Jokate Mwegelo ameipaisha Kisarawe, ni zaidi ya Mkuu wa Wilaya

Kwa interest zako,watu wafanye kazi anasifiwa mkuu wa wilaya.ongeza juhudi za kuhongwa ili utoe sifa
 
Yaani..huko insta ndio usiseme mpaka nikawa najiuliza amekuwa waziri au??
Kuna wapumbavu wanasifia mtu kutimiza majukumu yake kwa kodi zao!

Akina Mwalimu wangekua wanaita mikamera kwenye kila tukio la kutekeleza majukumu yao sijui ingekuaje!

Nadhani tungekua na maktaba ya picha ya Taifa!
 
Zilikuja nyuzi nyingi humu za bwana Sabaya... mwisho wake tunaujua. Am just saying!!
 
Kazi anayopiga huyu dada+uzuri/ urembo wake... aiseee she's so blessed
FB_IMG_16225550962416634.jpg
 
Sio rahisi. Mama anabadilisha watu vituo. Bila shaka atapelekwa Ilala kama sio Dodoma mjini.

Tuache majungu wakuu. Kama mtu anachapa kazi tumpe pongezi zake.
Siyo majungu mzee, ukiona mtu anatumia sana media kujitangaza jua kuna shida hapo, huyu mdada kila anachofanya lazima aite macamera, hata akikarabati choo cha shule macamera! Kuna wakuu wa wilaya wanafanya vizuri kuliko yeye ila sababu siyo watu wa macamera hatuwajui!!
 
Tena kama hayo maendeleo yangekuwepo yamkini yangetokana na upendeleo ulosababishwa na ukaribu unasemekana kati yake na mwendazake.?! Unapolinganisha na Wilaya nyingine.

Kwamba kila ushirikiano au msaada wa kiufundi au kama fedha ulipatikana kirahisi pale ulipohitajika sababu watoaji waliogopa kushitakiwa kwa mwendazake kuwa wanamkwamisha bidada? Ambapo wangeweza kutumbuliwa?!

Inahitaji tafakari!
 
Nilichogundua watu wengi ni kama wachawi tu, Yafaa kumpongeza, kisarawe ikivutiwa kiwanda kimoja kikawekwa pale pata mahali pazuri mno,HONHERA JOKATE PAMOJA NA UZURI WAKO IPO SIKU NITAKUJA KUKUSALIMU.
 
Salaam Wakuu,

Natumia nafasi hii kumpongeza Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo kwa kuipaisha Kisarawe, Kielimu na Kiuchumi.

Wakati anateuliwa nilimbeza sana na kumuona kama kapendelewa. Wengine Walidiliki kusema kwamba ni Nyumba ndogo ya mtu fulani ndo maana kateuliwa. Ila kafanya kazi Vizuri hata zaidi ya Baadhi ya Wakuu wa Mikoa wapenda Kiki.

Kisarawe ni moja kati ya halmashauri tisa za mkoa wa Pwani.Imeanzishwa tarehe 1 Julai 1907.Wilaya ya Kisarawe inapakana na Wilaya ya Mkuranga kwa upande wa Kusini-mashariki na Wilaya ya Morogoro upande wa Magharibi.Mashariki-Kaskazini kuna Jiji la Dar es Salaam, Kaskazini Wilaya ya Kibaha na Kusini Wilaya ya Rufiji. Lakini Utafikiri Kisarawe ndo Mkoa kumbe ni Wilaya tu kati ya Wilaya 9.

Pamoja na kukuta watu wa Pwani ni Wavivu, kwa muda mchache aliokaa Kisarawe, ameitambulisha kimataifa. Kisarawe imekuwa Maarufu. Kisarawe imekuwa maarufu zaidi hata ya Mkoa wa Pwani. Utendaji wake wa Kazi, umefanya Kisarawe kufunika Wilaya nyingine za Pwani.

Kuna baadhi ya Mambo ambayo ameyafanya na yanaonekana.

Elimu

= Wanafunzi walikuwa watoro na Shule za Kisarawe zilikuwa Zinafanya Vibaya, lakini sasa Zinafanya Vizuri.

= Wilaya ya Kisarawe aliikuta inauhitaji wa madawati 1166 ambapo kwa sekondari uhitaji ni 484, na 642
kwa shule ya msingi. Kafanyia kazi

= Alikuta Wilaya ina uhitaji wa shilingi milioni 124 kwa ajili ya kujenga matundu ya vyoo 113 Mashuleni, kafanyia kazi

= Alikuta Wilaya inauhitaji wa ofisi za Walimu za kisasa katika shule 14 ambazo zinagharimu shilingi milioni 880. Kafanyia kazi

= Alikuta Wilaya haina Maktaba, zinajengwa.

= Alikuta Kisarawe ina matatizo ya Maji. Kwa muda mfupi tatizo la Maji limepungua.

= Huduma za afya zimeboreka hasa huduma ya Mama na Mtoto. Ujenzi wa Wodi ya Upasuaji.

= Huduma ya Umeme imeboreka nk.

Ameweza kufanya mambo ya Maendeleo bila kuwasumbua vyama Pinzania wala kujenga Chuki kwa Wananchi. Hajihusishi na Ufusadi. Ana heshima kwa Kila mtu na ni msikivu.

Jokate ni Mfano kwa Viongozi wanaoteuliwa sasa.

Natamani angepewa Wilaya ya Kinondoni akamalize Migogoro ya ardhi.

Atawadanganyeni wachache tu msio na Fikra pana. DC Jokate Kipindi cha Hayati Rais Dkt. Magufuli wala alikuwa hana muda na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete.

Baada ya kuona Hayati Rais Dkt. Magufuli hayupo tena duniani na kuwa na wasiwasi na Cheo chake hicho sasa ameamua Kujipendekeza kwa Rais Mstaafu Kikwete ( ambaye ndiye Mshauri Mkuu wa Rais Samia ) ili ampiganie asimuondoe katika hiyo nafasi aliyonayo ya DC na ikibidi hata apandishwe kwa Kuteuliwa kuwa Mbunge.

Sasa wenye Fikra pana tumeshaanza kupata hisia kuwa katika Mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya ( ambayo muda wowote yanatangazwa ) kwa Kitendo cha DC Jokate Kujikomba kwa Rais Mstaafu Kikwete sasa hatotolewa hapo Kisarawe sana sana atahamishwa tu kwenda Wilaya nzuri zaidi au hata kuteuliwa kuwa Mbunge.

Ukita Uteuzi sasa Jipendekeze kwa JK.
 
Kwa mtu wa aina yake hata ukimpongeza ni sawa tu, binafsi sikutegemea kama angestahili ofisi yoyote ya umma.

Itoshe tu kusema amejitahidi.
 
Mtu anapongezwa kwa kufanya kazi zake?

Postman akifikisha barua au mzigo mahali husika tunahitaji kumpongeza?
Kwa mahali nchi hii ilipofika, ukiona mtu Serikalini ametekeleza majukumu yake mshukuru tu Kwa kweli..

Maana wengine hawatekelezi na cha kuwafanya hatuna.
 
Jokate yupo smart kichwani hadi kiutendaji,,mama hawezi kumpiga chini,tetesi ni kwamba anaenda wilaya ya temeke
Jokate yupo smart kichwani hadi kiutendaji,,mama hawezi kumpiga chini,tetesi ni kwamba anaenda wilaya ya temeke
Temeke hapawezi kabisaa,miongoni mwa wilaya zinazotaka uwe na maamuzi haswaaaa,Maana kwanza kuna viwanda vingi,bandari,wavuja jasho wengi,Wanafunzi wazazi wanaotegemea huduma Zaid za serikali kuanzia elimu, afya na maj.
Usafiri mkubwa ni daladala ,huku ni mtu ana nauli ya kwenda na kurudi tu humuelezi kitu.
Kila siku kusolve migogoro n.k
Jokate anaziweza wilaya ambazo bado Zina ushamba mwingi ili aweze waleta wasanii washangae shangae,event za kisanii Zaid kama mialiko kedekede,pichapicha nyingi.
Wilaya za watendaji weziwezi na wafanya biashara wabishi wabishi haziwezi

Wilaya za kazi na kusolve matatzo yanayotegemea viongozi wa serikali badoo ana ile ya kutaka kumridhisha kila mtu,Abaki tu kisarawe ama ateuliwe viti maalumu
 
Temeke hapawezi kabisaa,miongoni mwa wilaya zinazotaka uwe na maamuzi haswaaaa,Maana kwanza kuna viwanda vingi,bandari,wavuja jasho wengi,Wanafunzi wazazi wanaotegemea huduma Zaid za serikali kuanzia elimu, afya na maj.
Usafiri mkubwa ni daladala ,huku ni mtu ana nauli ya kwenda na kurudi tu humuelezi kitu.
Kila siku kusolve migogoro n.k
Jokate anaziweza wilaya ambazo bado Zina ushamba mwingi ili aweze waleta wasanii washangae shangae,event za kisanii Zaid kama mialiko kedekede,pichapicha nyingi.
Wilaya za watendaji weziwezi na wafanya biashara wabishi wabishi haziwezi

Wilaya za kazi na kusolve matatzo yanayotegemea viongozi wa serikali badoo ana ile ya kutaka kumridhisha kila mtu,Abaki tu kisarawe ama ateuliwe viti maalumu

Umekuza sana vitisho... huku uhalisia mkuu wa wilaya ya temeke wa sasa hivi hana competence yeyote ya kumzidi jokate.. kuanzia elimu mpaka mafanikio waliyoyaleta kwenye wilaya zao..

Yaani sehemu aweze muandishi wa habari ambays hata chuo kikuu hajafika, ashindwe binti mjanja mjanja mwenye degree na masters ya udsm + exposure ya kueleweka
 
Temeke hapawezi kabisaa,miongoni mwa wilaya zinazotaka uwe na maamuzi haswaaaa,Maana kwanza kuna viwanda vingi,bandari,wavuja jasho wengi,Wanafunzi wazazi wanaotegemea huduma Zaid za serikali kuanzia elimu, afya na maj.
Usafiri mkubwa ni daladala ,huku ni mtu ana nauli ya kwenda na kurudi tu humuelezi kitu.
Kila siku kusolve migogoro n.k
Jokate anaziweza wilaya ambazo bado Zina ushamba mwingi ili aweze waleta wasanii washangae shangae,event za kisanii Zaid kama mialiko kedekede,pichapicha nyingi.
Wilaya za watendaji weziwezi na wafanya biashara wabishi wabishi haziwezi

Wilaya za kazi na kusolve matatzo yanayotegemea viongozi wa serikali badoo ana ile ya kutaka kumridhisha kila mtu,Abaki tu kisarawe ama ateuliwe viti maalumu
Gondwe naona umeandika gazeti, jiandae kwenda kisarawe then Jokate aje Temeke
 
Back
Top Bottom