Una lako jamboo wewee naona mnakuja na style nyingii na badoooooo,sie wengine tuna ndungu zetu huko wanatujaliii sanaaa, kwa hiyo huyo kaka yako ni roho yakee tu kama marehemu Lukindo
Umerudi lini bongo?
Nina kaka wa damu ughaibuni ila amenitenga na hivyo hatuna mawasiliano mazuri kwa mda sasa.Huyu Jamaa wakati Maza alifariki tulijadiliana aende ughaibuni kwa kuchukua fedha alizoacha marehemu mama kwa ajili ya yeyey na Mimi kusaidiana,sasa amenitenga na ni Kama amenisahau na tunazaliwa wawili tu kwa baba na mama.Naskia hasira na ma chungu nkimkumbuka Jamaa na amenisababisha kuhate all diasporas will all my heart
na hilo ndio tatizo...mara nyingi watu wakishindwa maisha abroad huwa hawakubali..yaani wataendelea kudanganya km wako vizuri ila unashangaa tu hawasaidii ndugu zao huku bongo kumbe wenyewe wanaishi maisha ya kuunga unga..
huyo kaka yako hana kitu..msamehe tu..
Nimekubari, hiii poa!"Kaka akikutenga chukua jembe ukalime na siku akikukumbuka chukua kapu ukavune!
Usilaumu kabla hujajua huko alipo hali ikoje.., sio kila anayekwenda nje anafanikiwa huko maisha nayo ni magumu, pia sometimes lawama zetu na over-expectations ndizo zinazompelekea mtu kukata mawasiliano sababu kila mkiwasiliana au akirudi ni lawama mwanzo mwisho
Msome dogo hapo,braza kakacha na fungu lake la urithi masiku yanasonga bro anajidai hata simu tu hana muda wa kutwanga!!!
Tuko pamoja asilimia 100% tatizo langu ni source ya income aliyotumia kuondoka bongo na pia it's not just ndugu he is my only brother hakuna mwingine.Kuhusu kufight I have been there na bado naendelea with or without him.Tatizo no connections no communication no nothing suppose he dies Kama LUKINDO what will happen will I get to know and How?! au ndo ntaletewa MAITI home au ikiwa mbaya zaidi nsiimuone tena maishani
Ps:We went to school tog and grew up in the same hood and used to be around much for us as a family,where is that all gone,naongea kwa uchungu,hii siyo hekaya msiniquote wrong
Kuna ujinga fulani wa utegemezi unaenea sana.
Hakuna namna nzuri ya kuweza kuendelea kama ile ya kutengwa na ndugu zako.
Kutengwa na ndugu ni bahati ya mtende ambayo wajaaliwa wachache tu dunia hii wanaweza kuipata.
Namuonea donge mleta mada kwa kupata bahati hii iliyoje ya kutengwa na ndugu, wengine hatujaipata vilivyo bahati hii.
Sasa ni muda wake wa ku prove kwamba anaweza kufanya mambo bila ya msaada wa ndugu.
Mimi moja ya sababu iliyonifanya niondoke Tanzania ni kukataa habari ya kuendesha baskeli yenye "training wheels" za kuwa karibu na macho ya ndugu yanayoweza kumfanya mtu abweteke, nimejikita huku mbaaaali na ndugu, ni mwendo wa discipline tu, one mistake ten goals. Having said that, nina keep in touch na nyumbani na kusaidia kadiri ninavyoweza. Why not? Kipato cha wiki mbili kinamlipia mtu mwaka mzima wa chuo.
Tukirudi kwa huyu mtoa mada, anatakiwa agangamale aitoe halafu ajue kwamba anaweza bila msaada wa ndugu.
Waswahili walisema "Mtegemea cha ndugu, hufa masikini"
Na pia "Mtaka nyingi nasaba, hupata mwingi msiba".
Kujitegemea ndio mpango mzima.
mkuu bado mpaka karne hii unapigia mahesabu vya urithi we msamehe tafta vyako pambana usiwe kama wale watoto wa chama flani wanaombea washua wao wafe wapewe kiti