Mpui Lyazumbi
JF-Expert Member
- Sep 1, 2010
- 1,856
- 371
Wakuu heshima kwenu, kulingana na habari zilivyo ni dhahiri kwamba Mbunge Kafulila kavuliwa uanachama wake. Jambo hili limenisukuma kuyapitia makabrasha kadhaa kuona kama kwa kuvuliwa uanachama ndugu kafulila ataukosa ubunge automatically. Kuna utata nimeupata sambamba na ule wa mbunge wa Arumeru mashariki bwana Sumari ni mbunge ama la. Imani yangu naiweka hapa jamvini kwa ufafanuzi iwapo huu sasa ndo ukomo wa kafulila kuwa mbunge. Nimepitia katiba yetu haisemi kwa uwazi juu ya ukomo wa mbunge kama ilivyo kwa nafasi nyingine kama vile rais, makamu wa rais, waziri mkuu n.k. Swali langu linabaki palepale -Kafulila ataendelea na ubunge licha ya kuvuliwa uanachama?