kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,255
- 16,185
Mwili ulinisisimka nilivyoona na kusikia kuwa "askari" waliomaliza mafunzo ya JKT bila kupatiwa ajira rasmi wanataka kuandamana kuelekea Ikulu. Mmmh, nikasema sasa huu ni ukurasa mpya katika historia ya majeshi yetu hapa nchini.
Askari hawa wamepata wapi ujasiri wa kuandamana kwenda Ikulu kuonana na Amiri jeshi mkuu? nani yuko nyuma yao? utamaduni huu wameupata wapi?
Kwanini wasingeazia kwa Mkuu wa majeshi kwanza kabla ya kwenda kwa Amiri jeshi mkuu?. Kama kweli vijana hawa watafanikisha malalamiko yao kwa njia hii basi iko siku "kaka zao" pia walioko kambini wanaweza kufuata njia hii hii ya kudai malalamiko yao, maana inawezekana na wao wanayo malalamiko makubwa pengine kuzidi haya ya "wajukuu zao" yaani mchezo wa ndama wanaocheza mchezo wa kupigana ndani ya zizi unaweza kuamsha hamu na hamasa ya madume nayo kuanza kupigana. Hatua tunazoziona sasa dhidi yao ni jitihada za kuwatenganisha ndama kwa kuwatoa zizini na kuwavisha kamba shingoni na kuwafunga kwenye vigingi juani ili waache kucheza mchezo wao huu hatari kwa usalama wa zizi na ng'ombe wengine (give a dog a bad name and ......)
Ni vema suala la vijana hawa wa JKT lichambuliwe kwa kina bila kutoa majibu ya juujuu na ya hasira. Inavyoonekana malengo ya mafuzo yao ya JKT hayakueleweka vema kwao, au yuko mtu aliyekiuka maagano au yuko mtu nyuma yao anawashauri vibaya
Askari hawa wamepata wapi ujasiri wa kuandamana kwenda Ikulu kuonana na Amiri jeshi mkuu? nani yuko nyuma yao? utamaduni huu wameupata wapi?
Kwanini wasingeazia kwa Mkuu wa majeshi kwanza kabla ya kwenda kwa Amiri jeshi mkuu?. Kama kweli vijana hawa watafanikisha malalamiko yao kwa njia hii basi iko siku "kaka zao" pia walioko kambini wanaweza kufuata njia hii hii ya kudai malalamiko yao, maana inawezekana na wao wanayo malalamiko makubwa pengine kuzidi haya ya "wajukuu zao" yaani mchezo wa ndama wanaocheza mchezo wa kupigana ndani ya zizi unaweza kuamsha hamu na hamasa ya madume nayo kuanza kupigana. Hatua tunazoziona sasa dhidi yao ni jitihada za kuwatenganisha ndama kwa kuwatoa zizini na kuwavisha kamba shingoni na kuwafunga kwenye vigingi juani ili waache kucheza mchezo wao huu hatari kwa usalama wa zizi na ng'ombe wengine (give a dog a bad name and ......)
Ni vema suala la vijana hawa wa JKT lichambuliwe kwa kina bila kutoa majibu ya juujuu na ya hasira. Inavyoonekana malengo ya mafuzo yao ya JKT hayakueleweka vema kwao, au yuko mtu aliyekiuka maagano au yuko mtu nyuma yao anawashauri vibaya