Kakobe aitunishia misuli TANESCO

kama wachangiaji wengine wanavyosema,ni kweli kwamba Kakobe hana haki katika hili kama anvyodai,nadhani tatizo ni uelewa wa sheria husika.ukisoma sheria iliyoanzisha Tanesco(TANESCO ACT),shera ya ardhi ambayo ni sheria namba 4 ya mwaka 1999,pamoja na sheria ya mipango miji (COUNTRY AND PLANNING ACT) ziko wazi kuhusu kile ambacho tanesco wanataka kufanya.Ila tatizo la nchi yetu utekelezaji wa sheria umekuwa ni ndoto,kwani kakobe hajaanza kuishi pale leo.
 
Heshima wakuu,
Katika miradi kama huu licha ya EIA kutakiwa kufanywa ilitakiwa pia Social Impact Assessment ifanyike na wale wote watakaoguswa na mradi ikiwa Gospel church wahusishe na kutoa madukuduku yao halafu maoni yao yafanyiwe kazi kwa uwazi na kuwapa matokeo utatuzi wa madukuduku yao wahusika mfano mzuri ni ujenzi wa barabara ya horohoro na baada ya hapo ndio mradi unaweza kuendelea sijui kama Tanesco walizangatia hivyo maana wangekuwa na ufumbuzi wa tatizo la kanisa la kakobe
Nawasilisha
 
hawa waumini wa Kakobe wapo mpaka leo hii tar 25/01/2010, wanalala pale masaa 24.
hivi tujiulize katika nchi masikini kama hii, nguvu ya kuwashindisha na kuwalaza watu zaidi ya 100 pale inatoka wapi?
wanzetu (ambao wanaheshimu muda na kufanya kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo) huwa wanafanya maandamano makubwa kuonyesha kuchukizwa na kitu na si kukaa na kulala zaidi ya mwezi.
makanisa kama haya yenye mwelekeo wa ushawishi kwa watu wasifanye kazi kwa bidii ni hatari sana kwani yanarudisha nyuma maendeleo ya wananchi wengi

hili suala linanikera sana mimi binafsi

ni vyema vyombo husika vikapiga marufuku hali hii wananchi waondoke pale wakafanye kazi

wana JF mnasemaje?
 
Ukweli unabaki palepale na haya ndio madhara ya kubakisha viporo hili la richmond wanalihusisha na mambo ya maendeleo ya kupitisha nguzo za umeme sasa kakobe acha mizengwe na serikali malizeni longolongo za richmond
 
Makanisa siku hizi hawapiganii waumini kufika peponi, wanatafuta utajiri, mali na ukuu hapahapa Duniani.
 
Kakobe anastahili kuwekwa kwenye lile kundi la Mapapa la mzee Mengi kwa sababu anafanya watu waache shughuli zao kulinda kanisa kwa ajili ya maslahi yake mwenyewe huku akitumia jina la Mungu.
sawa lakini hata mawazo hasi kama yako ni ufisadi pia, nijuavyo mimi kanisa siyo kakobe kwa imani ya kikristo may be kuringana na imani mitaani.com tunaweza kukubaliana na wewe
 
Mwisho wa utapeli wa Kakobe unakaribia.
Kama anataka siasa aingie tu mzima mzima kama Mtikila.Hao vijana 70 woote wanaingia selo moja tu!!
Tanesco ni shirika la serikali na si la mtu na kujidai kupambana na Tanesco ni kuvua shati ili upambane na serikali.
Kanisa la Kakobe liko barabarani, halina parking wala sidhani kama lina kibali cha kukalisha waumini wengi katika confined space.
Hili suala la Kakobe Vs Tanesco litamuumbua.
hakuna watu hakuna serikali, hivyo serikali isiyoja utu wa watu haifai ni serikali ya kuzimu na kuongozwa na ndoto, utabiri, na uchawi kwa akili zako ndogo unadhani ingekuwa pana msikiti wa manyema pale tanesco wangepeleka ufirauni huo? hata kama shule hukusoma kupunguza ujinga hapo tumia akili ya kuzaliwa kama pia huna tumia akili ya vijiweni
 
Mimi nilitegemea Bwana Askofu Kakobe angekuwa msitari wa mbele kumaliza matatizo kama haya kwa njia za amani zenye kuonyesha UWEPO WA MUNGU badala yake yeye anatumia njia za kibabe, vitisho vya mapambano bila silaha ambayo mwisho wa siku ni uvunjifu wa amani na kumwagika damu isiyo na hatia kwa ajili ya ubinafsi wa kutaka kuzuia swala muhimu lenye maslahi ya taifa. Ni rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko mwenye dhambi kufika mbinguni.

Umesema vyema, yeye kama Askofu angelitatua suala hili kibusara zaidi na sio kuanzisha upinzani usiokuwa na maana.
 
LICHA ya mazungumzo ya takribani wiki mbili kati ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja pamoja na Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Fellowship, Zachary Kakobe kuhusu mgogoro uliozuka wa waumini wa kanisa hilo kupinga Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kupitisha njia ya umeme wa msongo mkubwa wa kilovoti 132 mbele ya kanisa hilo, serikali imejikuta njia panda katika kufikia uamuzi.


Taarifa ambazo zililifikia gazeti hili jana zilieleza kwamba baada ya mazungumzo ya viongozi hao kumalizika wiki iliyopita, wataalamu wa wizara hiyo walikaa pamoja, ili kufikia uamuzi. lakini ukazuka mparaganyiko ambao uliwagawa, wengine wakaishauri serikali iwapuze huku wengine wakiwaunga mkono wakisema wana hoja ya msingi.


Hali hiyo, imempa wakati mgumu Waziri Ngeleja katika kutoa uamuzi, hasa ikizingatiwa kwamba baadhi ya wataalamu wake wanadai kwamba tayari mamilioni ya fedha yametumika katika njia hiyo jambo ambalo litaisababishia serikali hasara na hata kuwakasirisha wafadhili.


Kwa mujibu wa wataalamu hao, tayari Tanesco wamejenga misingi na kuweka vifaa kwa ajili ya kufunga nguzo upande wa kanisa hilo lililopo barabara ya Sam Nujoma, Mwenge, jijini Dar es Salaam na kwamba kuhamishia upande wa pili itawagharimu fedha nyingi ambazo kiwango chake hakikutajwa, lakini ikadaiwa ni mamilioni ya fedha.


Wataalamu hao wanadai kuwa hata upande wa pili wa barabara hiyo, kuna ubishi wa kuruhusu njia hiyo kujengwa ingawa ndiko kuna nafasi kubwa iliyobaki kwa hifadhi ya barabara ukilinganisha na upande wa kanisa.


Baadhi ya wataalamu wanaounga mkono msimamo wa waumini hao, wanadai kwamba sababu zilizotolewa na kanisa hilo ni za msingi na zinapaswa kuheshimiwa.


Miongoni mwa hoja za waumini hao ni kwamba kuwepo kwa njia hiyo ya msongo mkubwa kutasababisha muingiliano na mashine za kurekodi na kunasa sauti ndani ya kanisa hilo.


Isitoshe mpango huo utaathiri moja kwa moja mkakati wa kanisa hilo kuwa na kituo cha televisheni kwenye eneo hilo.


Wiki iliyopita Ngeleja alisema atatoa uamuzi wake wiki hii na juhudi za kumpata jana ziligonga ukuta baada ya simu yake ya mkononi kutopatikana.


Mwananchi liliwasiliana na Naibu wake, Adam Malima, lakini alisema asingeweza kuelezea jambo lolote kuhusu suala hilo na isitoshe alikuwa kwenye kikao.


Mwananchi jana lilishuhudia waumini wa kanisa hilo wakiendelea kutoa ulinzi baada ya Tanesco kuwa na mpango wa kung’oa mabango mawili mbele ya kanisa hilo, ili kupisha njia hiyo ya umeme.


Kakobe aliliambia Mwananchi kwamba baada ya kumaliza mazungumzo na Ngeleja, wanasubiri uamuzi wa serikali baada ya kushauriana na wataalamu wake.
 
LICHA ya mazungumzo ya takribani wiki mbili kati ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja pamoja na Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Fellowship, Zachary Kakobe kuhusu mgogoro uliozuka wa waumini wa kanisa hilo kupinga Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kupitisha njia ya umeme wa msongo mkubwa wa kilovoti 132 mbele ya kanisa hilo, serikali imejikuta njia panda katika kufikia uamuzi.


Taarifa ambazo zililifikia gazeti hili jana zilieleza kwamba baada ya mazungumzo ya viongozi hao kumalizika wiki iliyopita, wataalamu wa wizara hiyo walikaa pamoja, ili kufikia uamuzi. lakini ukazuka mparaganyiko ambao uliwagawa, wengine wakaishauri serikali iwapuze huku wengine wakiwaunga mkono wakisema wana hoja ya msingi.


Hali hiyo, imempa wakati mgumu Waziri Ngeleja katika kutoa uamuzi, hasa ikizingatiwa kwamba baadhi ya wataalamu wake wanadai kwamba tayari mamilioni ya fedha yametumika katika njia hiyo jambo ambalo litaisababishia serikali hasara na hata kuwakasirisha wafadhili.


Kwa mujibu wa wataalamu hao, tayari Tanesco wamejenga misingi na kuweka vifaa kwa ajili ya kufunga nguzo upande wa kanisa hilo lililopo barabara ya Sam Nujoma, Mwenge, jijini Dar es Salaam na kwamba kuhamishia upande wa pili itawagharimu fedha nyingi ambazo kiwango chake hakikutajwa, lakini ikadaiwa ni mamilioni ya fedha.


Wataalamu hao wanadai kuwa hata upande wa pili wa barabara hiyo, kuna ubishi wa kuruhusu njia hiyo kujengwa ingawa ndiko kuna nafasi kubwa iliyobaki kwa hifadhi ya barabara ukilinganisha na upande wa kanisa.


Baadhi ya wataalamu wanaounga mkono msimamo wa waumini hao, wanadai kwamba sababu zilizotolewa na kanisa hilo ni za msingi na zinapaswa kuheshimiwa.


Miongoni mwa hoja za waumini hao ni kwamba kuwepo kwa njia hiyo ya msongo mkubwa kutasababisha muingiliano na mashine za kurekodi na kunasa sauti ndani ya kanisa hilo.


Isitoshe mpango huo utaathiri moja kwa moja mkakati wa kanisa hilo kuwa na kituo cha televisheni kwenye eneo hilo.


Wiki iliyopita Ngeleja alisema atatoa uamuzi wake wiki hii na juhudi za kumpata jana ziligonga ukuta baada ya simu yake ya mkononi kutopatikana.


Mwananchi liliwasiliana na Naibu wake, Adam Malima, lakini alisema asingeweza kuelezea jambo lolote kuhusu suala hilo na isitoshe alikuwa kwenye kikao.


Mwananchi jana lilishuhudia waumini wa kanisa hilo wakiendelea kutoa ulinzi baada ya Tanesco kuwa na mpango wa kung’oa mabango mawili mbele ya kanisa hilo, ili kupisha njia hiyo ya umeme.


Kakobe aliliambia Mwananchi kwamba baada ya kumaliza mazungumzo na Ngeleja, wanasubiri uamuzi wa serikali baada ya kushauriana na wataalamu wake.
Kutokana na ubabe huo wa TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini, kulazimisha kupitisha nguzo za msongo mkubwa katika kanisa hilo na kung''oa mabango ya kanisa hilo, jambo ambalo lilikuwa chukizo kubwa kwa Mungu.

Hivi sasa laana inazidi kuwatafuna serikali ya CCM, sawa sawa kabisa na maono aliyoyaeleza wakati huo, Mtumishi wa Mungu, Zacharia Kakobe, kuwa kutokana na kiburi na ubabe wa hali ya juu ulioonyeshwa na viongozi wa wizara hiyo ya Nishati na Madini dhidi ya kanisa hilo la Mungu, alitabiri mambo mawili makubwa yatatokea.

Mosi, alibainisha kuwa umeme huo wa msongo mkubwa uliopita hapo kanisani, hautakuja kamwe kuja kuwaka, jambo ambalo kweli lilitokea ambapo hadi leo, umeme huo uliopita kanisani hapo haujawahi kuwaka!

Kama kuna ofisa yeyote wa TANESCO atataka kulipinga hilo, ajitokeze hadharani kulikanusha hilo.

Pili, alitabiri kuwa wizara hiyo ya Nishati na Madini, itaendelea kukumbwa na laana kwa viongozi wake wakuu kukumbwa na kashfa mbalimbali, zitakazofanya watimuliwe kwenye nafasi zao.

Utimilifu wa utabiri huo tumeshuhudia tokea mwaka huo wa 2009, wizara hiyo ikijikuta Mawaziri na Makatibu wakuu wake wanashindwa kudumu kwenye wizara hiyo.

Tulishuhudia kipindi hicho, Waziri Ngeleja na Katibu wake mkuu Jairo, wakitimuliwa kwenye nafasi zao.

Hivi sasa tumeshuhudia pia Katibu mkuu Maswi na Waziri wake 'kiporo' Muhongo nao wakilazimika kung'oka toka wizarani hapo.

Ni wazi sasa serikali ya Sisiem itakuwa imepata 'somo' muhimu kuwa siyo jambo jema na la busara kulumbana, kuwanyanyasa na kuwapuuza watumishi wa Mungu, kama walivyofanya kwa huyo Askofu Kakobe.
 
Uaskofu sijui aliupataje maana ni mtu wa pumba na kuamini ushirikina mda wote. Ukizuia umeme je wengine wasipate huduma hiyo? Mbona unakuwa mbinafsi hvyo?
 
Kakobe kapata uaskofu kwa kuchaguliwa na mkutano mkuu wa kanisa lake ili kuwaongoza maaskofu wa majimbo na wachungajie.
 
Kutokana na ubabe huo wa TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini, kulazimisha kupitisha nguzo za msongo mkubwa katika kanisa hilo na kung''oa mabango ya kanisa hilo, jambo ambalo lilikuwa chukizo kubwa kwa Mungu.

Hivi sasa laana inazidi kuwatafuna serikali ya CCM, sawa sawa kabisa na maono aliyoyaeleza wakati huo, Mtumishi wa Mungu, Zacharia Kakobe, kuwa kutokana na kiburi na ubabe wa hali ya juu ulioonyeshwa na viongozi wa wizara hiyo ya Nishati na Madini dhidi ya kanisa hilo la Mungu, alitabiri mambo mawili makubwa yatatokea.

Mosi, alibainisha kuwa umeme huo wa msongo mkubwa uliopita hapo kanisani, hautakuja kamwe kuja kuwaka, jambo ambalo kweli lilitokea ambapo hadi leo, umeme huo uliopita kanisani hapo haujawahi kuwaka!

Kama kuna ofisa yeyote wa TANESCO atataka kulipinga hilo, ajitokeze hadharani kulikanusha hilo.

Pili, alitabiri kuwa wizara hiyo ya Nishati na Madini, itaendelea kukumbwa na laana kwa viongozi wake wakuu kukumbwa na kashfa mbalimbali, zitakazofanya watimuliwe kwenye nafasi zao.

Utimilifu wa utabiri huo tumeshuhudia tokea mwaka huo wa 2009, wizara hiyo ikijikuta Mawaziri na Makatibu wakuu wake wanashindwa kudumu kwenye wizara hiyo.

Tulishuhudia kipindi hicho, Waziri Ngeleja na Katibu wake mkuu Jairo, wakitimuliwa kwenye nafasi zao.

Hivi sasa tumeshuhudia pia Katibu mkuu Maswi na Waziri wake 'kiporo' Muhongo nao wakilazimika kung'oka toka wizarani hapo.

Ni wazi sasa serikali ya Sisiem itakuwa imepata 'somo' muhimu kuwa siyo jambo jema na la busara kulumbana, kuwanyanyasa na kuwapuuza watumishi wa Mungu, kama walivyofanya kwa huyo Askofu Kakobe.
kwa tahadhari yako tu muogope sana Kakobe kwa maana ni mtumishi wa Mungu wa viwango vya juu mno.Umeme mpaka leo miaka 6 umeshindwa kuwaka,unaishia kwenye nguzo wanayo bishania.Tanesco muogopeni Mungu.NAYAUNGA MKONO MAONI YAKO
 
kwa tahadhari yako tu muogope sana Kakobe kwa maana ni mtumishi wa Mungu wa viwango vya juu mno.Umeme mpaka leo miaka 6 umeshindwa kuwaka,unaishia kwenye nguzo wanayo bishania.Tanesco muogopeni Mungu

Acha uongo wewe, umeme unapita kama kawa na hakuna tatizo, halafu unasema kakobe ni mtumishi wa mungu! Mungu yupi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom