John Mallya: Fatma Karume ndio zawadi kubwa ambayo wajumbe wa TLS wanaweza kujipa wenyewe

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Wakili Stadi, Mtoto wa Rais na mjukuu wa mpigania Uhuru anayewania kurithi kiti cha Tundu Lissu kwenye nafasi ya Urais wa Tanganyika Law Society.

Kama alivyo mtangulizi wake (Lissu), Fatma ni Mwanasheria anayeumizwa na uvunjifu wa katiba, uonevu na ukandamizaji wa haki za kiraia, hivyo daima amekuwa mstari wa mbele kutetea haki hizo Mahakamani na kusema kweli yeye ndiye Wakili kinara Mwanamke kwenye harakati za usawa wa kisheria; hivyo basi ni haki kusema Fatma ni kielelezo cha uwezo wa wanawake!

Ni mama ambaye akina baba wote tunapaswa kujivunia kwa kuzingatia ujasiri wake uliojaa tumaini.

Mitihani mingi iliyomtokea Fatma imewahi pia mtokea Mwanamke mwingine wa ki-Islam na binti wa kiongozi wa zamani (Kama alivyo Fatma) Benazir Buttho:

-Wote wawili, Baba zao wamekuwa viongozi wa juu kabisa katika nchi huru.
-Baba yake Benazir kama ilivyo kwa Babu yake Fatma aliuwawa kwa sababu za kisiasa.
-Wote wawili, ofisi zao zimewahi kulipuliwa na bomu.
-Wote wawili ni wapigania haki za raia kupitia majukwaa tofauti.

Na kwa mtiririko huo, kwakuwa Benazir amekuwa Waziri Mkuu nchini Pakistan, Fatma atakuwa Rais wa TLS, na pengine Rais wa nafasi nyingine kubwa zaidi inshā'allāh.

Kwa historia yake (lakini si kwa makuzi yake) Fatma angeweza jiungab na waminya haki na demokrasia, angekaa kimya na kufaidika na namna mambo yalivyo. Jina la Babu yake linaimbwa kwenye nyimbo za Taifa, sura ya Babu yake ipo kama picha kwenye vipande vya pesa halali za Tanzania; Hata hivyo hivi vyote havitoshi kumfanya Fatma kukaa kimya na kuridhika, anataka kuona Mahakama zinaheshimiwa, Sheria zinafuatwa, Katiba inalindwa na haki za raia hazitoweshwi na viongozi wasiojua miiko ya kisheria ya ukubwa wa mamlaka zao.

Mbadilishano wa madaraka kutoka Tundu Lissu kwenda Fatma Karume ndio zawadi kubwa ambayo wajumbe wa TLS wanaweza kujipa wenyewe na wananchi (wateja wao) wakafaidika nayo na kuifurahia.

Mimi namchagua Fatma.

John Mallya, Esquire
Wakili.
 
Mada nzuri ila sioni kwa nini umeamua kumhusisha na familia ya wazazi wake,huyu ni wakili makini na unajenga brand yake kama yeye hawezi kuendelea kuwa chini ya kivuli cha baba yake,good luck
 
Huyu mama Fatuma karume yeye peke yake ni sawa na Serikali nzima ya mapinduzi Zanzibar anajitambua mno, huyu ndiye atawaletea ukombozi wa kweli wa nchi yao wazanzibar
Truee kabisa, maana Viongozi waliopo sasa hivi wanafanya kuambiwa tu kutoka Dodoma, Muungano hauwanufaishi lakini wao wapo wapo tu.
 
Kwn Tanganyika nzima hakuna mtanganyika WA kuongoza Tanganyika law society?
Hilo swali wanatakiwa wajibu sababu wao ndio waligoma kabisa chama chao Kuitwa Tanzania Law society wakagoma kujiita Tanzania ili waonekane wapigania Tanganyika .Mtihani wao huo watachagua mtanganyika au mzanzibari? Kule Zanzibar wana chama chao cha wanasheria mtanganyika haruhusiwi kugombea.Sasa tuone hawa wanasheria wa Tanganyika wana ujali utanganyika au ni utapeli tu wa kiuanasheria kujiita Tanganyika Law society wakati hawana utanganyika hata chembe ni kutapeli tu watanganyika
 
Anaandika Wakili Msomi John Mallya

Fatma Binti Karume:

Wakili Stadi, Mtoto wa Rais na mjukuu wa mpigania Uhuru anayewania kurithi kiti cha Tundu Lissu kwenye nafasi ya Urais wa Tanganyika Law Society.

Kama alivyo mtangulizi wake (Lissu), Fatma ni Mwanasheria anayeumizwa na uvunjifu wa katiba, uonevu na ukandamizaji wa haki za kiraia, hivyo daima amekuwa mstari wa mbele kutetea haki hizo Mahakamani na kusema kweli yeye ndiye Wakili kinara Mwanamke kwenye harakati za usawa wa kisheria; hivyo basi ni haki kusema Fatma ni kielelezo cha uwezo wa wanawake!

Ni mama ambaye akina baba wote tunapaswa kujivunia kwa kuzingatia ujasiri wake uliojaa tumaini.

Mitihani mingi iliyomtokea Fatma imewahi pia mtokea Mwanamke mwingine wa ki-Islam na binti wa kiongozi wa zamani (Kama alivyo Fatma) Benazir Buttho:

-Wote wawili, Baba zao wamekuwa viongozi wa juu kabisa katika nchi huru.
-Baba yake Benazir kama ilivyo kwa Babu yake Fatma aliuwawa kwa sababu za kisiasa.
-Wote wawili, ofisi zao zimewahi kulipuliwa na bomu.
-Wote wawili ni wapigania haki za raia kupitia majukwaa tofauti.

Na kwa mtiririko huo, kwakuwa Benazir amekuwa Waziri Mkuu nchini Pakistan, Fatma atakuwa Rais wa TLS, na pengine Rais wa nafasi nyingine kubwa zaidi inshā'allāh.

Kwa historia yake (lakini si kwa makuzi yake) Fatma angeweza jiungab na waminya haki na demokrasia, angekaa kimya na kufaidika na namna mambo yalivyo. Jina la Babu yake linaimbwa kwenye nyimbo za Taifa, sura ya Babu yake ipo kama picha kwenye vipande vya pesa halali za Tanzania; Hata hivyo hivi vyote havitoshi kumfanya Fatma kukaa kimya na kuridhika, anataka kuona Mahakama zinaheshimiwa, Sheria zinafuatwa, Katiba inalindwa na haki za raia hazitoweshwi na viongozi wasiojua miiko ya kisheria ya ukubwa wa mamlaka zao.

Mbadilishano wa madaraka kutoka Tundu Lissu kwenda Fatma Karume ndio zawadi kubwa ambayo wajumbe wa TLS wanaweza kujipa wenyewe na wananchi (wateja wao) wakafaidika nayo na kuifurahia.

Mimi namchagua Fatma.

John Mallya, Esquire
Wakili.
 
Nilikujua ukiwa mwanafunzi wa sharia Tudarco tulitofautiana kisiasa ila sio kichama kwa ili nakubaliana nawewe
 
Back
Top Bottom