Maaskofu na wachungaji 447 wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) kwamba Askofu mkuu wao Zachary Kakobe atakuwa askofu wa kudumu na kila watakapokuwa wanakutana watakuwa wanamptisha bila kupingwa. Msimamo huo waliotuoa jana katika Kanisa la FGBF Mwenge, Dar es Salaam ambapo walikuja kueleza kile kilichojiri katika mkutano wao mkuu huko Dodoma. Maaskofu wote 19 wa FGBF Tanzania nzima walikuwepo na wachungaji zaidi ya 400, isipokuwa 37 ambao pia hawakuhudhuria mkutano wa Dodoma.
Souce: Mimi mwenyewe nilikuwepo kanisani, lakini nawawekea habari kutoka Mwananchi la leo:
Kakobe amechaguliwa tena kuwa Askofu Mkuu wa Kanisa hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Kakobe alichaguliwa kwenye mkutano Mkuu wa kanisa hilo uliofanyika mjini Dodoma Julai 4 hadi 9 mwaka huu.
Akizungumza kwenye ibada maalumu iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana Kakobe aliwaambia waumini wake kuwa alichaguliwa akiwa mgombea pekee katika nafasi hiyo.
Katika uchaguzi ule hakuna mtu aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo, hadi tunaanza mkutano hapakuwa na jina, hali hiyo ndivyo ilivyokuwa hata katika mikutano ya uchaguzi katika vipindi vitatu vilivyopita,alisema Kakobe.
Kakobe alisema hiyo ni kutokana na kanisa lake pamoja na viongozi kuona suala la uongozi na vyeo siyo kitu cha msingi kwa na badala yake kuhubiri neno la Mungu.
Akizungumzia uchaguzi alisema ulitimiza vigezo kwa kuhudhuria na wajumbe wote wa mkutano mkuu ambao ni maaskofu na wachungaji.
Mkutano ulihudhuriwa na wajumbe 447 ambao kati yao ni maaskofu 19 toka kanda zote za Tanzania na wachungaji wote,alisema.
Katiba ya Kanisa
Alisema uchaguzi ulifanyika Dodoma ulikuwa halali na ulitokana na utaratibu uliowekwa na kanisa hilo kwa mujibu wa sheria na katiba na si shinikizo la watu waliofungua kesi mahakamani.
Katiba ibada hiyo Askofu Kakobe alitumia muda mwingi kuzungumzia katiba ya kanisa hilo aliyodai wengi wanaipotosha.
Watu wengi wanatumia katiba hii ya mwaka 1987, wakati huo kanisa hili halikuwapo na kulikuwa na kikundi cha uinjilishaji kilichojulikana kwa Gospel Evangelist Team.
Alisema kikundi hico ambacho yeye alifanya nacho kazi kama kiongozi wake kilikuwa na jukumu la kufundisha injili nchi nzima na kulihusisha mkusanyiko wa vijana kutoka makanisa mbalimbali.
Alisema baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu Kakobe alifanya uchaguzi na kugundua kuwa waumini wake hawakuendelea na imani waliyofundishwa ndipo alipopatwa na maoni ya kuanzaisha kanisa la FGBF.
Alisema hatua hiyo aliifanywa mwaka 1989 alipowasilisha taarifa wizara ya Mambo ya Ndani ya kutaka kubadilishwa kwa jina la Taasisi ya BET na kuwa FGBF.
Alisema baada ya hatua hiyo ndipo walipoandika katiba mpya inayotumika hadi sasa.
Kakobe alifafanua kuwa kwa katiba inampa mamlaka Askofu mkuu kuteua katibu Mkuu, mweka hazina na maaskofu wa majimbo mbalimbali.
Alisema pia askofu huyo ndiyo mwamuzi wa mwisho kwa mujibu wa katiba juu ya mambo yote yahusuyo kanisa ikiwa ni pamoja na nidhamu pamoja na mafundisho.
Katiba inampa mamlaka askofu kuonya na kuwafukuza wanachama au waumini pindi anapoona ipo haja ya kufanya hivyo,alisema Kakobe.
Katika ibada hiyo Kakobe huku akinukuu vifungu vya katiba alimteua na kumtangaza Askofu Nathan Meshack kuwa Katibu Mkuu wa Kanisa hilo na Askofu Jimmy Sekuye kuwa mweka hazina.
Souce: Mimi mwenyewe nilikuwepo kanisani, lakini nawawekea habari kutoka Mwananchi la leo:
Kakobe amechaguliwa tena kuwa Askofu Mkuu wa Kanisa hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Kakobe alichaguliwa kwenye mkutano Mkuu wa kanisa hilo uliofanyika mjini Dodoma Julai 4 hadi 9 mwaka huu.
Akizungumza kwenye ibada maalumu iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana Kakobe aliwaambia waumini wake kuwa alichaguliwa akiwa mgombea pekee katika nafasi hiyo.
Katika uchaguzi ule hakuna mtu aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo, hadi tunaanza mkutano hapakuwa na jina, hali hiyo ndivyo ilivyokuwa hata katika mikutano ya uchaguzi katika vipindi vitatu vilivyopita,alisema Kakobe.
Kakobe alisema hiyo ni kutokana na kanisa lake pamoja na viongozi kuona suala la uongozi na vyeo siyo kitu cha msingi kwa na badala yake kuhubiri neno la Mungu.
Akizungumzia uchaguzi alisema ulitimiza vigezo kwa kuhudhuria na wajumbe wote wa mkutano mkuu ambao ni maaskofu na wachungaji.
Mkutano ulihudhuriwa na wajumbe 447 ambao kati yao ni maaskofu 19 toka kanda zote za Tanzania na wachungaji wote,alisema.
Katiba ya Kanisa
Alisema uchaguzi ulifanyika Dodoma ulikuwa halali na ulitokana na utaratibu uliowekwa na kanisa hilo kwa mujibu wa sheria na katiba na si shinikizo la watu waliofungua kesi mahakamani.
Katiba ibada hiyo Askofu Kakobe alitumia muda mwingi kuzungumzia katiba ya kanisa hilo aliyodai wengi wanaipotosha.
Watu wengi wanatumia katiba hii ya mwaka 1987, wakati huo kanisa hili halikuwapo na kulikuwa na kikundi cha uinjilishaji kilichojulikana kwa Gospel Evangelist Team.
Alisema kikundi hico ambacho yeye alifanya nacho kazi kama kiongozi wake kilikuwa na jukumu la kufundisha injili nchi nzima na kulihusisha mkusanyiko wa vijana kutoka makanisa mbalimbali.
Alisema baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu Kakobe alifanya uchaguzi na kugundua kuwa waumini wake hawakuendelea na imani waliyofundishwa ndipo alipopatwa na maoni ya kuanzaisha kanisa la FGBF.
Alisema hatua hiyo aliifanywa mwaka 1989 alipowasilisha taarifa wizara ya Mambo ya Ndani ya kutaka kubadilishwa kwa jina la Taasisi ya BET na kuwa FGBF.
Alisema baada ya hatua hiyo ndipo walipoandika katiba mpya inayotumika hadi sasa.
Kakobe alifafanua kuwa kwa katiba inampa mamlaka Askofu mkuu kuteua katibu Mkuu, mweka hazina na maaskofu wa majimbo mbalimbali.
Alisema pia askofu huyo ndiyo mwamuzi wa mwisho kwa mujibu wa katiba juu ya mambo yote yahusuyo kanisa ikiwa ni pamoja na nidhamu pamoja na mafundisho.
Katiba inampa mamlaka askofu kuonya na kuwafukuza wanachama au waumini pindi anapoona ipo haja ya kufanya hivyo,alisema Kakobe.
Katika ibada hiyo Kakobe huku akinukuu vifungu vya katiba alimteua na kumtangaza Askofu Nathan Meshack kuwa Katibu Mkuu wa Kanisa hilo na Askofu Jimmy Sekuye kuwa mweka hazina.