Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,411
Ndugu Watanzania!
Mwanasheria Mkuu wa Serikali amemshtaki wakili Boniface Kajunjumele Mwabukusi katika Kamati ya Mawakili kwa tuhuma za kuwasema Waziri Mkuu, Spika, Waziri Mbarawa na Katibu wake Mkuu, Bunge na Wabunge kuhusiana na suala la Bandari ambapo Mwabukusi alisema pia baadhi ya viongozi hao waachie nafasi zao.
Sisi Askofu Mwamakula tuna hofu kuwa kuna njama za kutaka kumnyang'anya leseni ya uwakili kama ilivyokuwa kwa Fatma Karume. Na kwa sababu hiyo, tuliita taarifa za Wajumbe wa Kamati hiyo na kuletewa maelezo yafuatayo kwa kila Mjumbe:
1. Jaji Ntemi Kilekamejenga. Ni Mwenyekiti wa wa Kamati na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba. Ni Mteule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni mtu wa karibu sana au ndugu wa damu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Feleshi, na kwamba uteuzi wa Jaji Ntemi ulitokana na 'connection' ya Feleshi kwa Rais Magufuli.
2. Dkt. Eliezer Feleshi ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mjumbe wa Kamati ya Mawakili. Huyu ndiye Sheria inamtaka apange vikao vya Kamati. Ndiye Mlalamikaji dhidi ya Mwabukusi ndiye alifanya press kufafanua Mkataba wa Bandari kama Mwanasheria Mkuu. Ndiye pia alimsimamisha wakili Fatma Karume kwenye kesi ya ADO SHAIBU v. RAIS MAGUFULI & AG KILANGI wakati huo Dkt. Feleshi akiwa Jaji Kiongozi. Kamawanasheria Mkuu wa Serikali kwa sasa anawajibika kuitetea Serikali na maamuzi yake yote ima fa ima. Ndiye mshauri wa Serikali kwa mambo yote ya mikataba, hata mkataba wa DPW anautetea.
3. Dkt. Evaristo Longopa ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Ni Msaidizi wa Dkt. Feleshi na anawajibika kwa Feleshi. Ni Mteule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na anawajibika kuitetea Serikali na maamuzi yake Malalamiko wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya wakili Mwabukusi yana kibali na ridhaa yake pia kwa kuzingatia dhana ile ya 'collective responsibility.'
4. Sylvester A. Mwakitalu. Ndiye Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP).
Ni Mteule wa Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania na hivyo anawajibika kwa Rais na Serikali na kuwajibika kuitetea Serikali na maamuzi yake ili kulinda ajira yake.
5. Adv. Victoria B. Mandari.
Ndiye mtu pekee katika Kamati hiyo ambaye hatokani na serikali. Ni Wakili wa Kujitegemea aliyependekezwa na Tanganyika Law Society (TLS) kuwa Mjumbe wa Kamati hii. Anawajibika kulinda na kutetea maslahi ya Mawakili wa Kujitegemea katika mazingira ya mashtaka yao ndani ya Kamati. Kura yake ni moja tu ndani ya Kamati. Yeye hana uwezo wa kubadilisha msimamo kama wajumbe wenzake wakiazimia na kuungana kumnyanyasa wakili yeyote.
6. Faraji R. Ngukah ni Wakili wa Serikali (State Attorney).
Ni mwajiriwa wa Serikali anawajibika na kusimamiwa na Mwanasheria Mkuu Dkt. Feleshi. Mamlaka yake ya nidhamu ni Naibu Mwanasheria Mkuu Dkt. Evaristo Longopa ambaye naye anawajibika kwa Dkt. Feleshi.
Analipwa mshahara wa Serikali kwa kazi ya kuitetea Serikali. Hivyo anawajibika kuitetea Serikali ili kulinda ajira yake. Huyu ndiye Katibu wa Kamati aliyeandika barua kwa Mwabukusi kwa niaba ya Kamati. Kama Katibu, anawajibika kwa Wajumbe wa Kamati ambao 'majority' ni watu wenye mahusiano ya moja kwa moja na Serikali pia.
Ndugu Watanzania!
Kwa muktadha huo na katika mazingira hayo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Feleshi amelalamika kwenye Kamati ya ndugu zake na kisha yeye atatoa ratiba za vikao ili kumjadili wakili Boniface Kajunjumele Mwabukusi kwa tuhuma za Feleshi mwenyewe.
Wakili Mwabukusi aliongea mambo yaliyo na maslahi mapana kwa taifa letu na hivyo hata mashtaka dhidi yake yana maslahi mapana kwa taifa letu. Ni kwa sababu hiyo, sisi Askofu Mwamakula tunalileta kwenu Watanzania ili muamue kama katika mazingira hayo, wakili Boniface Kajunjumele Mwabukusi atapata fair trial au hukumu ya haki.
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 1 Agosti 2023; 08:54 mchana.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali amemshtaki wakili Boniface Kajunjumele Mwabukusi katika Kamati ya Mawakili kwa tuhuma za kuwasema Waziri Mkuu, Spika, Waziri Mbarawa na Katibu wake Mkuu, Bunge na Wabunge kuhusiana na suala la Bandari ambapo Mwabukusi alisema pia baadhi ya viongozi hao waachie nafasi zao.
Sisi Askofu Mwamakula tuna hofu kuwa kuna njama za kutaka kumnyang'anya leseni ya uwakili kama ilivyokuwa kwa Fatma Karume. Na kwa sababu hiyo, tuliita taarifa za Wajumbe wa Kamati hiyo na kuletewa maelezo yafuatayo kwa kila Mjumbe:
1. Jaji Ntemi Kilekamejenga. Ni Mwenyekiti wa wa Kamati na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba. Ni Mteule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni mtu wa karibu sana au ndugu wa damu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Feleshi, na kwamba uteuzi wa Jaji Ntemi ulitokana na 'connection' ya Feleshi kwa Rais Magufuli.
2. Dkt. Eliezer Feleshi ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mjumbe wa Kamati ya Mawakili. Huyu ndiye Sheria inamtaka apange vikao vya Kamati. Ndiye Mlalamikaji dhidi ya Mwabukusi ndiye alifanya press kufafanua Mkataba wa Bandari kama Mwanasheria Mkuu. Ndiye pia alimsimamisha wakili Fatma Karume kwenye kesi ya ADO SHAIBU v. RAIS MAGUFULI & AG KILANGI wakati huo Dkt. Feleshi akiwa Jaji Kiongozi. Kamawanasheria Mkuu wa Serikali kwa sasa anawajibika kuitetea Serikali na maamuzi yake yote ima fa ima. Ndiye mshauri wa Serikali kwa mambo yote ya mikataba, hata mkataba wa DPW anautetea.
Ndiye alikuwa Mshtakiwa Namba moja kwenye Kesi ya Bandari ambayo wakili Mwabukusi alikuwa anaendesha kule Mbeya. Dkt. Feleshi aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kabla ya uteuzi wake kuwa Jaji.
3. Dkt. Evaristo Longopa ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Ni Msaidizi wa Dkt. Feleshi na anawajibika kwa Feleshi. Ni Mteule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na anawajibika kuitetea Serikali na maamuzi yake Malalamiko wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya wakili Mwabukusi yana kibali na ridhaa yake pia kwa kuzingatia dhana ile ya 'collective responsibility.'
4. Sylvester A. Mwakitalu. Ndiye Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP).
Ni Mteule wa Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania na hivyo anawajibika kwa Rais na Serikali na kuwajibika kuitetea Serikali na maamuzi yake ili kulinda ajira yake.
5. Adv. Victoria B. Mandari.
Ndiye mtu pekee katika Kamati hiyo ambaye hatokani na serikali. Ni Wakili wa Kujitegemea aliyependekezwa na Tanganyika Law Society (TLS) kuwa Mjumbe wa Kamati hii. Anawajibika kulinda na kutetea maslahi ya Mawakili wa Kujitegemea katika mazingira ya mashtaka yao ndani ya Kamati. Kura yake ni moja tu ndani ya Kamati. Yeye hana uwezo wa kubadilisha msimamo kama wajumbe wenzake wakiazimia na kuungana kumnyanyasa wakili yeyote.
6. Faraji R. Ngukah ni Wakili wa Serikali (State Attorney).
Ni mwajiriwa wa Serikali anawajibika na kusimamiwa na Mwanasheria Mkuu Dkt. Feleshi. Mamlaka yake ya nidhamu ni Naibu Mwanasheria Mkuu Dkt. Evaristo Longopa ambaye naye anawajibika kwa Dkt. Feleshi.
Analipwa mshahara wa Serikali kwa kazi ya kuitetea Serikali. Hivyo anawajibika kuitetea Serikali ili kulinda ajira yake. Huyu ndiye Katibu wa Kamati aliyeandika barua kwa Mwabukusi kwa niaba ya Kamati. Kama Katibu, anawajibika kwa Wajumbe wa Kamati ambao 'majority' ni watu wenye mahusiano ya moja kwa moja na Serikali pia.
Ndugu Watanzania!
Kwa muktadha huo na katika mazingira hayo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Feleshi amelalamika kwenye Kamati ya ndugu zake na kisha yeye atatoa ratiba za vikao ili kumjadili wakili Boniface Kajunjumele Mwabukusi kwa tuhuma za Feleshi mwenyewe.
Wakili Mwabukusi aliongea mambo yaliyo na maslahi mapana kwa taifa letu na hivyo hata mashtaka dhidi yake yana maslahi mapana kwa taifa letu. Ni kwa sababu hiyo, sisi Askofu Mwamakula tunalileta kwenu Watanzania ili muamue kama katika mazingira hayo, wakili Boniface Kajunjumele Mwabukusi atapata fair trial au hukumu ya haki.
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 1 Agosti 2023; 08:54 mchana.