Jwtz kuporomoka heshima kimataifa

geophysics

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
904
166
Watu 10 wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja mjini Zanzibar baada ya kupigwa na askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa kambi ya Bavuai Migombani kufuatia mke wa askari mmoja kuibiwa pochi na watu wasiojulikana.
Mwanamke huyo aliibiwa pochi hiyo huko Jang’ombe katika Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.
Habari kutoka eneo la tukio zimeeleza askari hao walianza kupiga watu kwa zamu katika mitaa ya Jang’ombe, Urusi na Mpendae majira ya saa 1:00 jioni juzi na kusababisha watu kukimbia ovyo na maduka kufungwa.
Source: www.ippmedia.com 11/03/2011
 
Watu 10 wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja mjini Zanzibar baada ya kupigwa na askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa kambi ya Bavuai Migombani kufuatia mke wa askari mmoja kuibiwa pochi na watu wasiojulikana.
Mwanamke huyo aliibiwa pochi hiyo huko Jang’ombe katika Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.
Habari kutoka eneo la tukio zimeeleza askari hao walianza kupiga watu kwa zamu katika mitaa ya Jang’ombe, Urusi na Mpendae majira ya saa 1:00 jioni juzi na kusababisha watu kukimbia ovyo na maduka kufungwa.
Source: www.ippmedia.com 11/03/2011

jaman wanajesh wa TZ ni wapole sana ukilinganisha na wa kenya,uganda,kongo na kwingneko! Huwa hawaguswi kabsa ila apa kwetu tunaish nao vizur ila sisi raia ndo tunawachokoza mara nyingi.
 
Muda mrefu jeshi letu limekuwa likipata heshima kimataifa pamoja na umaskini wa taifa letu kutokana na kushiriki oparetion nyingi kwa mafanikio makubwa eg Kagera war, Comoro, Liberia etc.

Ufanisi huo ulitokana na mafunzo mazuri,nidhamu ya askari pamoja na ushirikiano mzuri kati ya askari hao na viongozi wa juu jeshini etc.

Sasahivi niliyotaja kama baadhi ya sababu ya za ushindi hazipo au zipo kwa kiwango cha chini sana.

Tukianza kwenye mafunzo, hali ni mbaya kwani kujiunga na jeshi sasa inachukuliwa kama ajira nyingine yoyote kitendo kinachofanya watoto wa vigogo wengi kujiunga huku wazazi wao wakiagiza kwamba wasifanye mazoezi 'magumu'. Pia viongozi wakuu hawana ushirikiano mzuri na askari wa chini kwani wamekuwa wakiwaona kama mashine za kufanya kazi bila kujali maslahi yao. Mfano, wakati wa maafa ya kilosa askari walishiriki kuokoa na kurudisha hali ya miundombinu iliyoharibika katika hali nzuri na kuahidiwa kupewa posho lakini mpaka sasa hawajapewa.

Si hivyo tu bali hata mitambo iliyonunuliwa na kitengo cha maafa na kukabidhiwa JWTZ ili isaidie kurahisisha kazi ili cheleweshwa kufika eneo la kazi hivyo askari kuumia bila sababu.

Mbaya zaidi baada ya kazi ile kumalizika, mitambo iliyoletwa ilikubaliwa wapewe wataalam wa jeshi ili iweze kutumika kwa wakati mwingine kama itatokea tatizo kama hilo lakini cha kushangaza, bila taarifa za wazi mitambo hiyo ameichukua kigogo mmoja na kuwakodishia SUMA JKT kwa maslahi binasfi.

Kutokana na wakubwa hao baadhi kutowajali askari na watendaji wengine wa chini imefika hatua ya kuwakata hata pesa zinazo tolewa na UN kwa wale wanaoenda DARFUR ambapo kila mwanajeshe bila sababu za msingi hukatwa 20 percent ya pesa za UN huku pesa yake nyingine aliyokuwa apewe ya chakula hapewi bali kuishia mikononi mwa hao vigogo wachache.

Hali hii imefikia kuwavunja moyo askari na kukosa ile nidhamu ya kazi kwa kujua ukweli kuwa wakuu wao wanawaibia.

Hali hii isiporekebishwa heshma ya jeshi letu itaporomoka sana.
 
Jeshi limeshaporomoka. Unatarajia hali hiyo irekebishwe na nani? Na Kikwete? Subutu!
 
Jeshi limeshaporomoka. Unatarajia hali hiyo irekebishwe na nani? Na Kikwete? Subutu!

Mkuu Jasusi, hana ubavu huyu wa kurekebisha chochote. Kila kitu tangu aingie madarakani kimezidi kuwa shakalabaghala na yeye bado anacheka cheka tu na kujiweka mstari wa mbele katika kutatua matatizo ya Ivory Coast wakati yaliyopo kwake yanamshinda.
 
Jeshi limeshaporomoka. Unatarajia hali hiyo irekebishwe na nani? Na Kikwete? Subutu!

tatizo uswahiba wa jk na vigogo hao.
Kwamba anawakingia kifua ,hali ni mbaya labda askari waamue kujikomboa wenyewe.
 
Naunga mkono hoja na sasa nawez kukonekti dots kuwa ni kweli ile milipuko ya g-mboto ilikua salam kwa hao vigogo!!! ni kweli
 
na bado mpaka watambue kuwa hawana kiongozi ndipo wataamuka.
wasipochukua maamuzi ya busara basi kazi kwao.
 
kama jeshi halina mwenyewe vile

Poleni sana Afandi, twajua huko kwenu ukipeleka malalamiko kama haya hakuna atakayekusikiliza, but naomba nikukumbushe kuwa Geshi hili lina wenyewe, na wenyewe ni SISI wananchi, kwa umoja wetu tukiamua itawezekana na heshima ya nchi itarejea. Watanzania tunatakiwa kuacha woga wa kuthubutu, let's take risk, twaweza kwenda....Risk business has high profit!
 
Kumbe jamaa wanaonewa sana aisee, na wameamua kuasi kwa kutembeza kichapo kwa Raia siku hizi...

Kaa mbali na Jeiwii mazee..
 
jeshini kuna siasa nyingi sana-ndo mana wengine wakistaafu wanjikuta wanapewa ukuu wa wilaya na mikoa
 
Jeshi limeshaporomoka. Unatarajia hali hiyo irekebishwe na nani? Na Kikwete? Subutu!

Wanajeshi wasiokuwa na nidhamu kazi yao ni kupiga raia wasio na hatia AIBU! Heshima yao itarudi ukija utawala wa chama kingine ambacho sio CCM kwa sababu CCM ni wezi hawawezi kubadili mfumo wa kifedhuli.
 
Mimi kwenye suala la milipuko ya mabomu ndo nimeachwa hoi na nimekosa imani nalo kabsaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom