John Mnyika: Pinda ni muongo

John Mnyika: Pinda ni muongo

Ili Tuendelee tunahitaji vitu 4
1. watu
2. Ardhi
3. Siasa safi
4. Uongozi Bora
Kwa sasa Taifa linaangamia Siasa safi na Uongozi Bora vimepotea na haya yanayotokea tumeyataka wenyewe kwani hata baba wa Taifa angefufuka Leo angetulaumu sana kwa kumchagua mtu ambaye hakuwa Chaguo lake.

kibogo, shirikisha ubongo wako vizuri. tofautisha kati ya "reported speech" na "speech"
"ILI TUENDELEE TUNAHITAJI WATU WENYE AKILI" haya ni maneno yangu.

zingatia:-
hakuna nchi isiyo na ardhi,
hakuna nchi isiyo na watu,
bali nchi zenye watu wajinga zimefanywa mtaji wa nchi zenye watu wenye akili.
 
Last edited by a moderator:
Pinda anatumia jina la mtoto wa mkulima kwa kuwahadaa watanzania! Pinda ni kawaida yake kusema uwongo bungeni, nakumbuka kisa cha Arusha na lema!
 
nampongeza sana mbunge wa ubungo, john mnyika kwa kumuumbua waziri mkuu, mizengo pinda juu ya uongo wake kwa taifa kuhusu mapendekezo ya mabadiliko ya katiba mpya yaliyowasilishwa na chadema.
Nami nathibitisha pinda ni muongo kinoma!

ndiyo umegundua sasa ivi huyu pm sijui akoje ahaa anafaa waziri asiekua na wizara maalum
 
:high5:
Eti mtoto wa mkulima, mtoto wa mkulima mjinga kiasi hiki mnafiki kazi yake kulialia tu wakati yeye ndiyo kiongozi wa serikali, watoto wa wakulima/ wafungaji walikuwa akina Sokoine siyo huyu mpuuzi...

Ahhh Kamanda unamfananisha huyu na Sokoine? Hamna kitu hapo.
 
Mnyika alishika pabaya kwa PM. Madame Speaker akaikaushia eti leo atajibiwa. Angemruhusu PM ajiume ume kama ilivyokuwa kawaida yake. Na jana bila shaka PM alimshukuru tena Madame

View attachment 90291
 
Wewe umeweka post ya Pinda na weledi wa Mbowe. Kama unaangalia bunge au upo bungeni guambie wewe kasemaje.

Au unajua kujamba tu kwasababu harufu huisikii kutokana na usugu wa magamba ya makamasi puani.

Duu? staha haiuzwi madukani hizo kashfa zote za nini?
 
attachment.php


Hawa viongozi wetu wakifanya mambo flani wanaweza kutoa product inayoweza kuwa kivutio cha utalii.
 
PM kusema uongo siyo mara ya kwanza hata ile issue ya arusa he did the same...tumeshamzoea wakimtait sana kitu cha chozi ndiyo mpango mzima
 
Unampongeza amekupa nn mkuu..weka hapa maelezo ya mh Mnyika tujue ili tuchangie

Mvutano kuhusiana na mchakato wa kupata Katiba Mpya unaozigonganisha Serikali na Chadema ulizidi kupamba moto bungeni jana wakati wa mjadala wa kuhitimisha hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu.



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana alitumia muda wake karibu wote wa saa moja kujibu maoni na kumshambulia Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe aliyoyatoa kuhusu hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu.


Hoja za Mbowe zilizoonekana kumsumbua Pinda ni malalamiko dhidi ya Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kauli yake kwamba serikalini hakuna weledi wa kuwezesha kupanga mipango ya maendeleo.


Hata hivyo, baada ya kuhitimisha hotuba hiyo, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika alisimama kuomba mwongozo wa Spika chini ya kanuni ya 68 (7) akidai kuwa Pinda alikuwa ametoa kauli ya uongo kuwa Chadema haikuwasilisha mapendekezo yake juu ya muundo wa Mabaraza ya Katiba, badala yake walilalamika tu kwenye mkutano wa hadhara.


Akizungumzia, Pinda alieleza kumshangaa Mbowe kwa kudai kuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba haina weledi wakati kuna maprofesa na kati ya hao ni Profesa Mwesiga Baregu wa Chadema.


“Hivi kweli hawa wazee na maprofesa ni mambumbumbu kweli au ni kauli ambayo hakuipangilia. Haiwezekani kwa mjumuiko wa wazee wote waliomo mle ndani."


“Tuwatendee haki Watanzania na tusiwakatishe tamaa wazee wetu ambao wamezunguka nchi nzima na kufanya kazi kubwa, kama haya ndiyo Mbowe ametumwa basi nadhani aliteleza.”


Pinda alisema kama kuna tatizo kwenye mchakato ni kutokana na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba iliyopitishwa na Bunge.


Wakati anazungumzia suala hilo ilisikika sauti kuwa wakati sheria hiyo inapitishwa Chadema walitoka bungeni, na Pinda alirudia, “Nasikia kuwa mlitoka bungeni.”


Pinda alisema kutakuwa na Bunge la Katiba na wabunge wote ni wajumbe, pia kwa Zanzibar kuna Baraza la Wawakilishi, hivyo Mbowe kuanza kutoa maoni hayo inaonyesha wana hofu.


“Kama Chadema wana hofu basi ni jambo lingine, nilipoisoma `speech’ (hotuba) ya Mbowe mawazo yake yanaonyesha anawaza uchaguzi wa 2015 na si kitu kingine,” alisema Pinda na kupigiwa makofi na wabunge wa CCM.


Alisema Mbowe alimtisha zaidi pale aliposema kuwa wataitisha maandamano nchi nzima kupinga suala hilo, kitu ambacho si sawa.
 
Nampongeza sana Mbunge wa Ubungo, John Mnyika kwa kumuumbua Waziri Mkuu, Mizengo Pinda juu ya uongo wake kwa Taifa kuhusu mapendekezo ya Mabadiliko ya Katiba Mpya yaliyowasilishwa na CHADEMA.
Nami nathibitisha Pinda ni Muongo kinoma!

Pinda ni kati ya 'matatizo makuu ya tanzania na uongozi kwa future ya taifa letu'...this is serious! This is a very fake and self unconscious leader (PM) this beautiful country had unfortunately ever have.

Uongo kwake sio issue, ni 'hali halisi', na anaweza kulia machozi ili muone kuwa yupo passionate na aloliongea au kulijali...kumbe, ni 'Funika Kombe, Mwanaharamu apite' - by Filikunjombe!

Matekeo ya worst performance ya Cabinet nzima ni sababu ya opacity/lack of transparency ya huyu jamaa only, period!
 
attachment.php


Hawa viongozi wetu wakifanya mambo flani wanaweza kutoa product inayoweza kuwa kivutio cha utalii.


Hiki ki-bonzo cha 'Bi KiRoBoTo' na 'Zero - Mtoa chozi muongo' chaweza kuwa kumbukumbu nzuri sana kwa historia ya watoto wetu na mwelekeo wa siasa zinazokufa za watawala tanganyika! Kamebeba ujumbe muhimu saaaana!

ANGALIZO: Tukiweke ktk diary zetu, katatusaidia kuwaelimisha watoto wetu siku sii nyingi...! Tutajajikumbusha na siye!
 
Wewe umeweka post ya Pinda na weledi wa Mbowe. Kama unaangalia bunge au upo bungeni guambie wewe kasemaje.

Au unajua kujamba tu kwasababu harufu huisikii kutokana na usugu wa magamba ya makamasi puani.
Hee! Naona mbunge wa Zanzibar kawapa msamiati wa kujamba. Ululuu!


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom