Kama habari hii ya Acacia kukataa kutulipa hata hiyo dola milioni 300 ni ya kweli, sijui nini kitafuata

Mkuu ulitarajia hao wazungu watalipa chochote? nilipoona akina Kabudi wamekaa na hao wazungu miezi miwili mjadala ulikuwa ni deni $190b, wakatoka bila maelezo ya hilo deni la 190b imekuwaje, wakaiashia kusema sijui $300m goodwill ndio nikajua hakuna mzungu mjinga. Kibaya zaidi hata hawa viongozi wetu hawakuthubutu kuweka hiyo mikataba wazi bungeni. Hapo ndio nilijua hakuna lolote zaidi ya kulishana upepo wa uzalendo uchwara.

Nilichoka nilivyomsikia Prof. Kabudi akitoa ufafanuzi wa marekebisho ya mikataba ya madini, sasa kama prof anatoa ufafanuzi wa jambo na wala hajaeleweka hata na wasomi hapo huoni ni utata mtupu? Ni hivi hakuna chochote tunaowadai hao wazungu bali wabaya wetu ni viongozi wetu walioingia hiyi mikataba ambao wanaitwa makaburi yasiyofukuliwa na kinachowalinda ni kinga yao ya chama twawala. Kumbuka Magu alisema Chenge, Yona, Karamagi and the likes wakamatwe, lakini hawajaguswa mpaka leo. Hapo utasema kuna unayemdai wakati hata hawa tunaowamudu hatujawachukulia hatua?

Acacia tuliambiwa hawajasaliwa hapa nchini wala hawatambuliki, lakini mpaka leo wapo na wanaendelea na shughuli zao. Sana saba tunaona watz wakipoteza ajira zao. Mkuu ukiona hata bei ya sukari, mafuta ya kula yametushinda na sasa mafuta ya taa hamna kwenye petrol station, ndio tutawaweza hao wazungu. Sisi tungojee uchaguzi wa 2020 watu washinde kwa kishindo chini ya uchaguzi wa kikatili na sio kumdai mzungu au kumzuia kuchimba madini.
Agiza unachotaka, nasemaa agiza unachotaka mkuu ntalipa ..
 


Kama hii habari ni ya kweli,basi kusema kitakachokubalika katika mazungumzo kati ya Barrick na serikali ni lazima kwanza Acacia wayaridhie ndio yakubalike,hakika huu ndio ulikuwa mtego na janja ya hawa wazungu.

Anyway,wacha tusubiri taarifa rasimi kujua ukweli ni upi.

Hapa ndo utaona widening gap kati ya village reasoning capacity vs universal based knowledge
 
Uzuri mali zote za ACACIA Bulyanhulu zipo ndani ya mgodi na kule Buzwagi walijaribu kutaka kupiga mnada baadhi ya mashine lakini Serikali ikawapiga stop,kila kitu kibakie humo mgodini,hawana pa kukwepea hao Wakoloni.

Wakati mwingine makampuni makubwa ya migodi huwa wanakodi / hire / rent mitambo na vifaa vya gharama kubwa badala ya kuvinunua. Nia ni kutumia fedha ndogo katika operesheni zake Kadri inavyowezekana.

Hii yote ni katika mikakati ya kukwepa capital gains tax mwisho wa uhai wa mgodi wakati wa kupiga mnada mitambo au kuihamishia katika migodi mingine ndani au nje ya Tanzania.

Hivyo hatuna uhakika kama mitambo yote iliyopo mgodini Bulyanhulu / Buzwagi ni ya ACACIA au ilikodiwa toka kampuni nyingine isiyo milikiwa na ACACIA.

Maana yake, serikali inaweza ikawa imezuia mitambo na vifaa visivyo vya ACACIA na kuingizwa ktk mgogoro mwingine na kampuni ya kimataifa yenye kumiliki vifaa hivyo.
Read more Source: When to buy or rent heavy equipment – five factors to consider. | Ritchie Bros. Auctioneers
 
Wakati mwingine makampuni makubwa ya migodi huwa wanakodi / hire / rent mitambo na vifaa vya gharama kubwa badala ya kuvinunua. Nia ni kutumia fedha ndogo katika operesheni zake Kadri inavyowezekana.

Hii yote ni katika mikakati ya kukwepa capital gains tax mwisho wa uhai wa mgodi wakati wa kupiga mnada mitambo au kuihamishia katika migodi mingine ndani au nje ya Tanzania.

Hivyo hatuna uhakika kama mitambo yote iliyopo mgodini Bulyanhulu / Buzwagi ni ya ACACIA au ilikodiwa toka kampuni nyingine isiyo milikiwa na ACACIA.

Maana yake, serikali inaweza ikawa imezuia mitambo na vifaa visivyo vya ACACIA na kuingizwa ktk mgogoro mwingine na kampuni ya kimataifa yenye kumiliki vifaa hivyo.
Read more Source: When to buy or rent heavy equipment – five factors to consider. | Ritchie Bros. Auctioneers
Mitambo isingekuwa ya ACACIA wasinge-attempt kuipiga mnada,unaweza kupiga mnada mali isiyokuwa ya kwako?
 
Hatutapata hata dollar million moja...mark my words... Sana sana watatuachia mitambo chakavu tuitaifishe ama tuipige mnada kufidia deni... Lakini mabepari wale hawatoi hata dola moja... Sio policy yao hiyo
Sasa mbona walimzuga mdingi wetu akashangilia kumbe hola.
 
Mitambo isingekuwa ya ACACIA wasinge-attempt kuipiga mnada,unaweza kupiga mnada mali isiyokuwa ya kwako?

Mambo haya ktk mikataba ya makampuni ya kimataifa ni complex / yana changamoto sana.

Inaweza kuwa ACACIA walikubaliana dhamana kusimamia usalama wa mitambo ktk migodi yao mpaka kuwezesha wakala wa uuzaji kufanikisha zoezi lakini si wamiliki.

Tufanye subira ukweli wa jinsi makampuni ya kimataifa kama haya yanavyofanya operesheni zao utatupatia uzoefu.
 
Mambo haya ktk mikataba ya makampuni ya kimataifa ni complex / yana changamoto sana.

Inaweza kuwa ACACIA walikubaliana dhamana kusimamia usalama wa mitambo ktk migodi yao mpaka kuwezesha wakala wa uuzaji kufanikisha zoezi lakini si wamiliki.

Tufanye subira ukweli wa jinsi makampuni ya kimataifa kama haya yanavyofanya operesheni zao utatupatia uzoefu.
Poa poa mkuu,tuvute subira maana rasilimali yetu ya madini ni kubwa sana. Pale Bulyanhulu wanafanya uzalishaji ( reclaim of Final Tails ) si kwamba wanapata faida bali ni katika kulinda leseni wasije pokonywa.
 
Ngekua ni nchi nyingine,ni maandamano tu kwa kwenda mbele kushinikiza mabepari hawa walipe pesa.hapa kwetu tunamsikiliza magu tu....our god on earth.
 
Ngekua ni nchi nyingine,ni maandamano tu kwa kwenda mbele kushinikiza mabepari hawa walipe pesa.hapa kwetu tunamsikiliza magu tu....our god on earth.

Kabisa Mkuu, ndiyo maana huyu Mzee Thomas Ngawaiya anasema nchi hii hakuna Bunge wala Wizara zinazofanya kazi. Kwa vile kila kitu kina amuliwa na mtu mmoja sasa.

Source: Global TV online
 
Barrick sio muunganiko wa kampuni tano kama unavyosema Bali Barrick ni majority shareholder wa Acacia. Yaani Acacia hana share yoyote Barrick lakini Barrick ana share nyingi Acacia. Sijui kama umenielewa.
Suala la malipo, serikali ilikataa kuongea na acacia kwa sababu ndio mtuhumiwa lakini shareholder mkubwaBarrick ambaye ndiye mwenye maamuzi Juu ya acacia akaanza mazungumzo na serikali.
Barrick aliingia makubaliano na serikali kulipa hizo pesa, either kutoka acacia au yeye mwenyewe akiwa kama mmiliki wa acacia.
Kwa kawaida shareholder mkubwa ndio mwenye maamuzi kwa kampuni husika. Kama alishakubali kulipa kwa kusaini makubaliano basi Acacia hawezi kukataa.
Mwenye uwezo wa tukubali au kukataa kulipa ni Barrick aliyeingia nakubaliana na serikali sio acacia.
Mkanganyiko huwa unatokana na waandishi wetu kutojua ni nani wa kumuuliza. Wameenda kuuliza acacia kama atalipa na acacia akawajibu yeye hana uwezo wa kulipa na wako sawa kwenye jibu maana sio wao waliosema watalipa bali ni baba yao ambaye ni Barrick.
Hii ni sawa nakudai wewe lakini nikaja kumuuliza mtoto wako anilipe, ukiwa nje ya uwezo wake atasema sina uwezo lakini si kwamba sitalipwa kwa sababu nina makubaliano na baba mwenye vyanzo vingi vya mapato kuliko mtoto.
miaka inapita budget zinapita hao barick watalipa lini? je hayo malipo yapo kisheria, he hayo malipo yana accrued interest?
 
Whaaaaaaat???!!! Barrick watapitisha malipo kupitia account ya Acacia?! Without Acacia's Approval? Yaani unachosema ni kwamba, Barrick Gold wana uwezo hata wa ku-withdrawal pesa bila kuhusisha management na bodi ya Acacia...

Man, pamoja na maelezo yako ya awali unaonekana wazi hufahamu nguvu za Barrick zitaishia wapi!!!

This's what Barrick can probably do kwenye hili, assuming wana nia kweli ya kulipa hizo pesa!

Watapeleka agenda mezani for Acacia's approval!

Endapo Acacia wanakataa, pekee ambacho Barrick Gold pengine wanaweza kufanya ni kutumia majority sharing status yao ku-influence kuondolewa kwa management ya Acacia au Bodi ya Acacia (depending nani ni mkaidi) au both (kama power hiyo wanayo)!

Wakiweza kuwatimua, itaajiriwa management na bodi mpya!

Hawa kuingia na kuingia tu wanakumbana na deni la $300M wakati total annual revenue (not profit) as recorded by the company income statement ni:
View attachment 780430

Najua "Wazalendo" mtasema hizo ni data from fraud company (Acacia) but unfortunately, ndizo zitakazotumika tutake tusitake or else, TRA na vyombo vingine vya serikali vi-prove otherwise!!!

That having said, kwa hawa wenzetu hawawezi tu kukurupa kulipa kwa hofu tu ya kuogopa kutimuliwa au kulinda kibarua chao!

Badala ya kujitwisha zigo zito kama hilo, watataka kwanza ku-verify uhalali wa malipo!!!

Moja ya kosa kubwa tulilofanya ambalo nililisema tangu Day 01 ni uchunguzi wa timu ya Prof Mruma kutohusisha Acacia! Matokeo yake, Ripoti yao inakuwa ni ya upande mmoja na ndio maana, according Barrick Gold's 2017 Annual Report, page 174 wanasema:Sasa, kama serikali ina uhakika na findings za akina Profesa Mruma, kwanini basi wanashindwa kutekeleza hilo suala ambalo ni dogo sana?

Ni management na/au bodi ya aina gani zinaweza kulipa unverified debt?!

That having said, Barrick wanaweza ku-influence kutimuliwa bodi na management iliyopo na kisha ikaingia nyingine na hiyo nyingine, kama mwenendo wenyewe ndio huu, na wenyewe wanaweza kugoma!

Hapo tena Barrick Gold watimue na kutimua na kutimua....
deni halipo kisheria, ni pledge kama za harusi tu. management yoyote ile haibanwi kulipa, kabudi na wasiojulikana walishindwa kuwafix kisheria
 


Kama hii habari ni ya kweli,basi kusema kitakachokubalika katika mazungumzo kati ya Barrick na serikali ni lazima kwanza Acacia wayaridhie ndio yakubalike,hakika huu ndio ulikuwa mtego na janja ya hawa wazungu.

Anyway,wacha tusubiri taarifa rasimi kujua ukweli ni upi.

......hawa wanaume kweli kweli........ Ndo tuone sasa uanaume wao
 
Ngozi nyeupe haijawahi kufanya za hesabu za kijinga hivo. Eti wakupe pesa kibwege bwegw tu
 
Taarifa ya Prof. Mruma ilibainisha kuwa madini ya dhahabu yaliyopo ndani ya kontena 277 pale bandarini yana thamani ya shilingi bilioni 1,147 ukilinganisha na shilingi bilioni 97.5 zilizokuwa declared na Acacia. Hivyo tofauti ni shilingi bilioni 1,049.5. Hizi ni hela nyingi sana, badala ya serikali kupoteza muda kugombana na mwekezaji (Acacia) ningekuwa mimi JPM ningeamuru mzigo ukauzwe chini ya usimamizi wa Serikali tupate hiyo bilioni 1,147 cash halafu nawapa chao Acacia na kubakiwa na faida ya shilingi bilioni 1,049.5. Nadhani Acacia wasingekataa mpango huu maana ingewaokoa katika mengi. Sasa ajabu serikali haitaki kuchukua uamuzi huo, wanaogopa nini? nadhani ni hofu ya taarifa za kuchakachua za Mruma. Ndio maana wakiambiwa kuweka wazi taarifa ya Mruma hawataki, wakiambiwa kuchukua sampuli upya kwa pamoja na Acacia ili wakafanye analysis hawataki kurudia kazi hiyo? Matokeo yake tunabishania bil 300, what for? go for the big cake if at all you trust your findings.
 
Back
Top Bottom