Katika gazeti la Raia Mwema toleo la Mei 13 - Mei 19, 2009, Mwandishi Johnson Mbwambo aliandika Makala yenye kichwa cha habari "Ya Profesa Watson na Urais wa kina Zuma".
Katika makala yake hii nilifurahishwa na mifano yake miwili aliyoitoa na ambayo inaonyesha wazi si tu jinsi viongozi wetu walivyo na akili finyu, bali pia wenzetu wenye akili timamu wanavyotushangaa. Nanukuu mifano hiyo hapa chini.
".........Nilitoa mifano kadhaa ukiwemo wa waziri wetu mmoja aliyekatiwa tiketi ya ndege ya daraja la kwanza wakati akienda Ulaya kutembeza bakuli la ombaomba kwa wafadhili , na kwamba katika ndege hiyo hiyo alipakia balozi wa nchi hiyo inayokwenda kuombwa misaada hiyo; lakini yeye akiwa daraja la tatu.
Nilitoa mfano mwingine wa Mzungu mmoja aliyetoa pesa zake Tsh. milioni 5 kwa ajili ya kujenga kisima cha maji katika kijiji kimoja nchini. Nilisema kwamba wakati wa uzinduzi wa kisima hicho, Mzungu alikwenda katika kijiji hicho kwa gari la kawaida kabisa Suzuki, lakini Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya husika yeye alikwenda kwenye sherehe hizo kwa gari la kifahari la Serikali aina ya Landcruiser VX! Nilisema kwamba Tsh. milioni 120 zilizotumika kununua gari lile zingeweza kujenga visima 24 kwa vijiji 24 vya Wilaya hiyo"! Mwisho wa kunukuu.
Jamani tutapata wapi viongozi wa kweli, ambao wana akili timamu, wasiopenda makuu? Au tuwarejeshe wazungu watutawale?
Naomba kuwakilisha.
Katika makala yake hii nilifurahishwa na mifano yake miwili aliyoitoa na ambayo inaonyesha wazi si tu jinsi viongozi wetu walivyo na akili finyu, bali pia wenzetu wenye akili timamu wanavyotushangaa. Nanukuu mifano hiyo hapa chini.
".........Nilitoa mifano kadhaa ukiwemo wa waziri wetu mmoja aliyekatiwa tiketi ya ndege ya daraja la kwanza wakati akienda Ulaya kutembeza bakuli la ombaomba kwa wafadhili , na kwamba katika ndege hiyo hiyo alipakia balozi wa nchi hiyo inayokwenda kuombwa misaada hiyo; lakini yeye akiwa daraja la tatu.
Nilitoa mfano mwingine wa Mzungu mmoja aliyetoa pesa zake Tsh. milioni 5 kwa ajili ya kujenga kisima cha maji katika kijiji kimoja nchini. Nilisema kwamba wakati wa uzinduzi wa kisima hicho, Mzungu alikwenda katika kijiji hicho kwa gari la kawaida kabisa Suzuki, lakini Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya husika yeye alikwenda kwenye sherehe hizo kwa gari la kifahari la Serikali aina ya Landcruiser VX! Nilisema kwamba Tsh. milioni 120 zilizotumika kununua gari lile zingeweza kujenga visima 24 kwa vijiji 24 vya Wilaya hiyo"! Mwisho wa kunukuu.
Jamani tutapata wapi viongozi wa kweli, ambao wana akili timamu, wasiopenda makuu? Au tuwarejeshe wazungu watutawale?
Naomba kuwakilisha.
Last edited: