nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Saturday, 21 May 2011 21:43
Balozi Ibrahim Kaduma aliyekuwa Waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere akizungumza katika mahojiano maalumu na Gazeti hili jijini Dar es Salaam jana.Picha na Fidelis Felix
Elias Msuya
BALOZI Ibrahim Kaduma, ambaye alikuwa Waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere, ametilia shaka utekelezaji wa mkakati kujivua gamba kwa madai kuwa CCM na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete hawako makini kwa sababu wanashindwa kuwachukulia hatua wanaotuhumiwa kukivuruga chama.Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu jijini Dar es Salaam jana, Kaduma ambaye ameitumikia serikali kwa muda mrefu, alisema mkakati wa CCM kujivua gamba utafanikiwa endapo Kikwete na chama chake watakuwa na dhamira ya kweli.
"Kujivua gamba kwa CCM kutawezekana kama wakiwa ‘serious' (makini). Kwa sababu, wakati wetu hakuna mtu aliyeshutumiwa akabaki kwenye Kamati Kuu ya chama," alisema Kaduma na kuongeza:"Kama rais ana msimamo huo awatoe kwenye chama wanaotuhumiwa. Kwa nini awaseme tu au anataka wajiondoe wenyewe? Anasema mawaziri wana harufu ya wizi lakini wamo kwenye baraza, kwa nini asiwatoe?"
Huku akitaja sifa za kiongozi bora, Kaduma alisisitiza kuwa kutokana na kukosekana maadili kwa sasa, taifa limepoteza mwelekeo.
"Mpaka sasa hatuko kwenye ‘right truck' (njia sahihi) kwa sababu tumeshapoteza maadili. Baadhi ya sifa za kiongozi bora ni kuwa mcha Mungu na kupambana na rushwa kama alivyokuwa Sokoine.
"Viongozi wawe na huruma ya kweli, wanyenyekevu na wawe tayari kujikosoa na kukosolewa. Je, viongozi wa sasa wana sifa hizo?" alihoji na kusisitiza: "Sioni hali hii kwa utawala wa sasa".
Akizungumzia kuanguka kwa Azimio la Arusha na kuingia kwa Azimio la Zanzibar,Balozi Kaduma alisema hali hiyo ilisababishwa na ubinafsi wa viongozi wenye tamaa ya mali."Ufisadi ni zao la ubinafsi, walioshindwa Azimio la Arusha walikuwa wabinafsi. Mtu kama huwezi kufanya kazi uondoke serikalini, kwani hatukulipi mshahara hata ukashindwa kututumikia (wananchi)?"alihoji.
Akikumbuka uongozi wa Mwalimu Nyerere, Kaduma alisema, rais huyo wa kwanza wa Tanzania, alifanya viongozi waaminike katika jamii kwa sabahu alikuwa mkali."Mwalimu alikuwa ‘strict' (mkali). Aliwahi kutoa mfano wa mke wa Cesar (Kaisari) ambaye alipewa talaka kwa kutuhumiwa tu. Mke wa Kaisari hakupaswa hata kutuhumiwa," alieleza Kaduma na kuendelea:"Wakati ule ukifanya kosa unajiondoa mwenyewe, maana ukingoja (Nyerere) atakufukuza tu.
Ndiyo maana enzi za Mwinyi wafungwa walipokufa Shinyanga, alijiuzulu. Jenerali Natepe pia alijiuzulu kwa matatizo yaliyotokea Gereza la Ukonga." Balozi Kaduma ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Taifa ya Biashara (NBC 1997), alisema viongozi wa sasa wamejaa ubinafsi ndiyo maana ni mafisadi.
"Moja kati ya ahadi za mwanachama wa Tanu ni 'binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja' maneno tisa tu," alisema na kuendelea:"Biblia katika Zaburi 133 inasema ‘Tazama jinsi ilivyo vema ndugu wakikaa pamoja kwa umoja'. Kiongozi akishayajua haya hutakuwa mbinafsi."
Aliendelea, "Kiongozi ni mtumishi siyo mtawala, kila analofanya linufaishe jamii. Anapaswa kujitoa kwa ajili ya watu. Ufisadi ni zao la ubinafsi. Tuzitafakari ahadi 10 za mwana Tanu."Kuhusu kulegalega kwa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, ameshauri kuwapo kwa serikali moja akisema kuwa hilo ndilo lilikuwa kosa la Mwalimu Nyerere.
Hata hivyo aliwatahadharisha wananchi wanaotaka muungano uvunjwe akisema kuwa watatafakari kwanza hasara zake kabla ya kuchukua maamuzi."Kosa kubwa la Mwalimu Nyerere lilikuwa ni kukataa kuunda serikali moja akiogopa kuimeza Zanzibar. Karume alikuwa tayari kabisa. Nadhani hiyo ingemaliza matatizo yote".
Alisema muungano unaharibiwa na tamaa za viongozi ambao nao hutaka kuwa na madaraka bila ya kujali maslahi ya wananchi.
Kaduma alipinga wazo la baadhi ya watu kutaka kuwe na serikali tatu akisema kuwa hili litaongeza mzigo wa gharama za uendeshaji.
"Ni gharama kubwa, leo kuna wilaya mpya zimeanzishwa, umeona kuna ma DC? Lengo la kuunganisha Tanu na ASP lilikuwa kuunda serikali moja, lakini utashangaa kusikia Wazanzibari wanang'ang'ania serikali yao, sikatai, lakini watafakari" alisema. Kwa mujibu wa Kaduma kama viongozi wa sasa wangemsikiliza Mwalimu Nyerere, nchi isingefikia hapa ilipo.
Alisema licha ya kwamba wakati Nyerere anastaafu mwaka 1985, nchi ilikuwa na hali mbaya kiuchumi, alifanikiwa kuijenga katika maadili."Kama Nyerere angesikilizwa, maadili yake ndiyo yangekuwa uhuru wa Afrika yote. Ili nchi ikue inahitaji mambo matatu; uhuru wa bendera, uhuru wa kichwa (mind), uhuru wa kiuchumi. Hili ndilo lengo la Azimio la Arusha.
"Nyerere alifanikiwa mambo mawili akabakiza suala la kukuza uchumi."Balozi Kaduma ambaye pia aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wakati wa Mwalimu Nyerere, alisikitishwa na Umoja wa Afrika kwa kushindwa kumkemea kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi, kwa kuua raia wake.
Balozi Ibrahim Kaduma aliyekuwa Waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere akizungumza katika mahojiano maalumu na Gazeti hili jijini Dar es Salaam jana.Picha na Fidelis Felix
Elias Msuya
BALOZI Ibrahim Kaduma, ambaye alikuwa Waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere, ametilia shaka utekelezaji wa mkakati kujivua gamba kwa madai kuwa CCM na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete hawako makini kwa sababu wanashindwa kuwachukulia hatua wanaotuhumiwa kukivuruga chama.Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu jijini Dar es Salaam jana, Kaduma ambaye ameitumikia serikali kwa muda mrefu, alisema mkakati wa CCM kujivua gamba utafanikiwa endapo Kikwete na chama chake watakuwa na dhamira ya kweli.
"Kujivua gamba kwa CCM kutawezekana kama wakiwa ‘serious' (makini). Kwa sababu, wakati wetu hakuna mtu aliyeshutumiwa akabaki kwenye Kamati Kuu ya chama," alisema Kaduma na kuongeza:"Kama rais ana msimamo huo awatoe kwenye chama wanaotuhumiwa. Kwa nini awaseme tu au anataka wajiondoe wenyewe? Anasema mawaziri wana harufu ya wizi lakini wamo kwenye baraza, kwa nini asiwatoe?"
Huku akitaja sifa za kiongozi bora, Kaduma alisisitiza kuwa kutokana na kukosekana maadili kwa sasa, taifa limepoteza mwelekeo.
"Mpaka sasa hatuko kwenye ‘right truck' (njia sahihi) kwa sababu tumeshapoteza maadili. Baadhi ya sifa za kiongozi bora ni kuwa mcha Mungu na kupambana na rushwa kama alivyokuwa Sokoine.
"Viongozi wawe na huruma ya kweli, wanyenyekevu na wawe tayari kujikosoa na kukosolewa. Je, viongozi wa sasa wana sifa hizo?" alihoji na kusisitiza: "Sioni hali hii kwa utawala wa sasa".
Akizungumzia kuanguka kwa Azimio la Arusha na kuingia kwa Azimio la Zanzibar,Balozi Kaduma alisema hali hiyo ilisababishwa na ubinafsi wa viongozi wenye tamaa ya mali."Ufisadi ni zao la ubinafsi, walioshindwa Azimio la Arusha walikuwa wabinafsi. Mtu kama huwezi kufanya kazi uondoke serikalini, kwani hatukulipi mshahara hata ukashindwa kututumikia (wananchi)?"alihoji.
Akikumbuka uongozi wa Mwalimu Nyerere, Kaduma alisema, rais huyo wa kwanza wa Tanzania, alifanya viongozi waaminike katika jamii kwa sabahu alikuwa mkali."Mwalimu alikuwa ‘strict' (mkali). Aliwahi kutoa mfano wa mke wa Cesar (Kaisari) ambaye alipewa talaka kwa kutuhumiwa tu. Mke wa Kaisari hakupaswa hata kutuhumiwa," alieleza Kaduma na kuendelea:"Wakati ule ukifanya kosa unajiondoa mwenyewe, maana ukingoja (Nyerere) atakufukuza tu.
Ndiyo maana enzi za Mwinyi wafungwa walipokufa Shinyanga, alijiuzulu. Jenerali Natepe pia alijiuzulu kwa matatizo yaliyotokea Gereza la Ukonga." Balozi Kaduma ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Taifa ya Biashara (NBC 1997), alisema viongozi wa sasa wamejaa ubinafsi ndiyo maana ni mafisadi.
"Moja kati ya ahadi za mwanachama wa Tanu ni 'binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja' maneno tisa tu," alisema na kuendelea:"Biblia katika Zaburi 133 inasema ‘Tazama jinsi ilivyo vema ndugu wakikaa pamoja kwa umoja'. Kiongozi akishayajua haya hutakuwa mbinafsi."
Aliendelea, "Kiongozi ni mtumishi siyo mtawala, kila analofanya linufaishe jamii. Anapaswa kujitoa kwa ajili ya watu. Ufisadi ni zao la ubinafsi. Tuzitafakari ahadi 10 za mwana Tanu."Kuhusu kulegalega kwa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, ameshauri kuwapo kwa serikali moja akisema kuwa hilo ndilo lilikuwa kosa la Mwalimu Nyerere.
Hata hivyo aliwatahadharisha wananchi wanaotaka muungano uvunjwe akisema kuwa watatafakari kwanza hasara zake kabla ya kuchukua maamuzi."Kosa kubwa la Mwalimu Nyerere lilikuwa ni kukataa kuunda serikali moja akiogopa kuimeza Zanzibar. Karume alikuwa tayari kabisa. Nadhani hiyo ingemaliza matatizo yote".
Alisema muungano unaharibiwa na tamaa za viongozi ambao nao hutaka kuwa na madaraka bila ya kujali maslahi ya wananchi.
Kaduma alipinga wazo la baadhi ya watu kutaka kuwe na serikali tatu akisema kuwa hili litaongeza mzigo wa gharama za uendeshaji.
"Ni gharama kubwa, leo kuna wilaya mpya zimeanzishwa, umeona kuna ma DC? Lengo la kuunganisha Tanu na ASP lilikuwa kuunda serikali moja, lakini utashangaa kusikia Wazanzibari wanang'ang'ania serikali yao, sikatai, lakini watafakari" alisema. Kwa mujibu wa Kaduma kama viongozi wa sasa wangemsikiliza Mwalimu Nyerere, nchi isingefikia hapa ilipo.
Alisema licha ya kwamba wakati Nyerere anastaafu mwaka 1985, nchi ilikuwa na hali mbaya kiuchumi, alifanikiwa kuijenga katika maadili."Kama Nyerere angesikilizwa, maadili yake ndiyo yangekuwa uhuru wa Afrika yote. Ili nchi ikue inahitaji mambo matatu; uhuru wa bendera, uhuru wa kichwa (mind), uhuru wa kiuchumi. Hili ndilo lengo la Azimio la Arusha.
"Nyerere alifanikiwa mambo mawili akabakiza suala la kukuza uchumi."Balozi Kaduma ambaye pia aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wakati wa Mwalimu Nyerere, alisikitishwa na Umoja wa Afrika kwa kushindwa kumkemea kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi, kwa kuua raia wake.