Kagame kuongezewa Muhula Mwingine na Wanyarwanda!

Kagame kuongezewa Muhula Mwingine na Wanyarwanda!

Huku Kagame, kule Nkuruzinza! hawa watusi na wahutu taabu kweli kweli, wanatuvurugia EAC.

* Ifike mahala viongozi wa Afrika waache kung'ang'ania madaraka wanashindwa kujifunza kwa Madiba

* Yeye alikuwa anapaza sauti kuwa Nkurunzinza atoke kumbe na yeye ni walewale

* Hamna demokrasia Rwanda, kuna umuhimu wa kuheshimu ukomo wa madaraka na sio Rais kutumia kigezo cha kupendwa na watu kutawala miongo kwa miongo.
 
... Nashukuru Kwa Kuchangia Hoja. Vipi Lakin Hoja Umeielewa, Au Unaotafuta Tu Makosa, Kiswahili Sikuzaliwa Nacho Mkuu Nimekulia Kijijini

Sema ukweli we we umezaliwa kijiji gani? Anyway next week naenda RUBEHO unakazawadi nikupitishie nyumbani?
 
Kwa mchapa kazi kama Kagame acha atawale hata milele,ili mradi wananchi wana neemeeka.Uliza wa libya wanajuta kumuua Gadaffi kwa demokrasia waliyodanganywa na wamarekani

Nafikiri hii ni point. Pamoja na kwamba sisi tuna demokrasia kuliko Rwanda badi hatuneemeki na rasilimali zetu kama wanyarwanda. Kila raisi wetu akikaribia kutoka madarakani tumekuwa tunashuhudia ufisadi wa hali juu kwa wale wapambe wa raisi anayemaliza nuda wake kutokuwa na uhakika wa nafasi zao. Kwa kagame naona ni sawa kwsababu yeye ana uchungu na nchi yake kutoka rohoni. Hasiti kumchukulia mtu hatua endapo anakuwa fisadi bila kujali ukaribu wake naye.
 
Dictator wengi Afrika walifanya ufedhuli kwa maslahi yao na familia zao.
Kama kwa maendeleo na utangamano waliyonao wanyarwanda hivi sasa ni ZAO la udiktea basi ZAO JIPYA LA VIONCOZI WA AFRIKA WAWE MAKAGAME WEEEEENGI!!!
My goash.
 
Term tatu za Rwanda za miaka saba saba itakuwa miaka 21, ambao ni sawa na term 7 za Australia za miaka mitatu mitatu, zaidi ya term tano za Marekani za miaka minne minne, na zaidi ya term nne za nyingi za commonewealth za miaka mitano mitano. Hata hivyo hayo ni maamuzi yao wenyewe wanyarwanda; waache wajiamulie mambo yao wenyewe.
 
neno muhimu sana "wajiamulie" wenyewe.
i wish if life provides this always.
 
Hata sisi tumwongezee tuu braza mhula mwingine akamilishe ambayo hajafanya kuna ahadi nyingi hajatekeleza
 
Hata sisi tumwongezee tuu braza mhula mwingine akamilishe ambayo hajafanya kuna ahadi nyingi hajatekeleza

Tuonee huruma wenzio..katiba iheshimiwe miaka 10 ya manung'uniko imeisha,muache DR akapumzike Msoga
 
Siasa za Afrika zina matatizo maana hao wanyarwanda wamejikita kwa mtu binafsi na sio kutengeneza taasisi haiwezekani useme rwanda nzima hakuna atakaefanya vizuri zaidi ya huyo kagame, mkapa alitawala vizuri Tanzania, alistabilize uchumi, lakini alipotoka madudu mengi ya aliyofanya yalijulikana nahisi na huyo kagame itakua hivyo hivyo swali la kujiuliza mfano jamaa akafariki ghafla huo uraisi atapewa mke wake au watoto wake?
 
Hata sisi tumwongezee tuu braza mhula mwingine akamilishe ambayo hajafanya kuna ahadi nyingi hajatekeleza
Huyu msafiri hatumtaki,ila tungekua na rais kama Kagame tungetaka atawale milele.Rwanda wakuu wamepiga hatua kila kitu,kila raia anamuheshimu mwenzake,sera zao zinatekelezeka
 
Kwa siasa za nchi zenu za maziwa makuu hatushangai.hapo ni mpaka afe eau atokee mwanajeshi mwingine aweze kumpindua.mtajuwa wenyewe.sisi tunajiandaa Na uchaguzi.
 
Kama kwwli wanampenda basi waondoe term limit kwenye katiba ili atawale maisha kabisa mpaka atakapofia Ikulu ndo aingie mwingine!
 
Kama kwwli wanampenda basi waondoe term limit kwenye katiba ili atawale maisha kabisa mpaka atakapofia Ikulu ndo aingie mwingine!

katiba afrika hazieshimiki.Kuvunja katiba ni jambo baya sana kila mtu atataka kugangania madaraka.Nkurunziza,mseveni leo kagame kesho?
 
..sasa imekuwa ni 3 terms?

..na kama ni 3 terms, wanaanza kuhesabu toka ile ya kwanza, au huo uchaguzi unaofuatia ndiyo 1st term?

..au hakuna term limits kabisa?

NB:

..as long as Rwanda is stable I am fine with it.

..jambo la msingi ni mahusiano mazuri ya kiuchumi na kijamii baina ya mataifa yetu.



cc mchambawima1

Kesha kula two terms za miaka saba saba.Kabla ya hapo akikuwepo tayari. Two terms zake ni almost tatu za Bongo.
Watu wenye uwezo wapo lakini naona anafuata ya Museveni.
 
Last edited by a moderator:
Wangapi wanatamani baba riz aendelee?
 
Back
Top Bottom