Kaka wa boyfriend wangu ananitaka

Kaka wa boyfriend wangu ananitaka

belie

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2014
Posts
387
Reaction score
261
Nilikua na boyfriend wangu tukaachana akaja kuoa, sasa alikua na mdogo wake, akawa anamtaka rafiki yangu akanambia nimuunganishie ndipo tukapeana namba za simu na kweli akafanikiwa kumpata sababu na yule rafiki yangu alikua kicheche wakashndwana na kuachana.


Sasa karudi kwangu ananitaka mie, eti ananambia nilishndwa kukutongoza kipindi kile sababu ulikua na kaka yangu, na anasema ananipenda kiukweli na anataka kuja kwetu kutoa mahari ili anioe kama nikikubali?

Sasa huyu mzima kweli? japo yule kaka ake wamechangia baba tu.

Hivi hata nikimkubali nitaonekana mjinga mimi au yeye? mana kiukweli mimi mwenyewe ananivutia na nilimpenda kimoyo moyo toka mwanzo tulivyoonana nikatamani nigeanza kuonana nae yeye kwanza, na ana kila sifa ninayoitaka kwa mwanaume.

Embu mnishauri mwenzenu.... nifanyeje
 
Mimi naona mmefanana akili,, olewa tu bidada, angalia tu neno mahari lisiwe gia ya kuingia, halafu uachwe unasoma namba za gari
^^
 
Wewe binti hujielewi....samahani kwa hlo kama nimekukwaza.Huyu mwanaume amewaona ww na rafiki yako hamnazo na anapanga kukuvuruga.Una shida sana ya ndoa???

Halafu binti anayejitambua ningumu sana kufanya habar za kuunganishiana mabwana likewise kwa mwanaume anayejielewa ni ngumu kukubali kukuwadiwa mwanamke.
 
Jiulize kwa nini alitembea na rafiki yako, na kwa nini na wewe ulimtamani na kuomba ukutane nae kabla haujakutana na kaka yake, kwa nini ulitembea na kaka yake na kwa nini kaka yake hajakuoa wewe! Kama unajitambua upata jibu.
 
fanya kile moyo wako unapenda usipende kuangalia ya watu.
 
Back
Top Bottom