Julius S. Mtatiro
11 hrs ·
USHAURI WA BURE.
Msiwatukane wanaohama kwenye chama chenu ili siku wakirudi msianze kazi ya kusameheana matusi yenu na ama kununiana.
Kafulila alikulia ndani ya CHADEMA, baadaye akahamia NCCR MAGEUZI, kisha akarejea tena CHADEMA na hivi sasa amehamia CCM (amehama vyama mara 4).
Na mfano mwingine ni mwalimu wangu Prof. Kitila, amekulia ndani ya CCM (sina hakika kama aliwahi kuwa NCCR) lakini tunajua alihamia CHADEMA, akatoka CHADEMA akaanzisha ACT, na sasa ameiacha ACT amekwenda CCM.
Huo ni ushahidi thabiti kuwa wapo wanasiasa safari zao kisiasa huwa ziko namna hiyo, huhangaika sana lakini kibinadamu lazima tuwaheshimu kwa dhati. Hata binadamu anapokuwa anafariki yupo ambaye hufa kwa utulivu na yupo ambaye hufa kwa kuhangaika sana.
Msishangae kuwa baada ya mwaka mmoja au miwili Kafulila akarudi CHADEMA, Masha akaenda ACT, Patrobas akaenda CUF na Kitila akaanzisha chama kipya.
Kama mnachanganywa na hali hii ya sasa inaonekana mtakuwa wendawazimu kabisa siku mtakaposikia Kafulila ameichoka tena CCM na anahamia ACT na akitoa hoja kuwa "CCM imeshindwa kuongoza nchi!"
Msichanganywe na hali ya sasa ili msije kupumbazwa na hali ya baadaye. Nawasisitiza, waheshimuni wahamao, Songeni UGALI wenu na laleni usingizi, hakika kesho kutakucha na hali ya uchumi wa nchi itaendelea kudidimia, pambaneni na hali zenu, waacheni wahamao nao wapambane na hali zao.
Mtatiro J