Pascal Ndege
JF-Expert Member
- Nov 24, 2012
- 2,977
- 1,897
Tanzania ni nchi pekee kubwa yenye madini na fursa ya kuzungukwa na nchi jirani. Miaka ya zamani kabisa hata sijazaliwa masufuria na vijiko yalitoka Arusha, pasi za mkaa na majembe na spea vilitoka Arusha baada vita ya kagera viwanda vilikufa kabisa.
World Bank wakashauri tulete wawekezaji tukatiii agizo, viwanda vilikufa kabisa tukauza SISO. Kwasasa tumegeuka soko la bidhaa kutoka China, hakuna tena kijiko made in Tanzania.
Sasa hivi kila kijana ni bodaboda au anasubiri teuzi. Kwakuwa chama tawala ni cha kwao, kwanini wasiwezeshwe waende kufufua viwanda? Bidhaa kutoka nje mpaka lini? Good in transit kupitia Bandari za Tanzania kwenda nchi jirani mpaka lini?
Kuna wazee pale SIDO wanajua vile viwanda vilivyokuwa vinafanyakazi, hakuna uchawi wa Mzungu kwa hili na walifanya Watanzania. Tuna kiwanda cha Magari nyumbu kwanini kisiwezeshwe? Kijana upo hapo unapoteza nguvu za kuzalisha mali na kuanza kusambaza propaganda tu.
Tena nakuhakikishia CCM imekuwa, kubwa itafikia mahari utashaangaa mtoto wa mkubwa anatoka from nowhere anapata teuzina wewe upo hapo unatukana kwenye mitandao.
Wang'ang'anieni wafungue viwanda. Masufuria, majiko ya umeme yote yalitengenezwa Arusha hapa. Msidanganywe kuwa Wazungu wanaakili kuwazidi. Ingekuwa enzi zile kama tulitengeneza radio basi simu za mkononi zingekuwa zinatengenezwa hapa.
Wachangamsheni viongozi wenu, nchi ni yenu tu, hakuna mtu wa kuwaambia kitu. Vijana wakiamua lazima wasikilizwe tu. Wabaneni viongozi wenu mshike hatamu ya uchumi wenu, muanze kumiliki viwanda vya bidhaa mbalimbali.
Wasiwaambie serikali haina pesa. Kuna Rais mmoja wa CCM alifanya vitu vingi kabisa kwa pesa hizi hizi. Tatizo pesa zipo ila hazitumiki kimpango, wanagawa kwa machawa, machawa wanakula, wanaamka na njaa.
Wawafungulie viwanda ili mpate pesa, mfanye siasa safi na sio uchawa.
World Bank wakashauri tulete wawekezaji tukatiii agizo, viwanda vilikufa kabisa tukauza SISO. Kwasasa tumegeuka soko la bidhaa kutoka China, hakuna tena kijiko made in Tanzania.
Sasa hivi kila kijana ni bodaboda au anasubiri teuzi. Kwakuwa chama tawala ni cha kwao, kwanini wasiwezeshwe waende kufufua viwanda? Bidhaa kutoka nje mpaka lini? Good in transit kupitia Bandari za Tanzania kwenda nchi jirani mpaka lini?
Kuna wazee pale SIDO wanajua vile viwanda vilivyokuwa vinafanyakazi, hakuna uchawi wa Mzungu kwa hili na walifanya Watanzania. Tuna kiwanda cha Magari nyumbu kwanini kisiwezeshwe? Kijana upo hapo unapoteza nguvu za kuzalisha mali na kuanza kusambaza propaganda tu.
Tena nakuhakikishia CCM imekuwa, kubwa itafikia mahari utashaangaa mtoto wa mkubwa anatoka from nowhere anapata teuzina wewe upo hapo unatukana kwenye mitandao.
Wang'ang'anieni wafungue viwanda. Masufuria, majiko ya umeme yote yalitengenezwa Arusha hapa. Msidanganywe kuwa Wazungu wanaakili kuwazidi. Ingekuwa enzi zile kama tulitengeneza radio basi simu za mkononi zingekuwa zinatengenezwa hapa.
Wachangamsheni viongozi wenu, nchi ni yenu tu, hakuna mtu wa kuwaambia kitu. Vijana wakiamua lazima wasikilizwe tu. Wabaneni viongozi wenu mshike hatamu ya uchumi wenu, muanze kumiliki viwanda vya bidhaa mbalimbali.
Wasiwaambie serikali haina pesa. Kuna Rais mmoja wa CCM alifanya vitu vingi kabisa kwa pesa hizi hizi. Tatizo pesa zipo ila hazitumiki kimpango, wanagawa kwa machawa, machawa wanakula, wanaamka na njaa.
Wawafungulie viwanda ili mpate pesa, mfanye siasa safi na sio uchawa.