Tukio zima halina sura ya utekaji.
Mtu hawezi kuteka mtoto na akaruhusu ajulikane kwa kwenda yeye mwenyewe kwenye eneo la tukio na kuteka mtoto.
Ingekuwa utekaji, angetuma watu wakamteke mtoto bila yeye kuonekana, ili akwepe jinai ya utekaji.
Ila mada nzima imelenga kwenye jina la Chadema, ndio maana mada yote imekosa uzito kabisa.
sasa na nyie mnaleta mambo personal hapa jamvini kweli yanatusaidia nini sisi.yangefaa sana kama ungepeleka kwenye Magazeti ya Shigongo kwani hapa kwa Great Thinkers sidhani kama ni mahali pake kabisa .yaani they are not related at all.
Sasa huyu mtoto katekwa au kachukuliwa na baba'ke Lol!!Hivi Watanzania tutafika kweli yaani mambo ya kijinga yanamlaza mto nje ati Kada wa Chadema kateka mtoto nani kakuambia Chadema kuna Makada,
Kumbe mama mtoto anamfahamu baba mtoto kama mme wake wa zamani na mtoto anamfahamu baba'ke sasa shida nini??
Au kwa kuwa CCM Magamba walimteka Dr Ulimboka so wanataka kuchafua hali ya hewa ati na Ritz nae kasema Chadema mnateka mpaka watoto.
Ritz uko wapi mkuu mbona kimya kwa chaguzi za Ccm Magamba leta habari za Rushwa kaka au hujazikamatia bado aaaaah kaka acha hizo au wewe ndio wale wa Edward Lowasa na ulikuwapo kazini na wewe sio poa mkuu kukaa kimya kiivyo tiririka mkuu tupe mambo ya Chaguzi
Ama kweli CHADEMA ni chama kubwa mambo ya chumbani kichwa cha habari kinajina CHADEMA. mwishowe hata mtu akishindwa kulipa karo ya mwanae shule mtasema CHADEMA washindwa kusomesha watoto.
Huo ndio uchochezi wa waandishi wengi wa habari wanashindwa kuzitune mindset zao kwenye uhalisia na kuandika vichwa vya habari vyenye lengo la kuuza gazeti. Hakuna haja ya kuleta malumbano yasiyokuwa na tija ktk uandishi wenu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.