Nilipoambiwa na Rafiki yangu mmoja ambaye amepangiwa kituo cha kazi kusini mwa Tanzania kule Gas inapochimbwa Mtwara aliniambia kama naenda niwe makini kuchagua usafiri mzuri, vile sikuwa na uzoefu kusafiri mikoa ya kusini alinipa option ya magari/kampuni kama 3hivi machinga, maning nice na jm luxury na kuniambia kati hizo akaniambia nenda kachukue tiketi za jm, nilimuulza mbona mabasi hayo ni mageni njia hii? Akanijibu "ah hawa jamaa wapo kwenye game /huduma muda mrefu"
Nilichokikuta kwenye mabasi njiani tukienda mtwara.
kwanza nilipenda matangazo ya awali safari inapoanza likiwemo la kufanya sala, pili jamaa wanakuwa smart kwenye uniform na mabasi yao, pia issue ya uchafu kwamba mtu ukila usitupe nje uchafu -hii nimeipenda ila kwa mfumo wa ndugu zangu watanzania bado inasumbua wengi maana mpaka mwisho wa safari niliona wengine wamepewa mifuko ya uchafu lakini wakawa wanatupa ndani.ya bus, lililonifurahisha jamaa wanakataza abilia kusimama kuwahi mlangoni kushuka kabla bus halijasimama, hii imekaa vyema maana tatizo laweza kutokea bila hodi, nk.
Mwisho nilimpa big up driver na conda wake kwa hali ile walikuwa na bus lenye namba T956 CGK.
IN TAKE yangu angalieni msije.kuwa nguvu za soda maana mkisha nogewa tu mnajisahau, kwani tulikuwa na scandinavia jamaa walikuwa wazuri sana maana.hata abilia 5 gari inasonga mbele.
Na je,.mmekuwa mbadala au ni kipindi then mnahama biashara.