Kazi inaendelea kurekebisha baadhi ya miundombinu mataifa zaidi ya Saba yameanza kuja kununua mazao ndani ya soko la mazao ambalo now limekuwa la kimataifa makambako tcπππππZaidi ya Wafanyabiashara 1,000
wa soko la mazao la kimataifa linalouza mazao katika nchi 7 za Africa Mashariki na Kati lililopo Lyamkeni halmashauri ya mji wa Makambako wilayani Njombe wameomba serikali kujenga kituo kidogo cha polisi,Huduma ya mawasiliano ya simu pamoja Kuleta huduma za kifedha katika kituo hicho ili kulinda usalama wa fedha za wafanyabiashara na wateja kwasababu wako hatarini kupokwa fedha na majambazi kutokana na kutembea umbali mrefu kufata huduma za kibenki.
Wamesema usalama wao upo pabaya kwasababu kuna biashara kubwa zinafanyika katika soko hilo zikihusisha mabilioni ya fedha na wateja kutoka nchi za Rwanda,Malawi Burundi Uganda Congo Zambia na Msumbiji