Joram Kihango vs Willy Gamba

Ulikuwa unavutiwa zaidi na yupi kati ya wakali hao?

Yaani umenikumbusha mbali sana! Hiyo miaka ya mwanzoni mwa 80, nikiwa sekondari, alikuwa hatumwi mtoto sokoni!!! Mwalimu anaandika notisi ubaoni, mimi ninamsoma Willy Gamba kwenye Kikosi cha Kisasi, Njama,nk, nimekiweka chini ya benchi! Msisimko wa ajabu kama unaangalia sinema vile!
 
Willy Gamba alikuwa mwisho wa maneno. Kikosi cha kisasi na kile kingine cha 'kufa na kupona' vilikuwa vimetulia sana.
 
Kama kutatoke mtu akajribu kuigiza moja ya riwaya za Ben na Msiba basi zitakuwa kali sana, kuliko hizi za sasa amabzo hazina maudhui wala hujui zinaanzia wapi na zinaishia wapi.
 
Joram Kiango malaika wa Shetani..lakini wote kwa ujumla Riwaya zao zilikuwa nzuri sana .
Hivi mbona sasa hazipatikani?anayejua zunzuzwa waoi tafadhari tuwasiliane

Zawadi ya ushindi mtunzi alikuwa nani nimesahau?

You mean kati ya waandishi wenyewe Elvis Msiba (Willy Gamba's) na Ben R. Mtobwa (Joram Kiango's na Inspekta Kombora)? Mimi sijui.
Eti lakini nasikia watoto siku hizi nao wanasoma riwaya za akina Shigongo. Kweli waandishi wamekwisha. Basi niliona title moja ya kitabu "The President Loves my Wife" halafu ikatafsiriwa tena kwa kiswahili; "Rais Anampenda Mke Wangu". Yaani Heading tu unachoka unajua kwamba hapa hamna kitu kabisa.

Msiba na Mtobwa wameandika vizuri sana riwaya za kiswahili, hasa upande wa mambo ya upelelezi sababu walikuwa wanajaribu kuwaiga waandishi wengi sana mahiri wa novel hasa za kiingereza, mojawapo akiwa ni James Hardley Chase. Kuandika riwaya nzuri na zenye reflection kwenye maisha halisi ta watu, ...kunahitaji umakini wa hali ya juu sana. I really admire these people anyway!
 
Yaani umenikumbusha mbali sana! Hiyo miaka ya mwanzoni mwa 80, nikiwa sekondari, alikuwa hatumwi mtoto sokoni!!! Mwalimu anaandika notisi ubaoni, mimi ninamsoma Willy Gamba kwenye Kikosi cha Kisasi, Njama,nk, nimekiweka chini ya benchi! Msisimko wa ajabu kama unaangalia sinema vile!
Jamani hii thread imenikumbusha mbali sana,nilisoma karibia vya waandishi wote lakini vya Willy Gamba ni funga kazi!!niliwahi pata uvumi kuwa alipigwa stop kuandika vitabu vya namna ile kwani vinaweza kufundisha watu technique za kijasusi na hata ujambazi,don't know kama ni kweli!:confused2:
 
All in all,Ben Mtobwa alikuwa juu zaidi ya Musiba,kuna kile kitabu chake cha "pesa zako zinanuka",kinaelezea jinsi gani mafisadi wanavyoweza kubadilisha moyo wa kijana mpya kwenye ajira mpaka akafanya wanayotaka wao,"zawadi ya ushindi",ambacho kinatumika mpaka mashuleni,Dar es salaam usiku,nyuma ya pazia,tutarudi na roho zetu,mtambo wa mauti,malaika wa shetani,roho ya poka,(rip)ben
 
All in all,Ben Mtobwa alikuwa juu zaidi ya Musiba,kuna kile kitabu chake cha "pesa zako zinanuka",kinaelezea jinsi gani mafisadi wanavyoweza kubadilisha moyo wa kijana mpya kwenye ajira mpaka akafanya wanayotaka wao,"zawadi ya ushindi",ambacho kinatumika mpaka mashuleni,Dar es salaam usiku,nyuma ya pazia,tutarudi na roho zetu,mtambo wa mauti,malaika wa shetani,roho ya poka,(rip)ben

Lakini Hassan, hapana; umechanganya. Hawa jamaa wanaweza kuwa ngoma droo. Unakumbuka kile kitabu cha Msiba kilichkuwa kinaongelea wizi wa almasi Mwadui, halafu alikuwepo pale shushushu watu wakiwa wanajua kuwa ni kicha amevaa malapulapu, anaokota makopo na kula mabaki yaliyotupwa kwenye majalala ya taka, analla nje kwenye mitalo halafu muda wote anakuwa anaongea maneno "saa za afrika", kumbe alikuwa anamaanisha "South Afrika"? Uliwahi kukisoma hicho kitabu? Partly huwa nakifananisha na picha moja ya James Bond 007 inaitwa DIAMONDS ARE FOPREVER!
 
Duuh umenikumbusha mbali saaaana... Kile kitabu cha "Dar es Salaam usiku kilisababisha mdogo wangu aliyekuwa darasa la tatu enzi hizo 1986 apigwe sana mikanda na dingi... Doh Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Ben Mtobwa!!!
 
Nilibahatika kusoma njama,nikatamani sana kuwa mpelelezi hasa Willy Gamba alivyokuwa akifanya action na kummega mdada Vero,nimeishia kuwa mkulima na mfugaji maarufu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom