Kadhia ya Makonda: Dhana ya bunge halina ‘’meno’’ inakufa kifo cha mende.

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,974
Kuna methali inayosema, Mwanga mpe mtoo alee. Methali nyingine inasema, Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.

Mpaka sasa inavyoonekana wapinzani hawajalielewa somo la siasa za CCM ndani ya bunge na nje ya bunge.

Kwa muda mrefu, wapinzani waliisumbua sana CCM kwa kutumia dhana ya ufisadi. Kila mara CCM walikuwa wakishambuliwa kuwa ni mafisadi.

Kwa kutumia dhana ya mwanga mpe mtoto alee, CCM walitengeneza mazingira yaliyowafanya wapinzani kumchukua na kumlea mtoto wa CCM ambaye alikuwa ni nembo ya dhana ya ufisadi nchini.

Siku ambayo Lowassa alihamia CHADEMA ilikuwa ni siku ambayo hoja ya ufisadi kutoka upinzani ilikufa kifo cha mende mpaka hata neno ufisadi likaondolewa kwenye makabrasha ya upinzani.

Baadaye iliibuka hoja ya ‘’bunge la sasa halina meno’’ kutoka kwa wapinzani wakafikia mpaka hatua ya kuweka karatasi kuziba midomo yao.

CCM wamehangaika na hoja hii lakini kwa kutumia dhana ya ‘’ndege mjanja hunaswa na tundu bovu’’ wameanza kuiua kwa umakini mkubwa.

Tumeona na kusoma kwenye vyombo vya habari jinsi ambavyo baadhi ya wapinzani wakishangilia kuitwa kwa Makonda anayedaiwa ni ‘’kiongozi aliyekaribu’’ na Rais Magufuli kwenye kamati ya kudumu ya Bunge inayoshughulika na Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili ‘’akasulubiwe’’ baada ya wabunge kutoa azimio la pamoja.

Kwa maana nyingine kimantiki wanatuambia Bunge lina meno kwa sababu limeweza kumuita kiongozi ambaye wapinzani wanadai ni ‘’sauti ya Rais Magufuli’’ ili wamsulubu. Kwa maana nyingine, kuisulubu ‘’sauti ya Rais Magufuli’’ ni kumsulubu Rais Magufuli.

Wapinzani bila kujua wanachofanya ni kuua dhana ya ‘’bunge la sasa halina meno’’ pale ambapo masuala ya msingi kwa taifa yatakapojiri bungeni siku sijazo.

CCM wanafahamu vizuri kuwa mashitaka ya Makonda hayana athari zozote kwake na kwa CCM badala yake yanaifanya CCM na serikali yake kuimarika zaidi katika macho ya Watanzania kuwa bunge lina meno yake. Kusema bunge halina meno ni porojo tu.

Kuna ‘’wajinga’’ wasiojua taratibu na kanuni za bunge wanashangilia wakidhani Makonda atasimama ndani ya ukumbi wa bunge na kuanza kuhojiwa na wabunge. Hawafahamu kuwa mahojiano yatafanyika ndani ya ofisi za kamati yenye wajumbe 15 ambao kati yao kuna wabunge wa CCM 9.

Kikubwa zaidi, mashitaka ya Makonda hayawezi hata kutengeneza hoja ya kikanuni kumshauri Rais Magufuli amfute kazi badala yake, Kamati ya kudumu itatoa onyo/ushauri na biashara itaishia hapo.

Kwa mtu anayeangalia masuala ya kisiasa kwa kutumia 3D thinking atatambua kuwa suala la Makonda linaenda kuimarisha zaidi CCM na serikali yake huku likiwaacha wapinzani hawana hoja mbadala katika siku zijazo.

Politics is a dirty game!
 
Hii hoja ipo kisiasa na majibu yake yatakuwa siasa

propaganda kwa maana fupi.
 
Katibu wa bunge kawaumbua wabunge wote, mawaziri na mwengekiti chenge..Inaonekana maamuzi yalikuwa na mhemko na ushabiki dhidi ya makonda..wameumbuka kweli
 
Nadhani hoja yako iko nje ya mada yangu!
Hivi wewe toka lini ukawa na "mada" in the real context ya neno lenyewe, zaidi ya propaganda tu za kisiasa za chama chako na chuki dhahiri dhidi ya vyama vingine vya siasa? Nachojua mimi uko kundi moja na the likes of Lizaboni.....mimi huwaita "wabong'oaji".
 
24 Reactions
Reply
Back
Top Bottom