Inategemeana ni watu wa aina gani waliomuelekeza kakakuona kutabiri. maana huw kunahitajika wazee wa zamani wanaojua namna ya kuongea naye. Kwa kizazi hiki cha sasa wala sidhani kama kuna yeyote mwenye huo ujuzi wa kuongea na kaka kuona. Kijijini kwetu alitokea na wazee wakafanya walichoweza, na baada ya hapo wakatuambia ni nini kakakuona kakitabiri, na hali ilikuwa kama ilivyotabiriwa. Binafsi, kwa kiasi fulani namwamini huyu mnyama, maana mara nyingi hutokea mara moja kwa mwaka na huwa inaweza kutokea kwamba katika nchi nzima akaonekana mahali pamoja tu.kwa hiyo 'walimtoa lock' kwanza ndo wakamwekea vitu atabiri
Wewe Asigwa itabidi uni-pm ili kuanzia leo tuwe marafiki! Kama kweli hadi sasa tena kwenye jukwaa la GT kama hili lakini bado watu wana imani za kale za karne ya 18 basi ni dhahiri kabisa kuwa kuwa Watanzania ni ajabu jipya la 8 duniani! Ndio maana hata nchi inaongozwa kimazingaombwe tu!inabidi siku moja ujipigie kura aisee maana kuwa mtanzania ni sehemu ya maajabu saba ya dunia aisee
Wewe Asigwa itabidi uni-pm ili kuanzia leo tuwe marafiki! Kama kweli hadi sasa tena kwenye jukwaa la GT kama hili lakini bado watu wana imani za kale za karne ya 18 basi ni dhahiri kabisa kuwa kuwa Watanzania ni ajabu jipya la 8 duniani! Ndio maana hata nchi inaongozwa kimazingaombwe tu!
Baada ya kutabiri huyo kakakuona alielekea wapi?
Huyo mnyama ndo kwanza namsikia sasa,hivi yukoje mkuu jaribu kunifafanulia,ukubwa wa maumbile na makazi yake haswa ni wapi?...majini au nchi kavu?...Je kuna matukio ya nyuma amewahi kutabiri na kutokea kweli?...Pia kihistoria ni makabila yote Tanzania yanaamini utabiri huo?...Kuuliza si ujinga!
Tukamtafute eee?
Ha ha ha haah!! Tukamtafute ndio huenda akatabiri tofauti....