Kainerugaba Msemakweli anatumiwa - Saed Kubenea

nyabhingi

JF-Expert Member
Oct 12, 2010
15,515
20,005
Katika makala yake kwenye gazeti la mwanahalisi la septemba 7,2011, Kubenea anasema msema kweli anatumiwa pale anaposema CCM hawakuiba fedha za EPA kwa ajili ya uchaguzi wa 2005 wakati ushahidi upo wazi kuwa fedha zilichotwa kuanzia septemba 2005 kwa maelekezo maalum ya rais mkapa.

Anasema wanaomtumia Msemakweli ni wapambanaji hewa wa ufisadi..

 
ngoja tuendelee kusubiri data! lakini ushahidi wa msemakweli haujaonyesha popote kuwa fedha za kagoda zilitumiwa na CCM, pesa za EPA zimechotwa kwa staili nyingi, inawezekana hizo zilizosaidia CCM ndo hazikupitia kagoda.
 
Bwana wee,,,,,,,,jamani miluzi mingi ilimpoteza mbwa,,,,kubenea nawe endelea kuutoa ushahidi zaid
 
hivi kuna watu wana hati miliki ya nchi hii?
yaani kuna watu hawataki mtu atoe neno lazima watamvamia
kama kubena ana info za kulikoa ili taifa au kumpinga msemakweli kwa data na sio kwa KEEYBOARD na maneno
mengi ya kuungaunga
 
Kila post mawazo ni 'anatumiwa' tu! Upupu mwingine wa wachangiaji. Kwani na ninyi mnatumiwa? Nini? Kutoka wapi? Mnapokeaje hizo sijui zawadi mnazotumiwa? Mliomba ndo mkatumiwa?
Sijui ni nini kutumiwa? Msamiati huu kiinglish chake ni kipi? Kama kutumiwa ni vibaya acheni nanyi kutumiwa kabla hamjasema Kubenea na Msemakweli wanatumiwa.
 

Jamani mbona mnatuchanganya watanzania......Kwanini wapambanaji mnaanza kuumana wenyewe kwa wenyewe tena.......
 
Kosa la WanaCCM lilikikua ni kuwakubali watu waliojitanabaisha kuwa wana mbinu na mikakati ya kutengenezea pesa kwa ajili ya CCM.Kwa hiyo CCM kama Chama has nothing to do with that dirty game of some few CCM leaders.Hakika tufike sehemu kitanzi hiki ni lazima kiwaangukie watu na sio Taasisi [Institution]

Na Watanzania wengi sana kwa sasa hili swala la EPA wanakubali kupumbuzwa na MAFISADI kulifanya kuwa ni kitaasisi kumbe ni wezi wachache tu ambao kama mchakato ukikaa vyema basi wahusika wafikishwe mahakamani.

Tatizo Watanzania tunajenga utamaduni wa kulewa na kukumbatia kuwa tunatoa lawama za kitaasisi baada ya kuwa tuna lawama za watu binafsi kama watu binafsi.Ndio maana wenzetu walioendelea wao lawama uenda kwa mtu binafsi kama yeye hata kama ilikuwa ni kwa dhamana ya taasisi aliyopewa.

Kuna kiongozi wa kitaifa wa zama hizo alipopewa taarifa ya pesa ilivyokwapuliwa wakati wa EPA,alishika kichwa na kupiga ukete.Lakini walioinjinia mkakati ule ifike sehemu watajwe kwani walipokuwa wanatoa vimemo kwa wahindi na waarabu huyu asikilizwe walitegemea nini?

Wazee ambao wamechafuliwa kwa kashfa hizo za EPA wajitokeza kujisafisha Watanzania kwa kuwa ukweli ukidhihiri uongo ujitenga na nafsi zenu zitakuwa huru na uenda mkapata piece of mind,mkatumia muda huu uliosalia kulea wajukuu zenu kwa amani.
 
Ingekuwa vizuri kama Kubenea angesema Msemakweli anatumiwa na nani. Naye alete ushahidi wa jinsi fedha hizo zilivyotumika ili tusome na tucheje hizo data kuliko kusema tu mtu anatumiwa. Siasa za bongo zinakuwa hazina tija hata siku hizi. tunataka ushahidi tu.
 
Some other people bana hata siwaelewi..... Isue ni kwamba hela ziliibwa full stop. kwamba zilienda wapi is not an issue coz now tunatakiwa kuwashughulikia wezi.
 
Kubenea kadai, msemakweli ama hajui asemalo au anatumiwa. Acha kuchakachua habari
 
Kubenea hajamuelewa Msemakweli! Msemakweli anasema hela ya Kagoda haikutumia kwenye kampeni na CCM! hakusema hela ya EPA! Kuna kampuni ya Deep green ambayo haijulikani ukweli wake labda na sio Kagoda kama alivyosema msemakweli! Mimi nampongeza Msemakweli amekuja na Ushahidi kama kuna mtu mwingine nae ana ushahidi wa kagoda auweke hadhalani ili tujue ukweli ni upi na uongo ni upi? Dr slaa alisema anaushahidi wa kagoda ebu nae auweke wazi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…