Sijui sheria zetu zinasemaje kwa hili ila kwa kawaida sehemu inayopitishwa waya za umeme (waya za simu, mabomba ya maji, mabomba ya maji machafu, waya za fiber optics etc) ni public; mafundi wa umeme wanaweza kufika ndani ya eneo hilo wakati wowote kufanya matengenezohilo bila ya kushtakiwa kwa trespassing. Inapokuwa ni lazima waya hizo zipite kwenye kiwanja cha mtu, basi hilo hufanyika kabla mtu yule hajapewa na kuruhusiwa kujenga kwenye kiwanja hicho, na huambiwa kabisa kuwa ndani ya kiwanja hicho kuna eneo la public kwa ajili ya waya za umeme; asichimbe (kama ni undergraoudn) bila kutaoa taarifa kwa ofisi husika. In fact ujenzi wa nyumba yake utaruhusiwa tu iwapo hauingiliani sana na njia za waya hizo.
Vile vile taratibu nyingi za mipango miji huwa zinatenga eneo la umbali fulani pembeni mwa barabara kwa ajili ya infrastructure, yaani zinamopita waya hizo za umeme, waya za simu, fiber optic cables kwa ajili ya CABLE TV na Broadband internet, mabomba ya maji safi na mabomba ya maji machafu. Ndiyo maana ile Hotel ya Crest kule Arusha ilibomolewa kwa vile ilikuwa inaingia ndani ya eneo hilo.
Wakati mwingine plan za mipangomiji huacha maeneo mengine ya wazi kwa makusudi hata kama hakuna barabara kwa ajili ya future expansions za infrastructure.
Mina naona kama vile kwenye huu ugonvi baina ya Kakobe na TANESCO kuna possibilities tatu.
(1) Kakobe amejenga kwenye eneo la karibu sana na barabara na hivyo kuwa eme-encroach public land ambayo TANESCO wana haki nayo. NI LAZIMA KAKOBE ATII AMRI; Ni lazima asuate fundisho la Yesu kuwa Ya Kaizari mpe Kaizari
(2) Kakobe kajenga ndani ya eneo ambalo lilikuwa limeachwa wazi kwa ajili ya infrastructure, ambalo TANESCO wana haki nalo. NI LAZIMA KAKOBE ATII AMRI; Ni lazima asuate fundisho la Yesu kuwa Ya Kaizari mpe Kaizari
(3) TANESCO wameona ni convenient kuptisha waya zao ndani ya eneo halali la Kakobe ambalo halikuwa limetengwa kwa ajili ya public infrastructure na city planners. Itabidi TANESCO waache ubabe huo; hawawezi kuamua kuptisha transmission lines mahali popte pale. Namna hiyo wataweza kutupitishia transmission line hizo vyumbani mwetu.