Hayawi hayawi sasa yamekuwa.Yule mwanasiasa mwandamizi ndani ya Ccm na serikali za awamu ya tatu na nne Mhandisi John Pombe Magufuli aichanganya kambi ya Lowassa akili baada ya kuamua kujitosa kugombea urais wa Tanzania 2015.Kabla ya kujitangaza alikuwa akitajwa kuwa atagombea ila jamii ilikuwa haina uhakika.Ni dhahiri sasa jamii imepata uhakika na kundi la Lowassa ambalo lilikuwa likijitapa kuwa litazigawa kura za kanda ya ziwa limekutwa na hali ya sintofahamu.
Ni vilio na simanzi katika viunga vya maeneo ya kujidai ya wanamtandao wa Lowassa kwasababu tangu awali katika watu waliokuwa wanawahofia ni pamoja na Magufuli.Mmoja wa vijana watiifu wa Lowassa alinukuliwa na chanzo kimoja cha habari kuwa hatua ya Magufuli kutangaza nia sasa hivi ni sawa na shambulio la kivita la kushtukiza.Alisema,"Sikia ndugu yangu hivi sasa mzee kachanganyikiwa,haamini kwasababu hakudhani kama Magufuli atagombea urais.Ni dhahiri sasa sherehe yetu ya kutangaza nia pale viwanja vya Sheikh Abeid imeingia doa".
Kutokana na hatua ya Magufuli kutangaza nia kumeamuliwa vikao vya dharura kuanza kufanyika maeneo ya Mbezi Beach,Regency Hotel,Sinza Madukani na Rose Garden.Wahusika wa vikao hivyo ni pamoja na Lawrence Masha,Daniel Nsanzugwako na mmoja wa wenyeviti wa Ccm kutoka mkoa wa Kanda ya Ziwa mwenye tabia ya kupenda kuvaa kofia aina ya kibalagashea.Hakika hii ni sudden attack.Tutajionea mengi sana.