Kainerugaba Msemakweli anatumiwa - Saed Kubenea

Naamini anatumiwa. Mkapa alimwambia rais wa zamani wa Botswana kwamba aliidhinisha fedha za EPA kwa uchaguzi wa Kikwete. Na waziri mkuu wa Kikwete alimwambia gavana wa zamani wa benki kuu kuwa bila msaada huo ngoma ya uchaguzi ingekuwa nzito. Sasa huyu anataka kutuonyesha kuwa CCM haikufadika na fedha hizo. Naamin anatumiwa.
 
Tukijiuliza WHY NOW? and WHY THIS WAY! Tutawajua kirahisi wanaotumiwa na Magamba.
 
Nyie naona hamjui kazi ya dalali...! hapa kagoda kama dalali amekata fedha chache kwa CCM then kilichobaki kikawa chake.
 
Nataka kujua huyo Msemakweli ameshindwa nini kufungua kesi? Na anataka kutuambia nini watanzania kwa kwenda kuwatuhumu watu hadharani wakati vyombo vya sheria vipo, hata kama ushahidi upo kwanini asingeanzia mahakani badala ya kuanzisha vita vya maneno? Nataka kujua ajenda yake ni ipi? Nasikitishwa sana vyombo vya habari vinavyoendelea kukumbatia ushabiki badala ya kufuata misingi ya uandishi
 
Masikini msemakweli ashageukwa baada ya ujio wa Thread hiyo hapo. kabla ya hapo watu walimuunga mkono nikiwamo mimi, ila sasa jamaa anaonekana mamluki mbele ya wanajamvi na jamii kwa ujumla. LAKINI kubla la kujiuliza mkuu aliye pindua pepo zivumaza kutoka kwa msemakwela kuelekea kwa kagoda (S.kubenea) Je? amechukua hatua gani baada ya kujua kuwa kagoda ni ccm yenyewe. kama
hakuna bado msemakweli ataaminika kwa hatua alochukua.
Mawazo yangu tu!
 
Kubenea said:

Andishi lake linaeleza kuwa Rostan Aziz, Peter Noni na Bered Malegesi walimthibitishia kuwa Rostam alikuwa kwenye kikao ambako rais mstaafu Benjamin Mkapa alitoa maelekezo kwa Gavana wa BoT, Dk. Daudi Ballali kutoa fedha hizo kwa Rostam kwa ajili ya uchaguzi.

Sanze anasema, "Niliitwa na Bw. Malegesi ofisini kwa Bw. Rostam Aziz…Nilipofika…niliwakuta Bw. Rostam Aziz, Peter Noni (Mkurugenzi Mtendaji wa sasa wa benki ya raslimali) na Bw. Malegesi; wakaniambia fedha hizo zinahitajika kwa ajili ya kugharamia uchaguzi wa CCM na rais wake."

Hili ni andishi ambalo mpaka sasa halijakanwa na serikali, Mkapa, Rostam, Sanze, Meregesi wala Peter Noni.

Sanze anakiri alichoambiwa na si kuwa anakiri alichoambiwa ni ukweli mtupu. Hapa inaonesha yeyote anaweza kuwa hasemi kweli au haujui ukweli. Sasa kwa nini tuchague ya Sanze kuwa yana ukweli na ya Msemakweli hayana ukweli.

Serikali kutoyakanusha maelezo ya Sanze kunaonesha kuwa inapata unafuu fulani na maelezo hayo kuliko labda ukweli wenyewe ungepatikana. Serikali ni wepesi wa kukanusha yanayowagusa na kuwaaumiza sana kuliko yale yasiyowagusa. Rejea suti za mwarabu na Kikwete.

Hata kama Msemakweli anatumiwa bado ana kitu cha kusema kwani anayemtumia anaonekana kuijua fika KAGODA na anataka watanzania waamke usingizini. Usingizi ambao wanaota ndoto za kuwa watu wawili au watatu ndio wametufikisha hapa tulipo wakati ukweli ni kundi la watu lukuki. Msemakweli anaelekea kwenye kumgusa mmoja mmoja badala ya kusema ti eti ni CCM. Hapana si CCM. Hapana si uchaguzi bali ni mambo mabaya zaidi ya kuhonga katika uchaguzi yaliyofanywa na watu tunaowaamini sana. Msibeze Msemakweli, mpeni moyo aendelee kuyamwaga kwani zikiwa pumba si tutazitupilia mbali? Hakuna haja ya kumbeza sasa
 
Masikini msemakweli ashageukwa baada ya ujio wa Thread hiyo hapo. kabla ya hapo watu walimuunga mkono nikiwamo mimi, ila sasa jamaa anaonekana mamluki mbele ya wanajamvi na jamii kwa ujumla. LAKINI kubla la kujiuliza mkuu aliye pindua pepo zivumaza kutoka kwa msemakwela kuelekea kwa kagoda (S.kubenea) Je? amechukua hatua gani baada ya kujua kuwa kagoda ni ccm yenyewe. kama
hakuna bado msemakweli ataaminika kwa hatua alochukua.
Mawazo yangu tu!


Mimi binafsi sijauona utata unaoweza kutafsiriwa kwamba Msemakweli anatumiwa na mtu yeyote yule. Tatizo lililopo hapa ni watu kutaka kile wanachokiamini kiendelee kuwa ndiyo ukweli hata kama kuna upotoshaji katika kile wanachokiamini. Suala lililopo hapa ni kulazimisha kwamba fedha za Kagoda zilitumika katika uchaguzi uliomuweka Kikwete madarakani. Ulazimishaji huu umekatwa mbawa na taarifa za Msemakweli na kwa bahati mbaya, wale wanaoshikilia msimamo huu (pengine kwa kutojua) wanabeba ajenda za mafisadi waliohusika na wizi huo, ambao wamekuwa wakishikilia kwamba fedha hizo zilitumika kwa uchaguzi ili kukwepa mkono wa sheria dhidi yao.

Kile kinachoitwa andishi la Sanze ni maelezo aliyopatiwa Sanze na hao waliokuwa wakipanga wizi huo, lakini si lazima maelezo hayo yawe na usahihi, hasa katika mazingira ambayo sasa kuna ushahidi wa dhahiri kwamba fedha hizo, zilizoibiwa kwa kisingizio cha uchaguzi, zilihamishwa na kutumika visivyo. Kwa hiyo kukaa kimya kwa waliotajwa hakudhoofishi hoja ya Msemakweli kuhusiana na matumizi ya fedha hizo.

Watu wamekuwa kila mara wanajificha kwenye hoja dhaifu ya kutumiwa kama utetezi wa tuhuma zinazowakabili. Lakini mimi sijali mtu kutumiwa kwa kusema kitu chenye ushahidi na kitu hicho kuwa ni chenye hatari kwa maslahi ya nchi au umma. Kama Msemakweli anatumiwa katika hili, basi anatumiwa kwa kitu chenye heri na kwa hiyo wanaomtumia na yeye mwenyewe Msemakweli ni watu wa kupongezwa. Mimi kwa maoni yangu kuna ukweli katika mafichuzi ya Msemakweli na ndiyo maana sasa watu, wakiwemo watuhumiwa, wako bize kumshambulia Msemakweli badala ya kushambulia kile alichokizungumza.

Tuwe waangalifu na hoja zenye nia ya kuchochea malumbano yatakayochelewesha kuchukuliwa kwa hatua za kisheria eti tu kwa sababu hatua hizo zinaelekea kuwa-prove wrong watu wenye hoja binafsi.
 
Masikini msemakweli ashageukwa baada ya ujio wa Thread hiyo hapo. kabla ya hapo watu walimuunga mkono nikiwamo mimi, ila sasa jamaa anaonekana mamluki mbele ya wanajamvi na jamii kwa ujumla. LAKINI kubla la kujiuliza mkuu aliye pindua pepo zivumaza kutoka kwa msemakwela kuelekea kwa kagoda (S.kubenea) Je? amechukua hatua gani baada ya kujua kuwa kagoda ni ccm yenyewe. kama
hakuna bado msemakweli ataaminika kwa hatua alochukua.
Mawazo yangu tu!

Ndugu ishu si kugeukwa, ishu huyo anayemgeuka anafanya hivyo kwa hoja zipi. Uzuri ni kwamba kila kitu kiko wazi hivyo yatupasa sisi wenyewe kufikiri na kupambanua mambo na si kumsubiri mtu mmoja afikiri kwa niaba yetu awe Kubenea na hata nani mwingine. Uvivu wa kufikiri na kukubali tunachoambiwa ndio kumetupeleka hapa tulipo. Mtu asilazimishe hoja wala asilazimishe ushahidi gani utumike ili kufikia ukweli.

Mafisadi na majangili ni watu mahili sana katika kutengeneza ushahidi hasa wanapojua wanadili wa watu kama watanzania ambao hawataki kufikiri vitu vigumu, watawapikia majibu yao rahisi kwa vile tayari wameshasoma mwelekeo wao, wanawapa kile walichodhani kuwa sahihi. Usiyumbishwe na wingi wa watu wanaounga mkono au kupinga, suala ni uzito wa hoja.

Hebu tujiulize kwa nini kutumika kwa Msemakweli kuwe habari? Kama yeye anatumika si ujinga wake mwenyewe? Hivi hakukuwa na jambo lingine la maana zaidi ya kuwaandikia watanzania zaidi ya kumzodoa Msemakweli? Kuna kitu hapa, lazima kuna kitu. Msemakweli hata kama anatumiwa kama wengine pia tunavyotumiwa ana haki ya kusema anayoyajua na kuwaambia nao pia wayajuwe.

Mbona tunaotumiwa tupo wengi tu lakini hatuandikwi? Wapo tuliowekwa na KAGODA madarakani ili tutumiwe, tupo tuliopewa uwaziri ili tutumiwe na tunatumika, tupo tuliopewa ubunge tutumiwe na tunatumika na tupo waandishi wa habari tuliopewa vijizawadi kutunika na tunatumika kwelikweli.

Angalau sasa Msemakweli anatumika kwa kile kitakachowafaa watanzania walio wengi kuliko sisi tunaotumika kwa kuzifaa familia zetu, maboy friend na magirl friend zetu. Pamoja na yote Msemakweli ana jambo la lutuambia
 
Mimi binafsi sijauona utata unaoweza kutafsiriwa kwamba Msemakweli anatumiwa na mtu yeyote yule. Tatizo lililopo hapa ni watu kutaka kile wanachokiamini kiendelee kuwa ndiyo ukweli hata kama kuna upotoshaji katika kile wanachokiamini. Suala lililopo hapa ni kulazimisha kwamba fedha za Kagoda zilitumika katika uchaguzi uliomuweka Kikwete madarakani. Ulazimishaji huu umekatwa mbawa na taarifa za Msemakweli na kwa bahati mbaya, wale wanaoshikilia msimamo huu (pengine kwa kutojua) wanabeba ajenda za mafisadi waliohusika na wizi huo, ambao wamekuwa wakishikilia kwamba fedha hizo zilitumika kwa uchaguzi ili kukwepa mkono wa sheria dhidi yao.

Kile kinachoitwa andishi la Sanze ni maelezo aliyopatiwa Sanze na hao waliokuwa wakipanga wizi huo, lakini si lazima maelezo hayo yawe na usahihi, hasa katika mazingira ambayo sasa kuna ushahidi wa dhahiri kwamba fedha hizo, zilizoibiwa kwa kisingizio cha uchaguzi, zilihamishwa na kutumika visivyo. Kwa hiyo kukaa kimya kwa waliotajwa hakudhoofishi hoja ya Msemakweli kuhusiana na matumizi ya fedha hizo.

Watu wamekuwa kila mara wanajificha kwenye hoja dhaifu ya kutumiwa kama utetezi wa tuhuma zinazowakabili. Lakini mimi sijali mtu kutumiwa kwa kusema kitu chenye ushahidi na kitu hicho kuwa ni chenye hatari kwa maslahi ya nchi au umma. Kama Msemakweli anatumiwa katika hili, basi anatumiwa kwa kitu chenye heri na kwa hiyo wanaomtumia na yeye mwenyewe Msemakweli ni watu wa kupongezwa. Mimi kwa maoni yangu kuna ukweli katika mafichuzi ya Msemakweli na ndiyo maana sasa watu, wakiwemo watuhumiwa, wako bize kumshambulia Msemakweli badala ya kushambulia kile alichokizungumza.

Tuwe waangalifu na hoja zenye nia ya kuchochea malumbano yatakayochelewesha kuchukuliwa kwa hatua za kisheria eti tu kwa sababu hatua hizo zinaelekea kuwa-prove wrong watu wenye hoja binafsi.

Watanzania ni wepesi sana kupotoshwa. Kwanza tuangalie alichosema Msemakweli, na tuangalie nyaraka alizowasilisha na anayekuja na hoja mpya, awasilishe nyaraka. Naamini mwandishi wa makala hii (Kubenea) anazo nyaraka kuonyesha CCM walitumia fedha za EPA na si yeye tu wako wengi wenye maelezo kama hayo.

Ni vyema kuyaanika lakini si kusema Msemakweli kakosea. yeye kasema ushahidi alionao ndio huo. Mwingine aje sema na mimi ushahidi ni huu, ili wahusika wawafuate kina Maranda gerezani na si kuendelea kutuchezea akili.
 
Tamthilia nzuri hii, wacha nitafute pop corn nikae nifaidi miye.... Mambo ya series hayo.

Tatizo chenga nyingi,halafu screen ya B&W....unaweza kudhani steringi kavaa shati black kumbe red! "Tamthilia" za bongo nuksi aisee!!
 
hapa nadhani kuna mchezo unachezw inawezekana anatumiwa kudhoofisha ufuatiliaji
 
Back
Top Bottom