Kama haulipwi mshahara wa 6 million kwa mwezi usinunue gari

Expensive life

JF-Expert Member
May 2, 2020
1,704
5,480
Mwanahabari nguli hapa nchini, Jenerali twaha ulimwengu amewaasa vijana kuacha mara moja kununua magari kama hawana kipato cha million 6 kwa mwezi.

Mwanahabari huyo ameainisha kuwa, Nimepata feedback kwa vijana wanasema wakiwa na kipato cha million mbili wanaweza kununua gari. Tatizo hapa ni kwamba, kama kipato chako hakikizi viwango fulani ni hatari kuendesha gari.

Unadhani kuwa unaweza ukalitunza na kulitengeneza na kulitilia mafuta kila siku, kukata insurance ya kutosha na kadhalika?

inawezekana vijana wanapata milion mbili au tatu, lakini wanaona kwamba wanaweza, na vijana wanasema kwamba wakiwa na Ist hiyo hela inatosha kabisa kuendesha gari.

Vijana mnaomiliki mandinga, embu tupeni uzoefu wenu na sisi tunaolipwa afu tatu kwa siku tumiliki mandinga.

AE731DF1-7C7E-4525-9623-D038D6F2A864.jpeg
 
Anazeeka vibaya huyu mzee kwani amesikia nataka kuendesha discovery 4 au Mercedes-Benz?

Mimi carina ti inanitosha kwa kipato changu cha laki 4
 
Kwa ushauri huu ni watanzania wasiozidi milion 1 kwa kipato halali ambao ndio wataweza kumiliki magari
 
Ndio maana mie nikitaka kufanya langu sisikii la muazini wala mnadi swala.

Sasa vibaby walker ndio mpaka nilipwe milioni 6 kwa mwezi, sasa hiyo 6 kwa mwezi si ninakuwa nanunua gari kila baada ya mwezi 🤣😂
 
Back
Top Bottom