Joseph Mbilinyi (SUGU) MB afanya kweli Mbeya Mjini

Joseph Mbilinyi (SUGU) MB afanya kweli Mbeya Mjini

...Kubali tu kuwa Mbeya huijui,hapo sio Mbeya...

Ni kweli haijui mbeya....hapo ni round-about kuu ya CCM jijini Mwanza....makutano ya Airport road,Kenyatta road,Nyerere road,na Region Drive......Kamwe picha sio mbeya....na kama anaweza kuzoom ajaribu kufanya hivyo ataliona jengo NCU na Benki kuu kwa mbali!
 
Mwaka 2015 wananchi wa Mbeya Mjini hawatarudi kosa kumpa kura mpiga porojo-SUGU
 
Mwaka 2015 wananchi wa Mbeya Mjini hawatarudi kosa kumpa kura mpiga porojo-SUGU

Na ndio tatizo la kuchagua watu mediocre na ambao hawana upeo.
Mie sina tatizo nachana lakini ni vyema kuchagua watu wenye upeo mkubwa, si wa machinga mentality.

Sasa hivi "kijiji kikubwa" cha Mbeya kimesha geyzwakuwa Chinga town, machinga mpaka milangoni mwa benki.

Cheap leaders with cheap visions.
 
Legacy ya Sugu hapo Mbeya ni hao machinga, katoka machinga amechaguliwa na machinga na jiji lita baki kuwa la kimachinga.

Kwa kukosa miundombinu iliyoenda shule, moto Mwanjelwa na kila soko kuu hauishi kila mwaka.

Mbaya zaidi umachinga umachinga emeanza kuzoeleka na jiji badala ya kuendelezwa viosk vimetandazwa kati kati ya jiji zima na soko hadi main streets karibu na Sokoine stadium.

Huu mimi naita uozo unaotokana na kuwa na akili ya kimachinga pamoja na uwakilishi wake.

machinga ndo waliomchagua na ana watendea haki mtachonga sana na atawabuluza tena kama kawaida....na atazid kuwakilisha we endelea kupiga domo utazd kuumia roho 2015 na roho yako mbaya
 
machinga ndo waliomchagua na ana watendea haki mtachonga sana na atawabuluza tena kama kawaida....na atazid kuwakilisha we endelea kupiga domo utazd kuumia roho 2015 na roho yako mbaya
Mkuu tatizo hulielewi hapa, tatizo nibeya "kijiji kikubwa" kugeuzwa public toilet.
Kana wewe unaridhika na hilo basi ndo ukomo wa uwezo wako kufikiri.
 
Kitu anachoweza kufanya msanii wenu ni kupiga miluzi tu, katurudisha nyuma maendeleo Mbeya mjini miaka mitano mizima!
Mtoa posti hapo kama huelewi kuwa hilo la machinga ni tatizo kubwa basi inaelekea umetoka kijijini jana, una uzoefu tu wa kuuza mazao kando kando ya barabara.
Sasa mnakuja mitandaoni kumtetea wakati muda umesha kwisha, 2015 Sugu kwishney!

wewe ni muogo mkubwa,Mbeya imebadilika sana tangu Sugu alipoingia na hasa baada ya kata za mjini kuchukulia na madiwani wa CDM, kajigili pamoja na Boid, na vijana hawa wamekuwa wakali sana kwenye mapato na matumizi ya jiji.Usitake kupotosha watu.

Mbeya imebadilika sana kwa kipindi cha miaka isiyozidi mitatu.
 
Legacy ya Sugu hapo Mbeya ni hao machinga, katoka machinga amechaguliwa na machinga na jiji lita baki kuwa la kimachinga.

Kwa kukosa miundombinu iliyoenda shule, moto Mwanjelwa na kila soko kuu hauishi kila mwaka.

Mbaya zaidi umachinga umachinga emeanza kuzoeleka na jiji badala ya kuendelezwa viosk vimetandazwa kati kati ya jiji zima na soko hadi main streets karibu na Sokoine stadium.

Huu mimi naita uozo unaotokana na kuwa na akili ya kimachinga pamoja na uwakilishi wake.

Usipotoshe watu,soko la sokoine ni temporary baada ya kuungua soko kuu.lazima ufahamu kuwa kutumika mahali hapo kama soko la muda ni maamuzi ya Halmashauri kupitia madiwani.sasa hapo unamlaumu sugu kivipi?Jengeni soko la uhindini ili hapo mahali parudi katika mpango wake wa awali.
 
Usipotoshe watu,soko la sokoine ni temporary baada ya kuungua soko kuu.lazima ufahamu kuwa kutumika mahali hapo kama soko la muda ni maamuzi ya Halmashauri kupitia madiwani.sasa hapo unamlaumu sugu kivipi?Jengeni soko la uhindini ili hapo mahali parudi katika mpango wake wa awali.

Usitetee uchafu huo hata kama ni temporary
 
Mmm !!!! Mbeya yataka moyo usanii mwanzo mwisho !! mbaya zaid mpaka kwa watu wasomi tunaowategemea siasa imewachakachua kiasi kwamba wanacheza ngoma kama vipofu!!! ukifika mahali unabeza kazi na juhudi za wazi zilizofanywa na hata kufikia kuzichakachua kuwa ni kazi za sugu tumekwisha kwani "FELIX MWAKYEMBE NI MWALIMU WANGU" Namkubali sana ila kwa hii article ni shaka kwani anafahamu vizuri miradi hii??? na ni baadhi ya miradi ikiwepo ya hostel za jiji, soko (mwanjelwa) office ya jiji, na shule mbalimbali za kata zipatazo 28 na dispensary, zimetokana na watu kuandika paper zao na kushawishi kwa kwenda mbele kupata fedha hizo ili miradi iende, Mh wangu Sugu kwa mbeya anatakiwa kutuliza kichwa ili aweze kuja na legacy ya kwake badala ya kumdanganya kwa kazi za wenzake aonekane anaperform, kiufupi labda mwakyembe angeniambia kuzagaa kwa wamachinga na uchafu kukithiri ni juhudi za viongozi wa awamu hii ningeweza kukubaliana naye.

wtu kuandika paper ni issue sio issue,kwani tuna papers ngapi zimefungiwa kwenye makabati?Issue ni kuzitafsiri hizo papers na impementation.
 
Ndiyo imebadilika for worse.

Machinga wametapskaa kila kona, wanajisaidia hovyo kila mahali.
Pale Soloine stadium ndo soko ambalo mfo kituo kikubwa cha vioski uchwara vilivyotapakaa centre ya joji zima.

Na huo ndio ukomo wa kuupangilia mji wa Mbeya wakati Mwanza na Arusha maghorofa yanapanda.

Kubali tu mkuu upeo wenu mdogo, si vibaya mkijifunza toka miji niliyoitaja.

nachokisema hapa ni nini chanzo cha machinga kuzagaa mjini,unaweza nijibu hilo?
 
wewe ni muogo mkubwa,Mbeya imebadilika sana tangu Sugu alipoingia na hasa baada ya kata za mjini kuchukulia na madiwani wa CDM, kajigili pamoja na Boid, na vijana hawa wamekuwa wakali sana kwenye mapato na matumizi ya jiji.Usitake kupotosha watu.

Mbeya imebadilika sana kwa kipindi cha miaka isiyozidi mitatu.
Ndiyo, Mbeya imebadilika for worse.

Machinga wametapakaa jiji zima wakijisaidia hovyo kila mahali.
Huhitaji kwenda shule kuambiwa hapo kutakuwa makao makuu ya kipindupindu.

Soko karibu na Sokoine Stadium ndo kitovu cha vioski uchwara centre ya jiji.
Yote yanatendeka wakati miji inayoongozwa kimakini zaidi kama Arusha, Moshi ma Mwanza maghorofa yana panda.

Halafu mkiambiwa mna mentality na upeo wa machinga mna kataa.
 
Shughuli kuu ya kiuchumi inatoa taswira ya jiji husika....manispaa ya moshi na jiji la Arusha kwa mfano vinategeme shughuli ya utalii....wakati Tanga uliandaliwa kuwa mji wa viwanda enzi za uhai wa bandari....na mbeya ni miongoni mwa jiji katika mikoa minne ya kilimo kikuu Tanzania!

....Hiyo ndio excuse ya ku-end up na "kijiji kikubwa"!?........kwa hiyo Mkoa ukiwa wa Kilimo Kikuu kama unavyodai ndio kusiwe na mipango miji.......unajua background ya miradi kama USRP?............tusijiridhishe na mediocre status ya sehemu kwa kisingizio kisicho na msingi.............
 
sasa tunaanza kutukanana au?
Ndio maana nasema ukiwa na mentality ya machinga huwezi kureflect kuwa soko lisilo kuwa controlled na vioski katikati ya jiji ni uchafu.
Na katika hilo kama huja nielewa, hutanielewa daima.
 
Ndio maana nasema ukiwa na mentality ya machinga huwezi kureflect kuwa soko lisilo kuwa controlled na vioski katikati ya jiji ni uchafu.
Na katika hilo kama huja nielewa, hutanielewa daima.

Mimi nimekuuliza swali unajua chanzo cha hilo tatizo?unajua watu walikaa na kuona temporarily soko lijengwe hapo wakati wanasubiri fedha za kujenga upya soko kuu?unajua kuwa hayakua maamuzi ya mtu mmoja?unajua kuwa machinga huwa hawabishi hodi?unajua kuwa inaweza kuwa ni strategy ya kuonyesha kuwa mji ni mchafu ili nyie mnaopinga mtafute sababu ya kuchukua jimbo?unajua kuwa kuwa sokomatola ingeboreshwa then hakukua na haja ya watu kuwekwa hapo sokoine ,wangehamia sokomatola?Unajua kuwa wakati watu wanahamishiwa hapo soko la mwanjelwa lilikua limeungua ,na ujenzi ulikua unaendelea?unajua kuwa soko la sido nalo lilikuja kuungua? so unaweza ktuambia mahitaji ya wakazi wa mbeya yangetoka wapi kwa kipindi chote ambacho masoko yameungua?
 
Aina ya siasa hizi za vipofu kama wewe ndio zimetusaidia Tanzania na hasa Mbeya tuendelee kuwa kama tulivyo. Katika hali ya kawaida kabisa nilitegemea ungebisha kwa hoja na kushambulia vipengele ambavyo nimeweka ushabiki wa kisiasa kama upo, kwa mshangao wangu na wapenda nchi/,mbeya wengine umekuja na majumuisho mepesi kama kwamba hujui kusoma wala kuandika.

Kama wewe ni mzazi inasikitisha kwa sababu sifikirii wewe kama mzazi upeo wako ndio huo, hao wanao nadhani watakuwa na hali mbaya sana!

Hivi pale niliposema viwango vya barabara si vizuri nilikuwa namshambulia nani kwa upeo wako?

Mungu ibariki Tanzania tajiri yenye wakazi masikini zaidi duniani.

jking katika vipofu na matahira na vihiyo nawe pia unaongoza . Mtu mwenye akili timamu na si mjinga mjinga kama mkwawa na wewe hii haiwezi kua hoja ya kujidai. Ni wazi unajua hamna anachofanya sugu zaidi ya kurukaruka tu. Plz kwa heshima ya wanambeya hoja zisizo na mashiko kumsifu mpuuzi wenu sugu mkome. Hizi ndo siasa mtelezo sasa
 
Mimi nimekuuliza swali unajua chanzo cha hilo tatizo?unajua watu walikaa na kuona temporarily soko lijengwe hapo wakati wanasubiri fedha za kujenga upya soko kuu?unajua kuwa hayakua maamuzi ya mtu mmoja?unajua kuwa machinga huwa hawabishi hodi?unajua kuwa inaweza kuwa ni strategy ya kuonyesha kuwa mji ni mchafu ili nyie mnaopinga mtafute sababu ya kuchukua jimbo?unajua kuwa kuwa sokomatola ingeboreshwa then hakukua na haja ya watu kuwekwa hapo sokoine ,wangehamia sokomatola?Unajua kuwa wakati watu wanahamishiwa hapo soko la mwanjelwa lilikua limeungua ,na ujenzi ulikua unaendelea?unajua kuwa soko la sido nalo lilikuja kuungua? so unaweza ktuambia mahitaji ya wakazi wa mbeya yangetoka wapi kwa kipindi chote ambacho masoko yameungua?
Ni mtu mvivu wa kufikiri na kuplan ndio anasubiri matukio yamkute ndio agutuke kuwa hakufanya kazi nzuri.

Kwa upande wangu sina haja ya kujiuliza hayo maswali wakati watu wa kufanya kazi hiyo wapo na wanakula viyoyozi.
Na ukweli ni kuwa wanatutapeli kutusambazia vioski mji mzima vitakavoleta takataka na kipindupindu, huku wanalipwa mishahara na osho za bure.
Wawilishi wa wananchi kama Sugu wasiona silaha ya uelewa Town Planning ni mdudu gani, hapo ndo tunaishia na uozo tunao uona Mbeya.
 
Msiwadanganye watu ambao hawajafika Mbeya.

Miradi hiyo haikuanzwa wala kufikiriwa na huyo mpiga zumari, Sugu
Miradi mnayoitaja mingine imekuwepo hata kabla Sugu hajaanza kuimba.

Kanyaga twende kamanda Sugu,kazi yako hapa Mbeya inakubalika sana. Mipango yako ya kusaidia machinga inafahamika vizuri kwa wanambeya mjini,
 
Sishabikii machinga kuwa barabarani lakini nahoji kwa nini barabara kubwa kama ile imepita katikati ya mji mkubwa kama Mbeya!? Kwanini isinge kwepeshwa kama kuanzia Uyole mpaka Mbalizi hivi!! Hata kama machnga wasingekuwepo hapo Mwanjelwa baada ya miaka 5 kutoka sasa bado kutakuwa na foleni kwa sababu hapo ni center ya Mbeya. Barabara kama Mandela pale Dsm bado inafoleni ya kutupa hata baada ya kuipanua kwa sababu ya hizo transit vehicles, maeneo kama Tazara, Buguruni, njia ya panda ya Tabata, Tabata relini na Ubungo.
Alafu mbunge hafanyi hizo kazi pekee yake na pia sio anatoa pesa mfukoni mwake na hayo ndio matatizo yetu tunafikiri mbunge kazi ya kufanya hizo kazi au kuzilipia kwa pesa yake, badili mtazamo wako msaidie mbunge wako (SUGU) hata kama itikadi yako ni tofauti na ya kwake, kwa sababu usipofanya hivo subiri miaka 5 ya bila maendeleo
Msiwadanganye watu ambao hawajafika Mbeya.

Miradi hiyo haikuanzwa wala kufikiriwa na huyo mpiga zumari, Sugu
Miradi mnayoitaja mingine imekuwepo hata kabla Sugu hajaanza kuimba.

Zaidi ya hapo hebu mtuonyeshe jinsi huyo Sugu anavyoweza kuondoa machinga barabarani pale Mwanjelwa.
Barabara ya kimataifa imegeuzwa kuwa uchochoro wa mtaa wa Congo, na foleni haziishi tokea Mafiati hadi Sai.

Kama huyo Sugu wenu ana akili ya kumtosha atatue hilo tatizo- hapo mtasikia ooooh, sie hatuhusiki!!
 
Sishabikii machinga kuwa barabarani lakini nahoji kwa nini barabara kubwa kama ile imepita katikati ya mji mkubwa kama Mbeya!? Kwanini isinge kwepeshwa kama kuanzia Uyole mpaka Mbalizi hivi!! Hata kama machnga wasingekuwepo hapo Mwanjelwa baada ya miaka 5 kutoka sasa bado kutakuwa na foleni kwa sababu hapo ni center ya Mbeya. Barabara kama Mandela pale Dsm bado inafoleni ya kutupa hata baada ya kuipanua kwa sababu ya hizo transit vehicles, maeneo kama Tazara, Buguruni, njia ya panda ya Tabata, Tabata relini na Ubungo.
Alafu mbunge hafanyi hizo kazi pekee yake na pia sio anatoa pesa mfukoni mwake na hayo ndio matatizo yetu tunafikiri mbunge kazi ya kufanya hizo kazi au kuzilipia kwa pesa yake, badili mtazamo wako msaidie mbunge wako (SUGU) hata kama itikadi yako ni tofauti na ya kwake, kwa sababu usipofanya hivo subiri miaka 5 ya bila maendeleo
Asante kwa mchango mzuri Zuberi Jr .
Tupo amoja katika kuliona tatizo la barabara ya Uyole mpaka Mwanjelwa.
Simlaumu Sugu kwa kulisababisha bali kwa kutokuwa chachu ya utatuzi wa tatizo hilo.

Tatizo kubwa la barabara hii ni mapungufu makubwa katika Master Plan ya jiji la Mbeya. Hiyo barabara haipo tena katika viwango vya highway bali sasa ni street-barabara ya mitaa.

Wakati barabara hiyo inajengwa hapakuwepo juhudi zozote kupanua au kujenga barabara za sambamba ili kuchukua traffic ya jiji la Mbeya.
Na vile vile hapakuwepo juhudi zilizokwenda shule kukidhi miundo mbinu mbadala kwa ajili ya shughuli za wananchi kama soko au viwanja vya michezo- hasa sehemu walipo watu wengi.
Na ndio tuaona sasa kila mwenye biashara anakimbilia Mwanjelwa, kuanzia mchoma mahindi, mchonga grilli hadi hoteli ya kisasa.
Picha inayojitokeza ni atotally unplanned settlement.

Sina uhakika kama ZuberiJr unajua kwamba zamani barabara kuu ilikuwa inapitia Mafiati,Lupa Way hadi Meta.
Tutaendelea kuhamisha barabara mpaka wapi badala ya kuwa ma mipangilio mizuri ya miundombinu.

Ndio maana kizazi hiki tunahitaji watu wa kusaidia kutatua matatizo sio nyimbo zisizoisha.
Utatuzi wa matatizo ya Mbeya mjini, pamoja na la machinga si kuwashabikia bali kutengeneza au kuboresha Masterplan ya jiji ili liondokane na sura ya "kijiji kikubwa".
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom