JKT na Uzalendo; Uzalendo kwa Nani?

daaah kweli zamani JF ilikua na true great thinker...thread ya mwaka 2011 bado ina mashiko hadi...poor Tanzania
 
Bravo kwa mwanzisha topic,inawezekana isipate wachangiaji wengi hii tabia ya Watanzania kuchangia' topic pendwa' ambazo utamu wake ni wa muda tu.Topic ni nzuri kwani niyakuijenga Tanzania tunayotaka.

Jkt...jkaya k.'kwte Team
 
kuna mazungumzo mengi kuhusu kurejeshwa kwa mafunzo ya JKT na mara nyingi yamekuwa yakipigiwa debe na Television ya Chama Cha Mapinduzi kila uchao.

ukiwasikiliza watetezi wa hoja ya kurejea kwa JKT na wanapropaganda wengi wengine wanajenga hoja kwamba vijana wengi wamekosa uzalendo. kwamba vijana wengi si wabunifu tena na wanashinda vijiweni.

wana hoja. labda. ni kweli kwamba vijana wengi sasa wa vijijini na mijini wanashinda vijiweni. mbaya zaidi hata wale walio vijijini wanadanganyika kuwa neema iko mijini na matokeo yake wimbi kubwa la vijana kukimbilia mijini linazidi kuongezeka kila leo. lakini tusisahau kuwa kwa wale walioko vijijini wanayasikia maneno ya wakuu wa nchi...kwamba serikali haiwezi kuiamuru mvua inyeshe. kwa hiyo wale wenzangu na mimi walioko shamba wanaoamini katika kilimo imekula kwao. inabidi waje mijini. kwa hawa wa mijini na hasa waliopita skuli wao waliambiwa wataandaliwa ajira milioni moja. sijui ni wangapi hata sasa wana hizo ajira? nani atuthibitishie?

kinachonishangaza hapa ni hii dhana kwamba vijana wamekosa uzalendo. najiuliza kivipi? kwani uzalendo ni nini?

kwa mujibu wa kamusi yangu hapa, uzalendo ni ile tabia au hali ya mtu kuiunga mkono nchi yake kwa moyo na nguvu zake zote kiasi cha kuwa tayari kuitetea.

Maswali:

  1. wanaotuhumiwa kwa rushwa kubwa kubwa kama kagoda, dowans, na richmond? ni vijana? hawakupita jkt?
  2. wanaotuhumiwa kusafirisha wanyamapori kwenye ndege ni vijana? hawakupita jkt?
  3. wanaotuhumiwa kuuza dawa za kulevya leo ni vijana? hawakupita jkt?
  4. wanaolalamikiwa kuiingiza nchi katika mikataba mibovu ya madini ni vijana? hawakupita jkt?
kuna maswali mengi ya kujiuliza, lakini tuanze na hayo manne.

kwamba vijana sasa tunalaumiwa na hawa wazee waliopita jkt kwamba hatuna uzalendo, wakati wenyewe hawana hata harufu ya uzalendo.

why?

Nadhani ni siasa. Kwamba vijana tumechoka na kauli-mbiu za kila mwaka, miaka 50 baada ya uhuru bado tunaishi kwa kaulimbiu zisizokuwa na msaada kwetu.


Matokeo ya uchaguzi uliopita pia ni moja ya vichochezi vya suala hili kupigiwa debe. kwamba vijana wengi wameongoka kifikira. na kwa vitendo walikipinga waziwazi chama cha mapinduzi katika uchaguzi uliopita. na sasa ili kuwadhibiti vijana, ccm sasa wanakuja na mavi ya kale. ati JKT. kwamba wakawajaze vijana na fikra mgando za ccm.

Too late:

it will never work. kwa waliosoma physics wanajua Hooke's Law. Elastic material ikishavuka elasticity, basi inakuwa inaingia katika region tofauti kabisa inayoitwa deformation ambako huwa haiwezi tena kurejea katika original shape.

Vijana tumeshavuka Elastic Limit. Tuko kwenye Deformation point.

Kama motives za kurejea kwa JKT una lengo la kutujengea uzalendo kwa CCM....waanzilishi wa mpango huo mmefulia na hautafanikiwa. Kwa mara nyengine tena mmemshauri vibaya mkuu wa kaya.

Vinginenyo mtuambie............

kwa wizi huu, kwa rushwa hizi na hujuma hizi zinazofanywa na wazee walioko serikalini na waliopita JKT miaka hiyo, manataka kutufundisha uzalendo, nauliza hivi..........


Uzalendo kwa Nani?

Umeandika marefu sana siwezi kumaliza yote ila kifupi unaonekana si mzalendo.
 
Back
Top Bottom