Kakobe Askofu Mkuu wa kudumu FGBF

ESAM

JF-Expert Member
Mar 15, 2011
1,164
548
Maaskofu na wachungaji 447 wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) kwamba Askofu mkuu wao Zachary Kakobe atakuwa askofu wa kudumu na kila watakapokuwa wanakutana watakuwa wanamptisha bila kupingwa. Msimamo huo waliotuoa jana katika Kanisa la FGBF Mwenge, Dar es Salaam ambapo walikuja kueleza kile kilichojiri katika mkutano wao mkuu huko Dodoma. Maaskofu wote 19 wa FGBF Tanzania nzima walikuwepo na wachungaji zaidi ya 400, isipokuwa 37 ambao pia hawakuhudhuria mkutano wa Dodoma.

Souce: Mimi mwenyewe nilikuwepo kanisani, lakini nawawekea habari kutoka Mwananchi la leo:

Kakobe amechaguliwa tena kuwa Askofu Mkuu wa Kanisa hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Kakobe alichaguliwa kwenye mkutano Mkuu wa kanisa hilo uliofanyika mjini Dodoma Julai 4 hadi 9 mwaka huu.

Akizungumza kwenye ibada maalumu iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana Kakobe aliwaambia waumini wake kuwa alichaguliwa akiwa mgombea pekee katika nafasi hiyo.

“Katika uchaguzi ule hakuna mtu aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo, hadi tunaanza mkutano hapakuwa na jina, hali hiyo ndivyo ilivyokuwa hata katika mikutano ya uchaguzi katika vipindi vitatu vilivyopita,”alisema Kakobe.

Kakobe alisema hiyo ni kutokana na kanisa lake pamoja na viongozi kuona suala la uongozi na vyeo siyo kitu cha msingi kwa na badala yake kuhubiri neno la Mungu.

Akizungumzia uchaguzi alisema ulitimiza vigezo kwa kuhudhuria na wajumbe wote wa mkutano mkuu ambao ni maaskofu na wachungaji.

“Mkutano ulihudhuriwa na wajumbe 447 ambao kati yao ni maaskofu 19 toka kanda zote za Tanzania na wachungaji wote,”alisema.

Katiba ya Kanisa
Alisema uchaguzi ulifanyika Dodoma ulikuwa halali na ulitokana na utaratibu uliowekwa na kanisa hilo kwa mujibu wa sheria na katiba na si shinikizo la watu waliofungua kesi mahakamani.

Katiba ibada hiyo Askofu Kakobe alitumia muda mwingi kuzungumzia katiba ya kanisa hilo aliyodai wengi wanaipotosha.

“Watu wengi wanatumia katiba hii ya mwaka 1987, wakati huo kanisa hili halikuwapo na kulikuwa na kikundi cha uinjilishaji kilichojulikana kwa Gospel Evangelist Team.

Alisema kikundi hico ambacho yeye alifanya nacho kazi kama kiongozi wake kilikuwa na jukumu la kufundisha injili nchi nzima na kulihusisha mkusanyiko wa vijana kutoka makanisa mbalimbali.

Alisema baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu Kakobe alifanya uchaguzi na kugundua kuwa waumini wake hawakuendelea na imani waliyofundishwa ndipo alipopatwa na maoni ya kuanzaisha kanisa la FGBF.

Alisema hatua hiyo aliifanywa mwaka 1989 alipowasilisha taarifa wizara ya Mambo ya Ndani ya kutaka kubadilishwa kwa jina la Taasisi ya BET na kuwa FGBF.

Alisema baada ya hatua hiyo ndipo walipoandika katiba mpya inayotumika hadi sasa.

Kakobe alifafanua kuwa kwa katiba inampa mamlaka Askofu mkuu kuteua katibu Mkuu, mweka hazina na maaskofu wa majimbo mbalimbali.

Alisema pia askofu huyo ndiyo mwamuzi wa mwisho kwa mujibu wa katiba juu ya mambo yote yahusuyo kanisa ikiwa ni pamoja na nidhamu pamoja na mafundisho.

“Katiba inampa mamlaka askofu kuonya na kuwafukuza wanachama au waumini pindi anapoona ipo haja ya kufanya hivyo,”alisema Kakobe.

Katika ibada hiyo Kakobe huku akinukuu vifungu vya katiba alimteua na kumtangaza Askofu Nathan Meshack kuwa Katibu Mkuu wa Kanisa hilo na Askofu Jimmy Sekuye kuwa mweka hazina.

 
Kakobe na FGBF sawa na Messi na Barca, hakuna wa kumweka benchi

Huwezi kuwadanganya watu wote wakati wote. Kuna siku waumini wake watadai uhuru na demokrasia katika kanisa lao, maana kanisa lao viongozi wanachaguliwa na sio kuteuliwa. Haiwezekani wachungaji???/maaskofu??? wote wakawa hawataki ulaji!!!!!!!!! Nani asiye na watoto, mke/wake??? ambao wanataka matunzo, elimu etc, nani asiyetaka kujenga nyumba kwa familia yake baadaye waachie watoto in case etc. Kuna siku watadai demokrasia.
 
Huwezi kuwadanganya watu wote wakati wote. Kuna siku waumini wake watadai uhuru na demokrasia katika kanisa lao, maana kanisa lao viongozi wanachaguliwa na sio kuteuliwa. Haiwezekani wachungaji???/maaskofu??? wote wakawa hawataki ulaji!!!!!!!!! Nani asiye na watoto, mke/wake??? ambao wanataka matunzo, elimu etc, nani asiyetaka kujenga nyumba kwa familia yake baadaye waachie watoto in case etc. Kuna siku watadai demokrasia.

Kanisani huwa hakuna demokrasia, huwa kuna theokrasia. Mambo ya FGBF yanawahusu wao ndiyo maana maaskofu na wachungaji wakafanya hivyo kwani wanajua uzuri na ubora wa Kakobe basi. Na huwezi kusema kadanganya, mtu mmoja atadanganya watu 400+. Wenyewe wamesema FGBF ni ndege ya kuwapeleka mbinguni na rubani wake ni Kakobe tu mpaka atakapokufa Mungu atawapatia mwingine lakini kwa sasa huwaambii kitu bwana hata uje na tuhuma gani wao wanamjua.

Halafu ndugu yangu kanisani hakuna ulaji. Kwa mfumo wa FGBF waumini wa kanisa la mahali (local church) ndiyo wanahakikisha mchungaji wao anapata mahitaji yote anayotaka. Na kwa kanisa la DSM lazima washirika wa hapa wahakikishe Kakobe kama mchungaji wao anapata mahitaji yote muhimu ili aweze kuwahudumia vizuri, ndiyo maana hana shamba, duka wala akaunti benki
 
Kanisani huwa hakuna demokrasia, huwa kuna theokrasia. Mambo ya FGBF yanawahusu wao ndiyo maana maaskofu na wachungaji wakafanya hivyo kwani wanajua uzuri na ubora wa Kakobe basi. Na huwezi kusema kadanganya, mtu mmoja atadanganya watu 400+. Wenyewe wamesema FGBF ni ndege ya kuwapeleka mbinguni na rubani wake ni Kakobe tu mpaka atakapokufa Mungu atawapatia mwingine lakini kwa sasa huwaambii kitu bwana hata uje na tuhuma gani wao wanamjua.

Halafu ndugu yangu kanisani hakuna ulaji. Kwa mfumo wa FGBF waumini wa kanisa la mahali (local church) ndiyo wanahakikisha mchungaji wao anapata mahitaji yote anayotaka. Na kwa kanisa la DSM lazima washirika wa hapa wahakikishe Kakobe kama mchungaji wao anapata mahitaji yote muhimu ili aweze kuwahudumia vizuri, ndiyo maana hana shamba, duka wala akaunti benki


Kaka umeweka hii thread kwa ajili ya maoni ya watu sasa unachofanya ni kumtetea kakobe why? ina maana hamna uhuru wa maoni?
 
Kanisa la kakobe wameamua kumuchagua kakobe , na watu wote wanaakiri timamu, na ndio maana wamehama kutoka kwenye makanisa mengine na kwenda hapo, hata wakaamua kujiwekea kiongozi wao hata kama wataamua atawle milele.

Sasa kwa nini watu wasio wa fgbf waingilie uchaguzi wa fgbf?

Kwa nini ccm na mafisadi wanaiingilia uchaguzi wa makanisa??

Mwaka jana akina lowasa walitaka kuingilia uchaguzi wa kkkt leo watu wanahoji uteuzi wa kakobe wakati hawayatambui mafundisho ya kakobe!!!


Sasa wewe kama hutambui ulokole kwa nini uhoji uchaguzi wa ulokole???

Huu ndio udini!!!
Kuingilia maamuzi ya dini nyingine!!!

John worsey alipinga mambo ya katoliki akajitoa huko na kuanzisha huduma yake na wala hakuhoji mambo ya katoliki!!!

Martini ruther aliasi katoliki , na kuanzisha kkkt na hakuwahi kuhoji mambo ya katoliki!!!


Sasa wewe unahoji uteuzi wa kakobe , je wewe ni fgbf ? Au unatumika na ccm
 
cha maana hapa mambo mengi huwa tunayachukulia vijiweni. watanzania tuanze kufuatilia mambo kwa kina sio kwa kusoma vichwa vya magazeti.
 
Kanisa la kakobe wameamua kumuchagua kakobe , na watu wote wanaakiri timamu, na ndio maana wamehama kutoka kwenye makanisa mengine na kwenda hapo, hata wakaamua kujiwekea kiongozi wao hata kama wataamua atawle milele.Sasa kwa nini watu wasio wa fgbf waingilie uchaguzi wa fgbf?Kwa nini ccm na mafisadi wanaiingilia uchaguzi wa makanisa??Mwaka jana akina lowasa walitaka kuingilia uchaguzi wa kkkt leo watu wanahoji uteuzi wa kakobe wakati hawayatambui mafundisho ya kakobe!!!Sasa wewe kama hutambui ulokole kwa nini uhoji uchaguzi wa ulokole???Huu ndio udini!!!Kuingilia maamuzi ya dini nyingine!!!John worsey alipinga mambo ya katoliki akajitoa huko na kuanzisha huduma yake na wala hakuhoji mambo ya katoliki!!!Martini ruther aliasi katoliki , na kuanzisha kkkt na hakuwahi kuhoji mambo ya katoliki!!!Sasa wewe unahoji uteuzi wa kakobe , je wewe ni fgbf ? Au unatumika na ccm[/QUAcha uongu ndugu usiwe shabiki aliyepitiliza achafact ziongee zenyewe unatudanganya martin luther hakuanzisha kkkt.kkkt maana yake kanisa la kiinjili la kilutheri la kitanzania.martin luther alikuwa mjerumani na kanisa lililoanzishwa na yeye siyo kkkt ila kkkt ilianzishwa na wamishionary wa kiluther kutoka ujerumani.
 
Jamani mwamakula muongo kabisa kkkt ilianzishwa na wamishenari wa kilutheri kutoka ujerumani na siyo martin luther.
 
Tunapo angalia namna ya hizi chaguzi za makanisa tusisahau pia kwamba RC nayo papa akiisha chaguliwa ni mpaka kifo kimtenganishe nao
.
 
Huwezi kuwadanganya watu wote wakati wote. Kuna siku waumini wake watadai uhuru na demokrasia katika kanisa lao, maana kanisa lao viongozi wanachaguliwa na sio kuteuliwa. Haiwezekani wachungaji???/maaskofu??? wote wakawa hawataki ulaji!!!!!!!!! Nani asiye na watoto, mke/wake??? ambao wanataka matunzo, elimu etc, nani asiyetaka kujenga nyumba kwa familia yake baadaye waachie watoto in case etc. Kuna siku watadai demokrasia.

Tatizo lako wewe unawaza ya duniani, wakati watumishi hawa wa Mungu wanawaza ya mbinguni. Hawako pale kwa ajili ya maslahi yao binafsi wala kutafuta ulaji. Wanawaza kumtumikia Bwana usiku na mchana, wametoa maisha yao kwa ajili hiyo tu. Askofu Kakobe mwenyewe pamoja na ukubwa wa kanisal analolichunga hajawahi kujenga nyumba yeyote kwa pesa ya kanisa. Nyumba anayokaa ni nyumba aliyoijenga mwenyewe kabla hajaitwa kuwa mchungaji. Gari analotumia amenunuliwa na watu kwa hiari yao wenyewe bila hata yeye kujua mpaka siku waliyomkabidhi. Hawazi hata siku moja kuweka uwekezaji wowote kwa ajili yake au familia yake. Na hata wachungaji wake wako hivyo hivyo.

Katika utumishi wa Kristo watu hawakimbilii ukubwa na hakuna kitu kinachoitwa demokrasia kwa sababu ni Mungu mwenyewe ndiye anayewaweka watumishi wake. Mungu ndiye alimchangua Musa, Joshua, Eliya, Elisha, Petro, Paulo na wengine wengi.
 
Mkuu ! Je, inawezekanaje mtoto kuwa Baba ?
Ndio maana Askofu Kakobe atakuwa askofu mkuu mpaka kifo;kama papa katoliki.
 
Kaka umeweka hii thread kwa ajili ya maoni ya watu sasa unachofanya ni kumtetea kakobe why? ina maana hamna uhuru wa maoni?

Ndo mnaanza kuingia siasa kanisani? UKAWA, ACT na wengineo kule hakuna hoja tena? Mbona Papa anadumu mpaka anapoamua mwenyewe! Tungemlaumu ZAKARIA KAKOBE kama angefanya hujuma kwa wagombea wenza endapo wangejitokeza. Acheni kutembea uchi kichwani!
 
Kanisa la kakobe wameamua kumuchagua kakobe , na watu wote wanaakiri timamu, na ndio maana wamehama kutoka kwenye makanisa mengine na kwenda hapo, hata wakaamua kujiwekea kiongozi wao hata kama wataamua atawle milele.

Sasa kwa nini watu wasio wa fgbf waingilie uchaguzi wa fgbf?

Kwa nini ccm na mafisadi wanaiingilia uchaguzi wa makanisa??

Mwaka jana akina lowasa walitaka kuingilia uchaguzi wa kkkt leo watu wanahoji uteuzi wa kakobe wakati hawayatambui mafundisho ya kakobe!!!


Sasa wewe kama hutambui ulokole kwa nini uhoji uchaguzi wa ulokole???

Huu ndio udini!!!
Kuingilia maamuzi ya dini nyingine!!!

John worsey alipinga mambo ya katoliki akajitoa huko na kuanzisha huduma yake na wala hakuhoji mambo ya katoliki!!!

Martini ruther aliasi katoliki , na kuanzisha kkkt na hakuwahi kuhoji mambo ya katoliki!!!


Sasa wewe unahoji uteuzi wa kakobe , je wewe ni fgbf ? Au unatumika na ccm
John Huss alijitoa Roman catholic akaanzisha Moravian Church
 
Mkuu ! Je, inawezekanaje mtoto kuwa Baba ?
Ndio maana Askofu Kakobe atakuwa askofu mkuu mpaka kifo;kama papa katoliki.

hao wengine wakitaka kuwa askofuu mkuu wakafungue makanisa yao lile nila kakobe akifa na huduma yake imekwisha
 
Back
Top Bottom