Kaa kimya

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,305
Reaction score
829,363
Ukimya ni hazina iliyofichwa. Ukimya unaturuhusu kutazama, kufikiria, kuelewa, na kuunganishwa na hekima yetu ya ndani. Wakati mwingine ni muhimu kunyamaza ili kupata majibu na kugundua mitazamo mipya na maono mapya. Sikiliza ukimya na utaona yote ambayo unaweza kujifunza na kujisahihisha.

~ Nyamaa, kaa kimya, katikati ya kilele cha hasira, kaa kimya,
~ Ikiwa maneno yako yanaweza kuharibu urafiki. kaa kimya.
~ Ikiwa maneno yako yatamchukiza mtu, kaa kimya,
~ Ikiwa huwezi kuongea bila kupiga kelele, kaa kimya,
~ Kama huna ukweli wote, kaa kimya.
~ Wakati unahisi kukosolewa, nyamaza.
~ Ikiwa maneno yako yanatoa maoni yasiyofaa.

Ukimya siku zote ni bora kuliko maneno yasiyo na maana.

Kaa kimya! Ukimya ni hekima, Ukimya ni tafakuri, Ukimya ni kujitathmini.

Good morning
Tanganyika
.
 
Asante sana kwa hili
Naunga mkono hoja, na kati ya vitu ambavyo nimeomba sana Mungu ni anifundishe, ni anifundishe kunyamaza.

Japo mimi ni mwalimu mzuri wa kufundisha wengine kunyamaza Swali la Morality: Je, ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele maslahi ya Taifa? lakini kwangu mwenyewe, kunyamaza ni changamoto. Naikumbuka hii Paskali, ukimya si utupu bali ukimya umebeba majibu mengi kuliko maandishi
P
 
Muda na ukimya ndio mambo mema zaidi katika ulimwengu wa leo
 



 
 
Huu ni ukweli mtupu na hongera kwa kutuelimisha. Ni binadamu wachache wamejaaliwa kuitambua hii hekima ya kunyamaza, ziko faida nyingi katika kunyamaza na iwapo ukajaliwa kuwa na uwezo wa kufumba maji kinywani kila unapokutana na nyakati ngumu hasa za maudhi, dharau na mengine mengi yanayofanana na haya huwezi kuingia kwenye ugomvi wa aina yoyote na mtu yeyote.
 
Hii Ni hekima kubwa sana kwenye maisha.Ukimya ukufanya huwe na amani na kujifunza zaidi mitazamo mipya.Asante kwa ujumbe mzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…