Joyce Kiria: Darasa la saba tu lakini mambo makubwa

Amavubi

JF-Expert Member
Dec 9, 2010
30,145
13,216
pic17.png

Mtangazaji Mashuhuri wa Kipindi cha Wanawake Live Bi Joyce Kiria leo 06/03/2012 ameweka bayana kiwango chake cha elimu na kusema kwamba licha ya kwamba ameishia darasa la saba tu lakini ni mwanamke anayeweza kujivunia kwa mafanikio aliyonayo hadi sasa kwa kuweza kumiliki kampuni mbili ikiwemo ya Local Media Entertainment.

Ameyazungumza hayo na kuishia kububujikwa machozi wakati wa maadhimisho ya kuelekea siku ya mwanamke duniani aliyoandaliwa na WiLDAF katika ukumbi wa Karimjee (mtoa makala alikua shuhuda) na kusema kwamba mfumo wa elimu uliopo sasa unamkwamisha kuendeleza kipaji chake.
 
big up sana kwa Joyce kiria,hata ukiangalia kipindi chake utaona ni jinsi gani anavyostahili kupongezwa kulingana na historia yake na alipo sasa amepiga hatua kubwa ya maendeleo na kingine anajiamini sana. Hongera dada kaza buti,nakutakia jitihada zaidi na mafanikio zaidi ya ulipo sasa.
 
duuuuh...kazi kweli kweli..............ati wanasema wanawake hatupendani, ni kweli????

Hivi mtu ana akili zake atasimama vipi kwenye media asema elimu haina umuhimu katika maisha ya mwanadamu alafu awekwe kwenye kundi la ma role model??? hapa sio swala la kupendana au kuchukiana....ila hana vigezo vya kupewa sifa mlizo mpa.
kwanza interview zenyewe anazo host kwenye kipindi chake full kuwa comand wageni wake.., na kuwapangia cha kusema (yani kinachomfurahisha yeye)...kwa kweli AKAJIPANGE UPYA, AJE KIVINGINE AKIWA ANA ELIMU LAKIN KWA PALE ALIPO SIDHANI KAMA ANA MIAKA 2 MBELE KUENDELEA KUMAINTAIN STATUS .... Kama amekutuma umpe promo mwambe hujatukuta
 
Kimeo tu.yeye na Sipora wanaitaji shule. Watanzania tuamke tusiwape sifa za kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa.huyu,kanumba,ray,ze komed wanaitaji shule.tusiwape sifa wasizostaili.

Sawa tumekuelewa, tutakupa sifa wewe mpiga majungu unajua sana kupiga majungu watu wenye maendeleo,wakati wewe huwafikii hata robo.
 
Sawa tumekuelewa, tutakupa sifa wewe mpiga majungu unajua sana kupiga majungu watu wenye maendeleo,wakati wewe huwafikii hata robo.

Ana maendeleo gani? au coz ni mke wa CHADEMA (kilewo) teh teh kama Joyce ana maendeleo basi Rita, akina mama Nkya na wengineo watakuwa sijui wako kwenye high mass consumption (maturity stage according to Rostow)
 
Mrembo by Nature said:
Hivi mtu ana akili zake
atasimama vipi kwenye media
asema elimu haina umuhimu katika
maisha ya mwanadamu alafu awekwe
kwenye kundi la ma role model???
Nionyeshe sehemu aliyotamka hayo maneno kwenye hìi thread??!
Amavubi said:
na kusema kwamba mfumo wa elimu uliopo sasa
unamkwamisha kuendeleza kipaji
chake......
Hayo maneno ndo niliyoyaelewa mimi!!
Mrembo by Nature said:
Wivu gani wa kumuonea Joyce? hzo
ndoa mbili au?? kuomba talaka?
may be coz alivaa shela mara
mbili
Tatizo lako hasa nini!? We uliyesoma una nini cha ziada kumshinda yeye!? Mwenzako kwa sasa anaendesha familia za watu kwa kupitia fedha anazowalipa wafanyakazi wake kwenye hz kampuni!? Wewe je au ndo wivu wa kike!?
 
Ana maendeleo gani? au coz ni mke wa CHADEMA (kilewo) teh teh kama Joyce ana maendeleo basi Rita, akina mama Nkya na wengineo watakuwa sijui wako kwenye high mass consumption (maturity stage according to Rostow)

Najua roho inakuuma sana ila huna la kufanya,kilichobaki usijenge chuki kama shida ni za kwako vumilia tu.
 
still elimu bado ni muhimu.
kwa maelezo yake tu nimeshaona kasoro Inayosababishwa na elimu
Hapo angekuwa na kampuni moja ikawa ina operate hiyo nyingine as subsidiary na kampuni kubwa as a parent company kuliko kuwa na kampuni mbili tofauti wa tz wanaona kuwa na kampuni nyingi ndio inshu wakati unaweza kuwa na kampuni moja ikawa ina operate kampuni mbali mbali aje kule jukwaa la biashara aanzishe thread tumsaidie
Darasa la saba sio mchezo
 
Back
Top Bottom