Kuna upotoshaji mkubwa sana, tena wa makusudi, tangu Lowassa alipojiunga na CHADEMA. na ukiangalia POVU lililowadondoka CCM na makuwadi wake baada ya Lazaro Nyalandu kujitoa CCM, pamoja na hatua za kukurupuka kumtimua uanachama kinyume na taratibu ili kuzima pigo alilorusha kwa chama chake cha zamani, utaelewa kwa nini hali iko hivyo katika kujaribu kumdhibiti Lowassa akiwa nje ya CCM.
Mleta uzi ameandika vizuri sana tena kwa hoja nzito, kuhusu kazi na majukumu ya vyama vya upinzani. Awamu ya tano ya CCM imejikita katika kujaribu kupambana na UFISADI, siyo kwa kupenda, bali kwa kujibu hoja kali za vyama vya upinzani, hasa CHADEMA, kuhusu ufisadi. unaweza kushangaa huyo aliyeitwa Tumbili juzi, na wabunge wa CCM wakashangilia, leo anapongezwa. Lakini upotoshaji pia upo katika yale yanayoendelea sasa hivi. CHADEMA inapinga matumizi nje ya bajeti, ambapo JPM na maafisa wake wanaamua tu kutumia fedha bila kufuata mipango ya serikali. huo ni ufisadi mkubwa, wa kitaasisi. Kujenga uwanja mkubwa wa ndege Chato ni ufisadi mkubwa. Kubomoa jengo la TANESCO kwa kisingizio cha kujenga barabara, ni UFISADI mkubwa