JK tazama mwezio huyu

Layman conclusions!! So what? Wewe Katibu Muhtasi wa REDET una nini cha maana zaidi ya kutaka KUWABEBA hao Mabosi wako! Ni mizigo ya moto hiyo! Haibebeki wala haishikiki! Waambie waende Mbeya wakafanye UTAFITI yale mawe yalikuwa na kilo ngapi! Naijua REDET vizuri kuliko wewe Kopitaipisti! Nimeishi hiyo mitaa tangu nikiwa darasa la nne na sasa nina 'mimvi' kibao! Nazijua siasa za UDSM kuliko wewe!

Ukitaka kujenga Hoja siku nyingine kusanya nguvu kwanza sio kukurupuka tu na kuwaambiwa wenzako ni mabingwa wa conclusions! Huu ni mjadala. Kinachotakiwa hapa ni Nguvu za Hoja na si Hoja za Nguvu unazotaka kutultea WEWE mtunza bustani wa Mukandala!

Ukweli ni kuwa ni vigumu kujenga hoja na mtu mwenye upeo wa ki-uchambuzi wa aina yako....

Tanzanianjema
 
Mkuu,

Nadhani wewe ndiye u can do better than your mediocrity generalization/conclusions nikilinganisha uliyoyaongea na aliyoongea FMES.

Inaingia kichwani kwa nani kusema waliotumia Magazeti walikuwa ni kina EL na RA kwa faida yao. Mtu ambaye alikuwa ANATARAJIWA kuchukua madaraka makubwa ya NCHI alikosa UWEZO wa kujua kwamba akina EL na RA walikuwa wanamtumia kupitia magazeti kujinufaisha wakati yeye hanufaiki chochote! Walichokuwa wanafanya EL na RA kwa asilimia 100 kilikuwa na baraka za JK! Basi.

Umetaja kuwa kuna watu walikataliwa kwa Uarabu wao, kwa Ukikongwe wao, kwa Uchapombe wao lakini unasahau kuna watu walitajwa kuwa ni 'wagonjwa' au wewe hukusikia au hukutaka kusikia au unajifanya hukusikia?

Hakuna mahali ambapo FMES amesema watu wote waliomuunga mkono JK walinunuliwa lakini TUNAAMINI watu wengi waliomuunga mkono JK walinunuliwa kwa bei taslimu (unapewa chako mapema) na wapo walionunuliwa kwa mkopo (ahadi za kupewa vyeo) au wewe unadhani fedha za EPA zilifukiwa kaburini?

Kwa taarifa yako SISI tunawajua kwa majina wasomi woote walionunuliwa pale UDSM! Kama wewe huwajui nyamaza kwa sababu wewe sio PRO wao! REDET ninayoijua mimi ni MALI ya Prof Mukandala ukubali usikubali. REDET ni Mukandala na Mukandala ni REDET! Hao wengine unaowasema ni vivuli tu! Ni mambo ya kawaida kabisa pale UD watu kujichukulia taasisi na kuzifanya ni za kwao. Anzia ESAURP ya Profesa Teddy Malyamkono, pitia Kijiji cha Sayansi na Teknolojia cha Profesa Shayo, nenda CEST ya Profesa Mwandosya, usisahau kupitia ESRF ya Profesa Wangwe. Pamoja na kwamba JK alikubalika wakati ule wa utafiti wa REDET lakini kuna 'chumvi' nyingi tu iliwekwa kumuongezea umaarufu. Suala la JK na Mukandala ni zaidi ya UKADA kama unavyotaka kudhihirisha. Hapa tunaonglea suala la USWAHIBA wao! NIPE nikupe. Waambie REDET leo waende wakafanye UTAFITI tena na UONE kama watatuletea matokeo SAHIHI! Hawajipendi? Au wako busy na kufanya tafiti za migomo ya wanafunzi wa vyuo, walimu, madaktari kwa sasa?

Umemtaja Profesa Chachage (RIP) kwamba alikuwa na mategemeo makubwa na JK! Hivi ni kweli kwamba akina Chachage na usomi wao uliotukuka, na tafiti zao zote walizofanya ni kweli kwamba waliamini JK PEKEE (BILA CCM yote) ndio mkombozi wa wanyonge? Unataka kuniambia Chachage naye alikuwa ni miongoni mwa watu waliomwona Salimu ni Mwarabu, Malecela ni Kikongwe, Kigoda ni Chapombe na JK ni Chaguo la Mungu? Binafsi ni mmoja wa watu ambao nilikuwa namheshimu sana Marehemu Chachage, lakini nilikuwa mmoja wa watu walioshitushwa na kitendo cha Profesa kuigeukia CCM! Kumbuka Marehemu alianguka hadi kupelekea kifo chake pale Kibaha akiwa anafanya kazi za CCM! Sipendi kusema mengi lakini inawezekana marehemu naye alikuwa na 'mkataba' fulani na CCM! Tumuache apumzike na amani huko aliko alifanya mengi ya maana kuliko yasiyo na maana.

Sio kina Chachage tu waliobadilika ETI kwa kumuona JK ni chaguo la Wanyonge. Bado tunazo kumbukumbu za kina Salva Rweyemamu, akina Jenerali Ulimwengu, akina Prince Bagenda, akina Gideon Shoo walivyoligeuza Gazeti la Rai na kuwa JUKWAA la kummaliza SAS na kumuinua JK! Katika hawa nadhani wapo walionufaika na wapo ambao hawajanufaika hadi leo! Jenerali Ulimwengu aliyekuwa na ushawishi na nguvu kubwa pale habari cooperation ALIKUBALI vipi kuuza 'utu' wa gazeti la RAI? Je na yeye 'alikopwa' na hajalipwa kama alivyolipwa Salva? Au majibu ya swali hilo ndio kuanzishwa RAIA MWEMA! Ni kweli kwamba Habari Cooperation ilikaribia kufilisika ndio ikaamua kutafuta 'mwekezaji' mpya RA? Jenerali alivyo mzoefu wa duru za siasa za Bongo, aliona ni sahihi kabisa kumuuzia RA kampuni yao? Nawasilisha.

Mkuu Gottee,

Heshima mbele sana bro, hakuna cha kuongeza hapo maana nyani amepigwa usoni tena mchana kweupeee, na ubarikiwe tu!

Tunawaambia lakini hawasikii, kwamba sio kazi rahisi kutetea mafisadi, maana hawateteeki wala hawasafishiki, na wale wote wanaowatetea mwisho wao utakuwa kama wa mafisadi yaani aibu ya milele!
 
Layman conclusions!! So what? Wewe Katibu Muhtasi wa REDET una nini cha maana zaidi ya kutaka KUWABEBA hao Mabosi wako! Ni mizigo ya moto hiyo! Haibebeki wala haishikiki! Waambie waende Mbeya wakafanye UTAFITI yale mawe yalikuwa na kilo ngapi! Naijua REDET vizuri kuliko wewe Kopitaipisti! Nimeishi hiyo mitaa tangu nikiwa darasa la nne na sasa nina 'mimvi' kibao! Nazijua siasa za UDSM kuliko wewe!

Ukitaka kujenga Hoja siku nyingine kusanya nguvu kwanza sio kukurupuka tu na kuwaambiwa wenzako ni mabingwa wa conclusions! Huu ni mjadala. Kinachotakiwa hapa ni Nguvu za Hoja na si Hoja za Nguvu unazotaka kutultea WEWE mtunza bustani wa Mukandala!


Ukitaka kumpiga nyani ni lazima usimuangalie usoni, yaani mkuu Gottee unanipa raha sana hapa, leo sina kazi tena, duh JF bwana ukifikiri umemaliza kuhesabu vichwa, unakumbushwa na hawa kina Gottee kuwa bado hujamaliza kuhesabu vyote!

Saafi sana, hoja hujibiwa kwa hoja!
 
And this is LAYMAN's analysis....jitahidi kutafuta ukweli zaidi ya kutegemea hizi onface conclusions...

Hoja zingine bwana, yaani huwezi amini zimetolewa na PHDs, duh kweli Tanzania tuna safari ndefu sana!
 
Ukweli ni kuwa ni vigumu kujenga hoja na mtu mwenye upeo wa ki-uchambuzi wa aina yako....

Bwa! ha! ha! ha! ha! unajua Mkulu Gottee, kwa kweli unanidai kesi ya bia bro maana sijawahi kuona this, mtu anapigwa mawe usoni bila huruma namna hii!

Oooh I Love it, maana this is fun, Where we Dare mwanangu!
 
Wazee kuna tetesi nimesikia kutoka kwa watu tofauti kuwa JK hata alipokuwa Wizara ya mambo ya nchi za nje ilikuwa zake kusita kuchukua au kupitisha maamuzi mazito na yanayoweza kuumiza watu ilikuwa sio rahisi kwake, mara nyingi alikuwa anamsukumia PS wake Mzee Luhanjo.....ni kweli hizi story?

Kama ni kweli inawezekana basi ndio maana ikabidi amchukue Mzee Luhanjo kwenda Ikulu na kama picha ni hiyo ndio maana tunaona msimamo hakuna au maamuzi ya ajabu kwenye masuala mengi kama EPA etc ....Tuabarisheni mnaojua zaidi.
 
Najua kuwa siku zote alipokua akisaifri na rais, ilikuwa lazima rais amngoje airport tena ndani ya ndege, kwa mara ya kwanza katika historia ya siasa duniani rais kumngoja waziri, only in Tanzania.
 
JK asikitishwa msafara wake kurushiwa mawe chunya

Rais Jakaya Kikwete amesikitishwa na kitendo cha wananchi wa Kijiji cha Kanga wilayani Chunya kuurushia mawe msafara wake na kuwajeruhi baadhi ya watu waliokuwa kwenye
msafara huo.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu wakati akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza(BBC) jana kufuatia habari kwamba msafara wa Rais Kikwete umeshambuliwa kwa mawe na wananchi wa kijiji hicho.

Rweyemamu alisema kuwa Rais Kikwete amesikitishwa na tukio hilo na kwamba lilitokea baada ya kushindwa kusimama na kuwasalimia wananchi wa kijiji hicho kwa kuwa muda haukuruhusu kufanya hivyo.
"Rais amesikitishwa kwa kuwa alishindwa kusimama na kuwasalimia wananchi, lakini pamoja na hayo mazingira ya jana asingeweza kusimama,"alisema Rwehemamu.

Alisema tukio hilo lilitokea baada ya saa 1:00 jioni na kwamba baadhi ya vijana waliurushia mawe msafara huo baada ya kuona Rais anawapita bila kusimama na kuwasalimia.

Habari na Salim Said na John Stephen
 
Wakati JK anapigwa mawe na watu waliomchagua, Tazameni mwenzie Obama leo St Louis amabako umati wa watu LAKI MOJA walikuwa wanamsikiliza

2i0ejvb.jpg


obamastlouis_Q_20081018135311.jpg

Obama rocks........whopeeeeeeeeeeeee
I love you Obama...oopps its me, Michelle
 
Alishindwa kuyazuia mawe kule Mbeya.
Alishindwa kusimamia ushindi wa chama chake huko Tarime.
Ameshindwa kuprovide anything kati ya alivyowaahidi wananchi ikiwemo maisha bora.
Ameshindwa kuwashughulikia mafisadi na sasa hadi vilema ni maadui wake.
Wild Card...Umesema eti unajuwa kuwa atawashughulikia watu wa EPA....Nyie si mlishafanya na maandamano ili kuipongeza ile hotuba yake ya Ki Fidel Castro? Ama unafikiri ilikuwa bahati mbaya?
OK....Weka vigezo vyako vya ubora kabla sijaendelea.

Kwa mgombea wa CCM kushindwa Tarime tunapaswa kumpongeza JK kwa kuacha DEMOCRACIA ichukue nafasi yake. Wala hakuna Rais yeyote duniani atakayekupa wewe au mwananchi mwingine yeyote maisha bora. Muhimu ni kuhakikisha Nchi ina AMANI, miundombinu inaboreshwa, huduma za kijamii zinaimarishwa,.....halafu watu kwa jitihada zao wenyewe wanajitafutia maisha bora. Haya kwa asiye kipofu anayaona yanafanyika.
 
Starting with an end in mind...good question Chuma.
Wadau,mbona swali halijibiwi?
I would take a crack at this ila,sina wa kumpendekeza.

Hivi nyie watu wazima na akili zenu mnadhani kura ndio inayomweka kiongozi wa kiafrika madarakani?Ingekuwa hivyo basi Kenya leo ingekuwa inaongozwa na ODM na Zimbabwe ingekuwa inaongozwa na MDC. Mafisadi hawatakubali chama kingine kichukue!Wapo tayari kuua kufanya kila kitu ili jambo hilo lisitokee. CCM hata waweke ndoo ya maji itashinda uchaguzi as long as hakuna fair election kura za polling station na zile zinazosomwa makao makuu ya tume always huwa zinatofautiana. (Tally)
 
Starting with an end in mind...good question Chuma.
Wadau,mbona swali halijibiwi?
I would take a crack at this ila,sina wa kumpendekeza.

Babaa Magofuli, naona amempeleka kwenye mapanki na bado anafanya vizuri?? tatizo mawazi ni kina nani sasa ila naweza kumpatia wa sheria awe Mwakyembe kwa sababu wabunge wa upinzani ndio watakaokuwa wengi basi Waziri wa dhahabu kiwira ampe Slaa hope atamake sure mikataba yote inapitiwa.

ila ni ngumu hakuna Mawaziri kabisa wote chokoraa afadhali atafute wote fresh from school tehetehetehe.....................................
 
Ukiwa na mtazamo wa kishabiki huwezi kuwa mchambuzi makini wa mambo kama haya. Huwezi ukaifananisha marekani na Tanzania. Tanzania kwa marekani ni kama Jimbo moja tu la Uchaguzi. Ni sawa na ulinganishe umaarufu wa Kepten Komba kwa JK.

Lakini kwa heshima ya kitaifa ilivyo, leo Obama akiwa rais atakuwa na heshima ile ile aliyonayo JK katika ngazi za kiutawala. Tofauti inayokuja hapa ni adhari ya utawala wa Marikani unaathiri Dunia nzima tofauti na Tanzania utawala wake ukiwa wa hovyo utamuathiri mtanzania mwenyewe.

kujua kuongea sana katika siasa haimaanishi utendaji, kwa kweli Obama ni muongeaji tena kwa mbwembwe taam taam lakini je ana nini kikubwa kinachothibitiasha kweli anaweza kuongoza America?

CHANGE what CHANGE? CHANGE haina tofauti na kusema ARI MPYA NGUVU MPYA NA KASI MPYA. tuombe JF idumu kwa miaka 4 ijayo ya Obama utaona hawa hawa mashabiki ndo watakuwa wapondaji wakubwa wa Obama, maana wengi wetu hapa ndo tulikuwa tunamsifu JK hivi sasa tumemgeuka na kumuona Fisadi.

Ujinga wa wamarikani wanadhani eti Obama akiwa Rais then wanakuwa na peace na Middle east attacks, wamechemka.

Clinton aliremba remba na Terrors wakakikuona cha moto TwinTowers. Magaidi huwa hayana rafiki ati. Hussein Obama atuambie yeye atawawekaje sawa hawa magaidi ili MMarekani aweze kutembea bila ulinzi huko mashariki ya kati.

Endeleaaa, mkuu, I am so sorry, nadhani umekurupuka na kuandika vitu bila kufikiria. Unaniaccuse kuhusu ushabiki, lakini hujakaa kuniuliza kwa nini ninamsupport Obama. Unafikiri ni kwa sababu Babake katoka nchi jirani au mweusi mwenzangu, or whatever. Hapana. Nimekuwa nikimfuatilia kwa karibu sana kila alichosema na kuandika. Swali langu: je we umefanya hivyo? umesoma vitabu vyake? Unajua philosophy yake?
1. Je unaelewa nyuma ya neno Change kuna maana gani? Ingekuwa ni neno tu mbona McCain alitumia neno Change pia lakini alishindwa kuwashawishi wapiga kura ikabidi atafute slogan nyingine?
Kama unataka kujua Obama ataleta mabadiliko gani hebu tembelea tovuti yake usome kwa makini papers zilizowekwa ambazo ni ndefu na zinaeleza kwa undani anatarajia kufanya nini. Unafiriki endorsement ya wanasiasa kama Kennedys na General Powell na Warren Buffet ni bure? These are highly intelligent people ambao wamepima na kujua kinachoendelea. If you have problems with Kikwete useme lakini usithubutu kufananisha watu wawili who are heaven and earth apart!
2. Kusema kwamba eti Tanzania ni ndogo (sijui kwa saizi) kuliko Marekani si hoja. Umaarufu wa Obama umevuka mpaka wa nchi yake, hebu nenda kaangalia kama JK atapata hata watu 10 akienda Berlin kuongea! Hata McCain hawezi kupata watu! Anachokifanya Obama na mvuto wake kwa watu ni phenomenon ambayo watu wengi wamekubali. JK
3. Kuhusu kupunguza ugaidi: sijawahi kusikia utumbo ulioutaja hapo juu kwamba eti wamarekani wanampigia kura Obama kwa sababu wanaamini eti itapunguza ugaidi?! Hiyo sijui umetoa wapi. Mpaka sasa katika polls zaidi ya nusu ya wamarekani wanampigia kura Obama kutokana na siasa zake za kiuchumi!

Sidhani kama JK anaelewa hata 1% ya kile anachofanya Obama and his vision.
 
Susuviri: Inakera sana watu wanapomfananisha Obama na JK. Tena ni aibu na ushamba vilevile, maana ni vitu viwili tofauti.

Maybe wanaangalie ile ya kupagawisha watu, hapa nakubaliana nao maana kwa kweli JK alipagawisha watu mno. Tofauti ni kwamba wale ambao wamepagawishwa na Obama wanajua kwa nini anawapagawisha na kwa nini wanampenda. Lakini wale ambao JK aliwapagawisha hawakuwa na sababu; ulikuwa ni uzuzu na ushambenga tu. Ndio maana ulikuwa ukiwauliza hivi kwa nini una-mind JK walikuwa wanabaki wakimumunya midomo, ndio maana hata leo anapoboa wamebaki kusonya!

In any case, JK and Obama are two different animals belonging to different kingdoms, phyla, classes and two distinct species!
 
Susuviri: Inakera sana watu wanapomfananisha Obama na JK. Tena ni aibu na ushamba vilevile, maana ni vitu viwili tofauti.

Maybe wanaangalie ile ya kupagawisha watu, hapa nakubaliana nao maana kwa kweli JK alipagawisha watu mno. Tofauti ni kwamba wale ambao wamepagawishwa na Obama wanajua kwa nini anawapagawisha na kwa nini wanampenda. Lakini wale ambao JK aliwapagawisha hawakuwa na sababu; ulikuwa ni uzuzu na ushambenga tu. Ndio maana ulikuwa ukiwauliza hivi kwa nini una-mind JK walikuwa wanabaki wakimumunya midomo, ndio maana hata leo anapoboa wamebaki kusonya!

In any case, JK and Obama are two different animals belonging to different kingdoms, phyla, classes and two distinct species!

exagerrated, on this case they are the same and will never be different.
 
Susuviri: Inakera sana watu wanapomfananisha Obama na JK. Tena ni aibu na ushamba vilevile, maana ni vitu viwili tofauti.

Maybe wanaangalie ile ya kupagawisha watu, hapa nakubaliana nao maana kwa kweli JK alipagawisha watu mno. Tofauti ni kwamba wale ambao wamepagawishwa na Obama wanajua kwa nini anawapagawisha na kwa nini wanampenda. Lakini wale ambao JK aliwapagawisha hawakuwa na sababu; ulikuwa ni uzuzu na ushambenga tu. Ndio maana ulikuwa ukiwauliza hivi kwa nini una-mind JK walikuwa wanabaki wakimumunya midomo, ndio maana hata leo anapoboa wamebaki kusonya!

In any case, JK and Obama are two different animals belonging to different kingdoms, phyla, classes and two distinct species!
Kitila,
Una jingine dhidi ya JK au ni huu URAIS wake tu? Watanzania kwa mamilioni hawakuliona lolote la maana kwa JK walibaki kumumunya midomo!
Lakini Tanzania ipo, na yeye ndiye RAIS wetu.
 
ameomba miaka 5 ya kwanza kuwalipa waliomsaidia jamani yeye alitumia fedha za watu kuingia ikulu including EPA..mnafikiri makene ataweza????????????
JF ni mashahidi mungu mpe baraka zako barakobama
 
Ukweli ni kuwa ni vigumu kujenga hoja na mtu mwenye upeo wa ki-uchambuzi wa aina yako....

Tanzanianjema

Huwezi kujenga hoja na 'a layman' as you concluded! Nami nasema siwezi kuongea na mtu ambaye ni lower than an *****, actually you are just a spoiled moron!
 
Originally Posted by Tanzanianjema
Ukweli ni kuwa ni vigumu kujenga hoja na mtu mwenye upeo wa ki-uchambuzi wa aina yako....

Tanzanianjema
!


Huwezi kujenga hoja na 'a layman' as you concluded! Nami nasema siwezi kuongea na mtu ambaye ni lower than an *****, actually you are just a spoiled moron!
 
kaka usemayo ni kweli. Hakuna kilicho maarufu kikadumu au kuisha kikiwa maarufu hivyo hivyo. Obama asome alama za nyakati kwa jk. Wa marekani wanategemea kuona real changes tena kwa kipindi kifupi sana ambacho siamini obama anavyojiuza kwao kweli ataweza kutimiza. Hapo ndipo atakapokuja kugeukwa na hao hao wanamshabikia sasa na kumuona ni mzushi tu kama vile leo tunavyomuona jk mzushi kwa watanzania.

Tunamuomba obama asidhani usa ni kama kenya au tanzania ambako unaeza ukaleta siasa za kihuni na watu wakakutizama tu.

Hakuna kitu kibaya kama watu kutarajia makubwa kuliko uwezo wako wa kuyatenda. Mkapa kamaliza fresh maana hakuna aliyetegemea anaweza kutimiza aliyokuwa ameahidi. Kwanza kila mtu aliamini hata urais hatouweza kwamba tungekuwa tunaongozwa na nyerere kupitia mkapa. Hiyo imemuwezesha kutulia na kuweza kujipanga na kutimiza zaidi ya 80% ya alivyotaka kufanya.

Obama asidhani itaendelea kuwa shangwe ki hivyo kila siku. Hizi shangwe zote zinaishia nov 4 baada ya hapo ni kiwango cha kazi tu kitaangaliwa. John anaaminika maana uwezo wa kazi anaaminika anao na ndo maana hata kwenye chama chake hakupata upinzani mkubwa. Kazi kwako obama na wanaokufagilia
mimi sioni tatizo kwa obama nadhani atakapo chaguliwa, umakini unakuwa kwa watendaji wa chini yake atakao wateuwa, tatizo la kikwete alitoa ahadi pasipo kuangalia kwa makini juu ya watendaji wa chini aliowachagua, matokeo yake kachagu watu wakuvuluga malengo yake, na kibaya zaidi akateua maswahiba ambao hata wanapovuluga malengo yake inamuwia vigumu kuwawajibisha
 
Back
Top Bottom