Game Theory
Platinum Member
- Sep 5, 2006
- 8,545
- 835
Kuna habari kuwa anaweza kufa eidha leo au Jumapili
Mwananyamala Hosp mtamuua mama huyu!
Imeelezwa kuwa hali ya mwanamke mjamzito ambaye kiumbe chake kimefia tumboni tangu wiki iliyopita, bado ni tete, huku ndugu zake wakijitahidi kutafuta tiba ili kunusuru maisha yake.
Kwa mujibu wa dada mkubwa wa mgonjwa huyo ambaye hakuwa tayari kutaja jina lake kwa kuogopa kuendelea kukosa ushirikiano kutoka Hospitali ya Mwananyamala, alisema hali ya ndugu yao si nzuri.
Kusema kweli ndugu yetu bado hali yake si nzuri, maana hata hii (leo) jana tumerudi tena Hospitali ya Mwananyamala lakini hakuna tiba tuliyopata, alieleza.
Aliongeza kuwa hata jana walipokwenda na kumtafuta daktari wa kuwasaidia, aliwaeleza kuwa wasubiri muda wa wiki mbili waliopangiwa awali.
Alisema kutokana na majibu hayo, waliamua kurudi nyumbani na mgonjwa huyo huku wakijaribu kuwasiliana na ndugu wengine, ili kutafuta fedha kwa ajili ya kumpeleka katika hospitali binafsi.
Kwa sasa hatuna njia nyingine, kwa muda huu tunajaribu kukusanyana na kufanya kikao ili tumpeleke katika hospitali binafsi, kwani hatuwezi kukaa kwa wiki mbili, kwani hali yake ni mbaya, alisisitiza.
Hivi karibuni hospitali hiyo imekuwa ikigubikwa na tuhuma mbalimbali, ikiwa pamoja na kumbadilishia mwanamke mmoja mtoto na kumpa mfu.
http://www.darhotwire.com/home/news/2009/11/26/mwananyamala_hosp_mtamuua_mama_huyu.html