Ndugu wananchi,
Hivi kweli wanataka kutudanganya kuwa Rais wa nchi hakuwa anajua mgao huu wa pesa za ESCROW? Kama itathibitika kuwa hakuwa anajua basi Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa ameshindwa kazi yake.
Ninashawishika kuamini kuwa "dili" hili ni la ikulu 100%.
Tutayajua mengi tu. Kama siyo leo basi kesho na wahusika watakula aibu na fedheha yao....
Mkuu, Mkombzi benki katika akaunti ya Rwega tumeonyeshwa majina na kiasi cha mabilioni ya shilingi mafisadi walichovuna bila kupanda lakini huko Stanbiki kulikochezwa mchezo mkubwa..majina hayakuwekwa kwa sababu maalumu na hapo ndipo kuna ukakasi na kuna kipolo hapa…hapa siwezi kuawapa mzigo kamati ya Zitto sababu PCB ndio kujua kwa nini hayakuwekwa majina na badala yake imetokea acc tu
Udhaifu wake uko wazi kuanzia anapomteua waziri mkuu pamoja na baraza la mawaziri. Yani hajifunzi chochote kutokana na makosa ya huko nyuma? Kule kulikuwa na EPA mara akaingia RICHMOND akang'oka mwenye nywele nyeupe ingawa sio mzee, kisha OPERATION TOKOMEZA UJANGILI wakang'oka watu 3, sasa ESCROW huyo tena ni baba lao. Yani ina maana hakuna hata jambo moja JK alilojifunza kutoka kwenye EPA-----RICHMOND----OPERATION TOKOMEZA na sasa ESCROW? Angekuwa makini angekuwa ameshajifunza jambo ili kuzuia ESCROW. Je; huyu ni rais au ni dalali wa mafisadi?
ukweli ni kwamba JK yupo strong kiasi ambacho kila anayeharibu anabeba mzigo wake. na kwa sababu mitanzania mmezoea kuiba na hasa nyie mnaojiita wasomi (uchwara) dawa yenu nikuwaacha muumbuke tu kwenye jamii. kama utakumbuka mkapa alilia sana na prof simon mbilinyi baada ya wabunge kumshikia bango. ilifikia kipindi akaanza hata kuwatishia wanaccm wenzake kuwa hatawapitisha kwenye ubunge tena wakati wakuteuliwa.
big up Kikwete for this. hutaki, acha.
Hili lilijulikana miaka mingi, hata humu kulikuwa na mjadala mrefu kama alistahili kupewa nafasi ya kugombea tena awamu ya pili. Mjadala ule mrefu ulisababisha John Malecela atoe kauli kwamba MACCM "wana utaratibu wao wa kuachiana Rais aliyeko madarakani amalize awamu zake mbili" Kama 2010 wangemtosa au kama si wizi wa kura nchi yetu ingeyaepuka majanga mengi makubwa yaliyosababishwa na DHAIFU kuendelea kuwemo Ikulu.
Udhaifu wake uko wazi kuanzia anapomteua waziri mkuu pamoja na baraza la mawaziri. Yani hajifunzi chochote kutokana na makosa ya huko nyuma? Kule kulikuwa na EPA mara akaingia RICHMOND akang'oka mwenye nywele nyeupe ingawa sio mzee, kisha OPERATION TOKOMEZA UJANGILI wakang'oka watu 3, sasa ESCROW huyo tena ni baba lao. Yani ina maana hakuna hata jambo moja JK alilojifunza kutoka kwenye EPA-----RICHMOND----OPERATION TOKOMEZA na sasa ESCROW? Angekuwa makini angekuwa ameshajifunza jambo ili kuzuia ESCROW. Je; huyu ni rais au ni dalali wa mafisadi?