Kagera: Basi la Kampuni ya Arusha Express lawaka moto na kuteketea maeneo ya Kibeta

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Basi la abiria linalomilikiwa na Kampuni ya Arusha Express lenye namba za usajili T 222 ABF, aina ya Scania Marcopolo, ambalo linafanya safari zake kati ya Bukoba kuelekea Arusha, limepata ajali ya kuwaka moto na kuteketea kabisa.

Ajali hiyo imetokea leo majira ya asubuhi eneo la Kibeta maarufu kwa Kagambo katika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.

Taarifa zinasema kuwa abiria wote waliokuwemo kwenye basi hilo wamefanikiwa kutoka salama bila madhara, hata hivyo chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika mara moja!
IMG_20190521_114446_651.jpeg
IMG_20190521_114501_592.jpeg
IMG_20190521_114544_798.jpeg
 
Leo tutapumzika kusemwa sisi wenye mabasi ya Kichina Yutong, Zhongtong Climber, Golden Dragon, Higer, ya kwamba kuna matatizo kwenye mfumo wa umeme..!

Asante Mungu kwa kunusuru waja wako..Poleni sana abiria..!
 
Ni wakati umefika sasa kwa wamiliki wa mabasi wawe wanatoa Insurance kwa abiria wao , ikitokea adha kama hizi kuwe na compensation , hii itawafanya wamiliki kukagua na kumiliki mabasi yaliyo salama
 
Ni wakati umefika sasa kwa wamiliki wa mabasi wawe wanatoa Insurance kwa abiria wao , ikitokea adha kama hizi kuwe na compensation , hii itawafanya wamiliki kukagua na kumiliki mabasi yaliyo salama
Exactly mkuu..Wamiliki wataongeza umakini katika service kuliko kuangalia kipato, uhai ni muhimu
 
Back
Top Bottom