuwalipa hawa watanzania wenzetu vizuri?Kweli ni bora kulipa vizuri mgeni na mwananchi wako kumwacha na njaa?Lazima ziwe ni akili za kichaa.........
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav
Acha upuuzi mbona unakuwa fara kama haufikirii. Mwenye kazi ya kuhudumia raia ni hii serikari yenu sikivu inayosikia hata ushauri wa kipuuzi.
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav
Walipelekwa mabwepande kung'olewa kucha na meno hao waliokufa?
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

Sisi tumefiwa na vichanga vyetu baada hospitali hapa nchini kukosa vacuum pump ya kuvuta maji machafu ambayo vichanga humeza wakati wa zoezi la mama kujifungua na kuziba njia za hewa. Pampu hiyo huuzwa Shs 5,000/= tu. Posho za kukaa ambazo maafisa waandamizi wa Serikali ya CCM hulipana ya Shs 200,000/= kwa kila kikao, hata kama ni kuhudhuria kikao mlango wa pili toka ofisi zao ingetosha kununua pampu 40 kama hizo na kukoa maisha ya vichanga hizi. Je ni akina mama wangapi wamepoteza vichanga vyao baada ya kubeba mimba miezi 9 kwa kukosekana kifaa hiki?

Sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa kukosekana sindano ya kuingiza maji ya dripu mwilini inayouzwa shs 250/= tu.

Jana katika tarifa ya habari ya ITV akina wawili waliopata ajali ya pikipiki na kukanyagwa na gari kubwa wametelekezwa katika vitanda vya hospitali ya Bombo Tanga wakingoja kupoteza maisha kwa sababu hospitai hiyo haina kifaa cha kupiga picha za X-ray, madakatari walikuwepo lakini hawakuweza kuwapatia huduma kwa wagonjwa wanalazimka kuwa na fedha za kuhamishiwa katika hospitali binafsi kupiga picha hizo. Gharama ya shangingi moja wanalopanda maafisa waandamizi wa CCM na Serikali yake zingetosha kuzipatia hospitali 3 vifaa vya aina hiyo. Je ni watanzania wangapi hupoteza maisha kila siku kwa kukosekana vifaa vya X-ray, Ultra sound, CT scan n.k katika hospitalia ilihali mashangingi yanannunuliwa kila mwaka na fedha Serikali ya CCM hutenge mabilioni kwa ajili ya kulipana posho za kukaa na safari zisizo na tija?

Katika madai yao madakatari wamesema wamechoka kuwaona watanzania wenzao wakipoteza maisha kimya kimya kwa kukosekana vifaa muhimu vya matibabu ilihali nchi ikisamehe Dola Bilioni kama kosi. Kuanzia sasa ni vyema idadi ya watanzania wanaopoteza maisha ikaanza kuwekwa wazi na sababu zake,
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav
unahaki ya kuilalamikia serikali na sio madaktali maana wewe mwananchi huna mkataba nao.wewe kama umefiwa lia na sserikali yako na wala sio madaktari maana mkata upo kati yako na serikali kwa kula yako ya ndiyo.lakini mkata wa serikali na daktari ni wa ajira.pole kwa kufiwa na sababu ya serlikali dhaifu.
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

hoja zako ni kama za watoto wadogo! Ndio maana humepandwa na hasira ukatukana kwaajili ya kukosa cha kuandika.

Sasa umefiwa na nduguzo kwa hiyo una halalisha wengine wauwawe?
Jaribu kufikiri kwa kina kama wewe unaweza kufanya kazi isiyo endana na malipo?

Unatakiwa utumie busara unapo ongea kitu, dr ulimboka alikuwa anatetea hata haki zako za kupata huduma bora.

Halaf hoja yeyote haimalizwi kwa kutukana ni aibu sana.

NB: Nothing goes for nothing
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

we punguwani nini?sasa ndugu zako wanatuhusu nini sisi?
 
hapo kwenye red ni kichaga au lugha gani dogo,unajifanya unahasira kama kweli jisaidie haja kubwa tuone.
Acha upuuzi mbona unakuwa fara kama haufikirii. Mwenye kazi ya kuhudumia raia ni hii serikari yenu sikivu inayosikia hata ushauri wa kipuuzi.
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? Hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? Na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.pumbav

dos santos umevurugwa kwa kuhemewa ,paka jike wewe
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav
Watu kama nyie you deserve to die and burn in hell.
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

Kufa kila mtu atakufa na Dr. Ulimboka si mtu wa kwanza kulazwa Icu sababu iliyofanywa alazwe icu haifanani na sababu iliyofanya hao ndugu zako kufa.Kwahiyo mkimuua ulimboka ndiyo itatuliza machungu yako na wenzio?
 
Ukweli ahata mimi nikiiumwa leo na nikakosa huduma sitawalaumu Madokta kwani sina Mkataba nao. Mimi najua serikali yangu ndio yenye jukumu la kunihudumia. Kila la kheri Tanzania.
 
Back
Top Bottom