Kada wa CHADEMA achinjwa akisherehekea ushindi

Kada wa CHADEMA achinjwa akisherehekea ushindi

Joined
Dec 11, 2010
Posts
3,321
Reaction score
6,331
Mume wa mwenyekiti wa kitongoji cha Kapela CHADEMA Kata ya Igulwa Wilaya ya Bukombe Ndugu Bundala amechinjwa jana wakati wa kusherehekea ushindi wa mke wake muda wa saa mbili usiku tarehe 15/12/2014 Ushirombo Mjini.

Bi Lucia (CHADEMA) alishinda kitongoji hicho Juzi kwa Kura 435 dhidi ya 220 za Benedict (CCM) aliyekuwa mgombea wa CCM Bw Benedict amekuwa akiongoza Kitongoji hiki kwa miaka 25 mpaka juzi alipobwagwa na Bi Lucia wa CHADEMA.

CCM anahusishwa kwa kiasi kikubwa na mauaji hayo.

Taarifa zaidi zitafuata.
 
siku mtu anaamka tumbo lina muuma atasema kaz ya CCM
 
Mume wa mwenyekiti wa kitongoji cha Kapela Chadema Kata ya Igulwa Wilaya ya Bukombe Ndugu Bundala amechinjwa jana wakati wa kusherehekea ushindi wa mke wake muda wa saa mbili usiku tarehe 15/12/2014 Ushirombo Mjini.

Bi Lucia (Chadema) alishinda kitongoji hicho Juzi kwa Kura 435 dhidi ya 220 za Benedict (Ccm) aliye kuwa mgombea wa ccm Bw Benedict amekuwa akiongoza Kitongoji hiki kwa miaka 25 mpaka juzi alipobwagwa na Bi Lucia wa Chadema.

CCM anahusishwa kwa kiasi kikubwa na mauwaji hayo.

Taarifa zaidi zitafuata..

Nyie ndo wapumbavu kweli kweli mnachinjana kwa sababu ya uenyekiti wa kijijii tuuu mbona title ndogo sana
 
Ndg Mtoi CCM wanajua muda si mrefu watakufa hivyo wanatafuta wakuwasindikiza huko ahera.
 
Mume wa mwenyekiti wa kitongoji cha Kapela Chadema Kata ya Igulwa Wilaya ya Bukombe Ndugu Bundala amechinjwa jana wakati wa kusherehekea ushindi wa mke wake muda wa saa mbili usiku tarehe 15/12/2014 Ushirombo Mjini.

Bi Lucia (Chadema) alishinda kitongoji hicho Juzi kwa Kura 435 dhidi ya 220 za Benedict (Ccm) aliye kuwa mgombea wa ccm Bw Benedict amekuwa akiongoza Kitongoji hiki kwa miaka 25 mpaka juzi alipobwagwa na Bi Lucia wa Chadema.

CCM anahusishwa kwa kiasi kikubwa na mauwaji hayo.

Taarifa zaidi zitafuata..

Mungu ailaze pema roho ya marehemu. Mtoi mimi shishangai sana kwani hali hii imechangiwa na watu kuanza kugeuza uongozi kama ajira ya kudumu na walio sio cheo ni Dhamana. Ukijaribu kuangalia wanaccm wengi wamegeuza uongozi kama ni sehemu ya kutokea kimaisha kwani wengi wao hawana kazi nyingine zaidi ya kuishi kwa rushwa, utapeli na udalali kupitia dhamana zao walizopewa na wananchi wakati mwingine unakuta hata hicho cheo hakukipata kwa njia halali bali rushwa. Nasema hivyo kwanini, unaona uongozi hata wa mtaa mtu anatoa hela nyingi ili achaguliwe, unategemea anapokosa hiyo nafasi zaidi ya kutoa uhai wa mtu nini kingine? Hali hii iko tokea uongozi wa juu kabisa na ndio maana unaona jeshi la polisi linatumika sana kukiuka sheria za nchi na haki za binadamu kwa kupiga na kuua wapinzani kisa tu viongozi wa ccm wanawapa au kuwaachia mwanya wa kula rushwa.
 
Iko siku moja hizi itikadi za kisiasa tutazifanya kuwa imani zetu, na hapo ndio tutashuhudia makubwa na ya ajabu kutoka kwa watanzania.
 
Kuna mama mmoja aligundulika juzi juzi kule manzese akiwa maemfungia mama yake mzazi ndani kwa miaka zaidi ya kumi bila kutoka nje kisa cheo cha mwenyekiti wa kitongoji.ccm ukoo wa panya kweli
 
Kuna tetesi kwamba mtu mmoja anayesadikiwa kwamba ni mme wake na mwenyekiti aliyeshinda wa mtaa wa igulwa ushirombo amechichwa kinyama na watu wasiojulikana jirani na nyumba yake,mauaji hayo yamefanyika wakati familia yake ikisherehekea ushindi wa kishindo alioupata mke wake kupitia chama cha chadema. Kama kuna mtu ana habari zaidi atujuze tafadhari
 
Wanahusishwa vipi sasa maana hakuna muunganiko wa moja kwa moja!!!????
Kiongozi unatoaje lugha nyepesi namna hii mbele ya hadhira??!!
 
Back
Top Bottom