John Shibuda: Mbowe ni dikteta

Haitatokea juu ya ardhi kiongozi akubaliwe na wote. Ni lazima kuwe na kutofautiana na inapotokea hivyo ni lazima kutumia kidogo ka elemene of dictatorship twende mbele as a team. Hata kwenye democrascy huwanyang'anya haki walio wachadche na kuwapa waliowengi na hao wachache wataishia kusema kulikuwa na dictatorship.


Mbowe anastahili pongezi na siyo kuomba msamaha.
 


Mbowe ndiyo kiongozi anayetakiwa kwa sasa CDM kwa kuna watu wanapewa vijisenti na mafisadi halafu wana leta choko choko kama Zito na wengine kwa hiyo lazima tuwe na kiongozi mwenye misimamo najua mafisadi wengi na matawi yao kama wewe hupendi lakini hakuna jinsi inabidi iwe hivyo kwa sasa hadi 2015 CDM itakapochukua nchi hii.

Embu ona MAFISADI, CUF, TLP, NCCR, UPDP, CCM, NEC, etc. wote hawa hawamtaki mbowe awe kiongozi wa CDM hivi si ukweli uko wazi hakuna kiongozi wa upinzani anayetaka mwenzake awe na mafanikio wanasahau ni watanzania ndio wanaofanya chadema iwe na mafanikio yanayoonekana.

Sisi wanachama wa chadema ndo tunafahamu chama chetu kinafanya nini.

Ukiwauliza wanataka nani awe mwenyekiti utasikia ZITO ndo anafaa, ukiuliza kwa nini utasikia ndio atamaliza issue ya udini. sasa udini uko wapi na kwa nini kiongo wa nchi hii akiwa muislamu hakuna udini lakini akiwa mkristi ni udini.

Mimi najua ukweli ni kwamba kuna watu wana maslahi binafsi na migogoro ya chadema na ukweli ni kwamba wameshindwa maana hata hela zao sasa zimepungu na miradi ya kupata hela kifisadi sasa imepungu tutawashinda tu hata kama hawataki.

Peoples Power, Songa mbele baba MBOWE na Slaa wananchi tupo pamoja nanyi.

WaTZ sasa hawadanganyiki tena.
 
asanteni kwa maoni yenu, mi nawatakia kila la heri 2015. Ila kumbukeni kuna zaidi ya nusu ya wa tz waliojindikisha kupiga kura lakini hawakupiga, kuna sababu nyingi zikiwemo za kutokua na imani na vyama husika pamoja na wagombea na wengine hatupo nchini ila tunafuatilia nini kinaendelea nyumbani. Asante kwa walionibeza na kuniita kibaraka ila kiukweli ni kwamba mi naipenda nchi yangu kwanza halafu chama kitafuata badae na pia nina haki ya kutoa mawazo yangu pamoja na ya wenzangu wenye msimamo na mitazamo kama yangu. Sina chama na bado sijakiamini chadema kwa asilimia zote. Buena suerte.
 

Kaka nadhani hoja yako ni nzuri ila haujajipanga vizuri maana citation yako haijitoshelezi na pia huna taarifa sahihi.

Kiongozi wa aina ya Mbowe anatakiwa kwa mazingira yetu (Tanzania) maana hatujaweza kwa hakika kusema nchi yetu ni ya kidemokrasia.
CDM chini ya Mbowe imetoka 5% votes hadi 26%(pamoja na uchakachuaji) na imeongeza idadi ya madiwani/wabunge pia.
Nchi yetu ikiwa na viongozi dhaifu inayumba kama ambavyo tumeona serikali ya awamu ya nne miaka 5 iliyopita.

Mimi binafsi ni shabiki wa madikteta wazuri kama Nyerere hivyo sitaona ajabu kama CDM ikiwa na dikteta mzuri.
 
Una uhakika gani kuwa nusu ya Watanzania waliojiandikisha kupiga kura hawakupiga kura? Una hakika gani kuwa kura zao hazikuGbagboliwa na tume ya uchaguzi? Ukishangaa ya Ivory Coast.....
 

We zoba watanzania walipiga kura kwa zaidi ya asilimia 70 ila ziliminywa ili ionekane watu hawakumpigua Slaa kura eti watanzania wanaoenda kwenye mikutano ya Dr slaa wanashangilia lakini hawapigi kura. Ukweli Rais aliyechaguliwa ni Dr Slaa ila Jk kaingia kwa mlango wa NEC na TISS hana tfauti na Gbagbo. Mwaka huu watu walihamasika kupiga kura kuliko miaka yote eti ndo turn out ikawa 42% kwangu mimi mwenye akili zinazoangalia nyuma ya pazia huwezi kunidanganya. Iweje hata miaka ambayo hakukuwa na hamasa ya kupiga kura kama mwaka huu turnout ilikuwa zaidi ya 70%?
Mbowe ni kiongozi mzuri kabisa na mwenye kujitolea. Niambie kiongozi yeyote wa upinzani anayejitolea kama mbowe. Nani? Mbowe is the best if not Dr. Slaa.
 

Una uhakika watazania hawakupiga kura? unaupata wapo huu ukweli? Kama unakumbuka vyama vya upinzani vilidai daftari la wapiga kura liwekwe wazi lakini Tume ya uchaguzi likaguoma kufanya hivyo. Tukaambiwa na Tume kuwa wapiga kura wapo milioni 20 (kati ya Watanzania milioni 40). Ina maana 50% ya watanzania ni wapiga kura?

Wakati wa matokeo waliopiga kura walionekana milioni 8. Nani alikuwa na uhakika wa wapiga kura wa Tanzania katika uchakachuaji wa NEC wa namna ile?
 
Una uhakika gani kuwa nusu ya Watanzania waliojiandikisha kupiga kura hawakupiga kura? Una hakika gani kuwa kura zao hazikuGbagboliwa na tume ya uchaguzi? Ukishangaa ya Ivory Coast.....
Du sio kuchakachua kura tena bali gbagboliwa kura!!!
 
nasikitika kuona ndg zangu wa kigoma kuwa wanachagua viongozi wao wanaowapenda mwishoe wanaonekana manunuzi kwa chama tawala kwa kuwanunua ivo basi inaonekana kuwa viongozi hao ni makahaba walioshindika wanaliwa na ccm,angalia aman kaboru na zito,zito kabwe amenunuliwa nyumba mbeazi beach na kimara n mme wake rostam.angalia sasa uyo kabachori ambae hana mahali pa kulala muda wote anishi kwa kuogopa.
 
hivi kumbe historia ya watu wa kigoma kumbe ni manunuzi kwa chama tawala,kumbe hawana lolote wamefirisika kimawazo wamepitwa na muda,zito katumiwa na mafisadi kufuruga chama,watanzania tunajisaliti wenyewe hebu angalia serikali ilivyovunja mkataba wa dowans afu leo hii inaambiwa lipe mabikioni pesa,je ofsi ya mwanasheria mkuu ina kazi gani au dowans ni deal ya kupata pesa kwa ajili ya uchaguzi 2015,siami ilo waziri mkuu tuna mashaka na wewe kumbe na wewe unasemw hauna jinsi na kampuni ambayo hamjui mmliki wake afu mnamlipa mtu ambae hamjui,fikiria vizuri kwa maisha ya watanzania.
 

Kama sisi letu moja na kama ni kweli hatuna ukombozi wa kweli kwa tz,Je?,tungeifikisha CDM hapa ilipo kiasi cha kukubalika sana na waTz hadi idadi yake ya wabunge ikaongezeka kuizidi hata CUF?,na pia kutengeneza sera ya msingi ya mabadiliko ya katiba ya kuja kukubalika na watu wote na kuishawishi serikali kwa nguvu zote?.Na yote hayo mabadiliko yametokea CDM ikiwa chini ya huyohuyo Mbowe unayemhisi vibaya.
MY DEAR BRUCE LEE,THINK TWICE,DEEPLY AND CLEAR.CHANGE YOUR MIND.
 

poor mind
 
Tusidanganyike mbowe ni kiongozi makini na ndio maana cdm inapendwa,kama unafikiri kuongoza chama ni lelemama waulize ccj,au anzisha na wewe ili utekeleze huo utawala usio wa kidikteta
 
CRAP........... hivi unamjua vizuri mtu unayemtetea???????? siku ukija kumjua vizuri utakuwa ushachelewa.pole saaana
 
Notradamme hukulazimishwa kuwa cdm,vyama ni vingi na ni hiari chagua kinachokufaa ujiunge achana na cdm, tumechoka bwana na spins zetu aahk...!
 
Mtaji wa CHADEMA ni Dr Slaa na Zitto tu, bila hao CDM kwisney bana.
 
Ugonjwa waliokuwa nao CUF sasa umerithiwa na CHADEMA. Maalim Seif kwa CUF hakosei na kwa CHADEMA ni hivyo hivyo Mbowe ni malaika hana kosa. Tujitahidi kuchanganua mambo bila hivyo tutamalizana.
 

KIoNGOZI YEYOTE LAZIMA UWE NA VIELEMENT VYA KIDIKTETA OTHERWISE UTAKUWA UNACHEKA TUU KAMA JEYKEI.LAZIMA UDIKTETA KAMA BEN MKAPA.KAZA BUTI MBOWE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…